picha

Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 9: Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu tukio la Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto

Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto

Mtume alipokuwa mtoto, tukio hili la kupasuliwa kifua na kutolewa moyo wake na kusafishwa lilitokea. Yote haya yalitokea kipindi akiwa analelewa na Bi Halima katika kabila la Bani Sa'ad. Wanazuoni wa sirah wameeleza kwa urefu tukio hili jinsi lilivyotokea, na hapa tutaangalia kwa ufupi tu.

 

Ni kuwa siku moja Mtume (s.a.w) alikuwa anacheza na watoto wenzie. Ghafla akatokea mtu mmoja, naye ni Jibril, akamshika Muhammad na kumlaza chini kisha akamtoa moyo wake na kuuosha kwa maji ya zamzam na aliondoa uchafu wa shetani kisha akaurudisha kwenye kifua na kukifunika.

 

Watoto walokuwa wakicheza na Mtume (s.a.w) wakakimbia na kwenda kumueleza Bi Halima kuwa Muhammad kauliwa. Bi Halima akatoka kwa haraka kufika akamkuta Muhammad akiwa amebadilika rangi. Muhammad alikuwa mzima wa afya, hapa Bi Halima alipata mashaka makubwa mpaka akawa na hofu juu ya kuendelea kumlea kijana Muhammad.

 

Katika maelezo mengine, waandishi wa sirah wameeleza tukio hili kama kupasuliwa kwa tumbo. Kwani zimekuja nukuu kuwa siku moja watoto walipokuwa wakicheza pamoja nao alikuwepo Muhammad (s.a.w), basi ghafla wakaja wanaume wawili walovaa nguo nyeupe (malaika) wakaulizana, "Ni huyu?" Basi yule mwingine akajibu, "Ndiyo, ni huyu." Wakamlaza kisha wakampasua tumbo lake na kutoa uchafu wa shetani kisha wakafunika kama lilivyo. Basi watoto walokuwa wakicheza naye wakaenda mbio kusema kwa Bi Halima na alipokuja kuulizwa Muhammad (s.a.w), akasema kuwa watu wawili wamekuja na kunipasua tumbo langu. Utapata maelezo zaidi ya kisa hiki kwenye kitabu kiitwacho "Nurul-Yaqin."

 

Bi Halima aliendelea kumlea Mtume (s.a.w) kwa muda wa miaka miwili mingine hadi alipotimiza miaka minne. Alipoamua kumrudisha mtoto kwa mama yake. Alihofia kuendelea kumlea mtoto huyu huenda akapatwa na jambo. Miaka minne ilikuwa imemtosha mtoto huyu kuwa na mwili imara na kuweza kuzungumza lugha ya Kiarabu kwa ufasaha tofauti na watoto walolelewa maeneo mengine.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-07-28 14:52:47 Topic: Historia ya Mtume Muhammad (s.a.w) Main: Masomo File: Download PDF Views 1070

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 49: Hila za Maquraish Dhidi ya Wahamiaji

Baada ya Waislamu kuhama Maquraish hawakupendezwa na jambo hilo, hivyo wakaanza kufanya hila ili Warejeshwe kutoka walipohamia

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 16: Historia ya Abu Talib

Katika somo hili utakwenda kujifunza historia ya Abu Talib ibn Abd al-Muttalib ambaye ni baba yae mkubwa Mtume ﷺ

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 22: Kujengwa upya kwa Al-Kaabah

Katika somo hili utakwenda kujifunza tukio la kujengwa upya kwa Al-Kaabah tukufu

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 57: Mkataba wa udhalimu

Baada ya Baini Abd Manaf kukubaliana kumlinda Mtume Muhammad basi Maquraish wakaweka mkataba wa udhalimu utakaozuia kutoshirikiana na banu abd Manaf kwa lolote lile.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 23: Maisha ya Mtume muhammad kabla ya utume

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu maisha ya Mtume Muammad ﷺ wakati wa ujana wake na kabla ya utume

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 5:Historia ya baba na mama yake Mtume Muhammad (s.a.w)

Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu historia ya wazazi wa Mtume Muhammad (s.a.w)

Soma Zaidi...