picha

MTAMBUE MDUDU MBU ILI UWEZE KUJIKINGA NA UGONJWA WA MALARIA (yajuwe maajabu makubwa ya mdudu mbu)

Mbu ni katika wadudu wanaopatikana maeneo yenye joto hususan maeneo ynye hali ya hewa ya kitropik.

MTAMBUE MDUDU MBU ILI UWEZE KUJIKINGA NA UGONJWA WA MALARIA (yajuwe maajabu makubwa ya mdudu mbu)

PAMBANA NA MALARIA KWA KUMTAMBUA MDUDU MBU (MOSQUITO)

 

Mbu ni katika wadudu wanaopatikana maeneo yenye joto hususan maeneo ynye hali ya hewa ya kitropik. Mbu anafahamika kwa kuwa ndiye msambazaji mkubwa wa malaria pamoja na matende na ngiri maji. Chakula cha mbu ni maji, bakteria pamoja na damu. Mbu dume huweza kumjua mwanamke kwa kutumia sauti ya mbawa. Mbu ni katika wadudu wadogo lakini wana maajabu makubwa. Katika mkala hii tutaangalia kwa ufupi mambo matano kuhusu mbu.

 

Tofauti na kuwa mbu ni mdogo lakini anaweza kunyonya damu iliyokuwa nzito kuliko mwili wake. Yaani sawa na mtu mwenye uzito wa kilo 70 kula chakula chenye uzito wa kilo 100. mara mbu anaponyonya damu mwili wake huchukuwa mpaka siku tatu kuweza kuimeng’enya damu ile na kuimaliza. Baada ya hapo mbu atakwenda kunyonya damu tena. Itambulike kuwa chakula cha mbu ni bakteria, maji pamoja na damu. Mbu jike hula damu pindi anapotaka kutaga. Wataalamu wanaeleza kuwa kuna aina 2000 za mbu.

 

Kabla ya mbu kutaga mayai yake anaanza kupima ardhi kama ina majimaji pamoja na joto la kutosha kwa maisha ya mayai yake. Mbu hutaga mayai juu ya maji, ardhi, miti na nyasi pamoja na maeneo mengine yaliyo na majimaji. Pia mbu anaweza kutaga yai lake hata pakiwa na maji kiasi cha tone moja tu. Nayai ya mbu ni chakula kwa samaki pamoja na watutu wengine hivyo mbu huwa makini sana wakati wa kutaga mayai yake.

 

Tofauti na wadudu wengine na ndege mbu anaweza kulizuia yai lake tumboni kulitaga pindia anapohofia usalama wa yai lake. Kuku na ndege wengine yai linapofikia kutagwa hana namna lazima akalitage, lakini hii ni tofauti kwa mbu. Yai la mbu linaweza kukaa kwa muda wa miaka miwili bila ya kufa na ndo maana ni vigumu kutokomeza kabisa mbu.

 

Yai la mbu lina rangi ya njano, tangi hii ni rahisi kulifanya yai hili lionewe na maadui walao mayai ya mbu. Hivyo ifikapo usiku yai la mbu hubadilika rangi na kuwa jeusi. Hali hii husaidia kuliepusha yai la mbu kuliwa na maadua. Pia yai la mbu halizami ndani ya maji, na linaweza kuelea hewani, njia zote hizi husaidia ulinzi wa yai hili lisidhuriwe.

 

Ijapokuwa mbu anakula binadamu lakini na yeye ni chakula kwa viumbe vingine kama popo. Hivyo popo hutusaidia katika mapambano dhidi ya wadudu hawa hatari. mbu pia anaweza kujuwa wati mtu yupo kwa kutumia pumzi anayopumua mwanadamu



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2796

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 ai web app     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Kiungulia, dawa yake na namna ya kuzuia kiungulia

Tambuwa kiungulia, sababu zake, dawa za kiungulia na namna ya kupambana na kiungulia

Soma Zaidi...
Dalili za uvumilivu wa pombe

Uvumilivu wa pombe unaweza kusababisha athari za haraka, zisizofurahi baada ya kunywa pombe. Ishara na dalili za kawaida za kutovumilia kwa pombe ni pua iliyojaa na Kuvuta ngozi. Uvumilivu wa pombe husababishwa na hali ya maumbile ambayo mwili hauwezi k

Soma Zaidi...
Je unaweza kupata ujauzito bila ya kupata hedhi miezi 9 baada ya kujifunguwa?

Baada ya kujifungua mwili wa mwanamke huwa na mabadiliko tofauti na siku za nyuma. Kwa mfano hatapatavtena hedhi, hatoweza kupata ujauzito kwa muda wa mwezi ama zaidi. Endelea na post hii ujifunze zaidi

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa moyo.

Posti hii inaelezea kuhusiana na mambo hatari yanayosababisha ugonjwa wa moyo.

Soma Zaidi...
Sababu za maambukizi kwenye nephoni

Posti hii inahusu zaidi sababu za maambukizi kwenye nephroni, ni vitu vinavyosababisha mabukizi kwenye nephroni.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kuharisha na sababu zake.

Kuharisha ni Hali ya kupitisha kinyesi Cha maji chenye damu au kisicho na damu

Soma Zaidi...