Pata jibu kamili kuhusu swali lako
Je kugusana na mwanamke ambaye unaruhusiwa kumuoa kama mkeo ukiwa na udhu je habatwilishii udhuu?
Kumgusa mwanamke ama mke hakuharibu udhu kwa maoni ya baadhi ya Maulamaa. Katika mapokezi ya Hadithi Mtume siku moja alikuwa nyumbani kwake. Sasa ikawa sehemu ambayo anasujudi mkewe Aisha alikuwa amelala na kuweka miguu yake. Hivyo akawa Mtume anamgusa miguu yake ili aondoke apate kusujudi.