picha

MTAMBUE MDUDU MBU ILI UWEZE KUJIKINGA NA UGONJWA WA MALARIA (yajuwe maajabu makubwa ya mdudu mbu)

Mbu ni katika wadudu wanaopatikana maeneo yenye joto hususan maeneo ynye hali ya hewa ya kitropik.

MTAMBUE MDUDU MBU ILI UWEZE KUJIKINGA NA UGONJWA WA MALARIA (yajuwe maajabu makubwa ya mdudu mbu)

PAMBANA NA MALARIA KWA KUMTAMBUA MDUDU MBU (MOSQUITO)

 

Mbu ni katika wadudu wanaopatikana maeneo yenye joto hususan maeneo ynye hali ya hewa ya kitropik. Mbu anafahamika kwa kuwa ndiye msambazaji mkubwa wa malaria pamoja na matende na ngiri maji. Chakula cha mbu ni maji, bakteria pamoja na damu. Mbu dume huweza kumjua mwanamke kwa kutumia sauti ya mbawa. Mbu ni katika wadudu wadogo lakini wana maajabu makubwa. Katika mkala hii tutaangalia kwa ufupi mambo matano kuhusu mbu.

 

Tofauti na kuwa mbu ni mdogo lakini anaweza kunyonya damu iliyokuwa nzito kuliko mwili wake. Yaani sawa na mtu mwenye uzito wa kilo 70 kula chakula chenye uzito wa kilo 100. mara mbu anaponyonya damu mwili wake huchukuwa mpaka siku tatu kuweza kuimeng’enya damu ile na kuimaliza. Baada ya hapo mbu atakwenda kunyonya damu tena. Itambulike kuwa chakula cha mbu ni bakteria, maji pamoja na damu. Mbu jike hula damu pindi anapotaka kutaga. Wataalamu wanaeleza kuwa kuna aina 2000 za mbu.

 

Kabla ya mbu kutaga mayai yake anaanza kupima ardhi kama ina majimaji pamoja na joto la kutosha kwa maisha ya mayai yake. Mbu hutaga mayai juu ya maji, ardhi, miti na nyasi pamoja na maeneo mengine yaliyo na majimaji. Pia mbu anaweza kutaga yai lake hata pakiwa na maji kiasi cha tone moja tu. Nayai ya mbu ni chakula kwa samaki pamoja na watutu wengine hivyo mbu huwa makini sana wakati wa kutaga mayai yake.

 

Tofauti na wadudu wengine na ndege mbu anaweza kulizuia yai lake tumboni kulitaga pindia anapohofia usalama wa yai lake. Kuku na ndege wengine yai linapofikia kutagwa hana namna lazima akalitage, lakini hii ni tofauti kwa mbu. Yai la mbu linaweza kukaa kwa muda wa miaka miwili bila ya kufa na ndo maana ni vigumu kutokomeza kabisa mbu.

 

Yai la mbu lina rangi ya njano, tangi hii ni rahisi kulifanya yai hili lionewe na maadui walao mayai ya mbu. Hivyo ifikapo usiku yai la mbu hubadilika rangi na kuwa jeusi. Hali hii husaidia kuliepusha yai la mbu kuliwa na maadua. Pia yai la mbu halizami ndani ya maji, na linaweza kuelea hewani, njia zote hizi husaidia ulinzi wa yai hili lisidhuriwe.

 

Ijapokuwa mbu anakula binadamu lakini na yeye ni chakula kwa viumbe vingine kama popo. Hivyo popo hutusaidia katika mapambano dhidi ya wadudu hawa hatari. mbu pia anaweza kujuwa wati mtu yupo kwa kutumia pumzi anayopumua mwanadamu



                   

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3269

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰2 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰4 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰6 web hosting    

Post zinazofanana:

Umuhimu wa kliniki na vipimo kwa wajawazito.

Ujauzito ni kipindi cha mabadiliko makubwa ya kimwili, kihisia, na kisaikolojia. Huduma za kliniki kwa wajawazito (Antenatal Care - ANC) ni nguzo muhimu inayohakikisha mama anakuwa na afya njema na mtoto anazaliwa akiwa salama. Makala hii inaangazia kwa nini kila mjamzito anapaswa kuhudhuria kliniki na umuhimu wa vipimo mbalimbali vinavyofanyika katika kipindi hicho.

Soma Zaidi...
DALILI ZA HOMA YA BONDE LA UFA (RVFD) NA INAVYOSAMBAZWA.

Homa hii inapatikana katika maeneo ya bonde la ufa barani Afrika na na Mashariki ya kati.

Soma Zaidi...
Dalili za Mimba Kabla ya Kipimo:

​Kipindi cha kusubiri ili kufanya kipimo cha mimba kinaweza kuwa na msisimko na wakati mwingine wasiwasi. Makala hii inakupatia mwongozo wa ishara za awali ambazo mwili wako unaweza kuzionyesha kabla hata ya kupata majibu ya vipimo vya maabara au vya nyumbani.

Soma Zaidi...
Minyoo na athari zao kiafya

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu minyoo na athari zao kiafya

Soma Zaidi...
Maumivu ya tumbo kitovuni

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu maumivu ya tumbo kitovuni

Soma Zaidi...
Njia salama za kuongeza uwezo wa kushika mimba.

Kupata ujauzito ni safari inayohitaji maandalizi ya mwili na akili. Kwa wanandoa wengi, mabadiliko madogo lakini yenye tija katika mtindo wa maisha yanaweza kuongeza nafasi za kupata mtoto kwa kiasi kikubwa. Makala hii inaangazia mbinu zilizothibitishwa kisayansi za kuboresha afya ya uzazi na kuongeza nafasi za kushika mimba kwa njia salama na ya asili.

Soma Zaidi...