Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 9: Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu tukio la Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto
Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto
Mtume alipokuwa mtoto, tukio hili la kupasuliwa kifua na kutolewa moyo wake na kusafishwa lilitokea. Yote haya yalitokea kipindi akiwa analelewa na Bi Halima katika kabila la Bani Sa'ad. Wanazuoni wa sirah wameeleza kwa urefu tukio hili jinsi lilivyotokea, na hapa tutaangalia kwa ufupi tu.
Ni kuwa siku moja Mtume (s.a.w) alikuwa anacheza na watoto wenzie. Ghafla akatokea mtu mmoja, naye ni Jibril, akamshika Muhammad na kumlaza chini kisha akamtoa moyo wake na kuuosha kwa maji ya zamzam na aliondoa uchafu wa shetani kisha akaurudisha kwenye kifua na kukifunika.
Watoto walokuwa wakicheza na Mtume (s.a.w) wakakimbia na kwenda kumueleza Bi Halima kuwa Muhammad kauliwa. Bi Halima akatoka kwa haraka kufika akamkuta Muhammad akiwa amebadilika rangi. Muhammad alikuwa mzima wa afya, hapa Bi Halima alipata mashaka makubwa mpaka akawa na hofu juu ya kuendelea kumlea kijana Muhammad.
Katika maelezo mengine, waandishi wa sirah wameeleza tukio hili kama kupasuliwa kwa tumbo. Kwani zimekuja nukuu kuwa siku moja watoto walipokuwa wakicheza pamoja nao alikuwepo Muhammad (s.a.w), basi ghafla wakaja wanaume wawili walovaa nguo nyeupe (malaika) wakaulizana, "Ni huyu?" Basi yule mwingine akajibu, "Ndiyo, ni huyu." Wakamlaza kisha wakampasua tumbo lake na kutoa uchafu wa shetani kisha wakafunika kama lilivyo. Basi watoto walokuwa wakicheza naye wakaenda mbio kusema kwa Bi Halima na alipokuja kuulizwa Muhammad (s.a.w), akasema kuwa watu wawili wamekuja na kunipasua tumbo langu. Utapata maelezo zaidi ya kisa hiki kwenye kitabu kiitwacho "Nurul-Yaqin."
Bi Halima aliendelea kumlea Mtume (s.a.w) kwa muda wa miaka miwili mingine hadi alipotimiza miaka minne. Alipoamua kumrudisha mtoto kwa mama yake. Alihofia kuendelea kumlea mtoto huyu huenda akapatwa na jambo. Miaka minne ilikuwa imemtosha mtoto huyu kuwa na mwili imara na kuweza kuzungumza lugha ya Kiarabu kwa ufasaha tofauti na watoto walolelewa maeneo mengine.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 54: Kusilimu kwa Umar bin Al- Khattab
Hii ni historia fupi ya kuslimu kwa Umar na kuanza kwa taswira mpya ya waislamu na uislamu katika mji wa makkah
Soma Zaidi...Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 47: Nyumba ya Arqam Ibn Abi Al Arqam na kazi zake
Katika somo hili utakwenda kujifunza mchango mkubwa wa nyumba ya Arqam Ibn Abi AL Arqam katika historia nzima ya Uislamu
Soma Zaidi...Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 11: Kufarki kwa babu yake na kulelewa na baba yake mkubwa
Katika somo hili utajifunza kuhusu Mtume MUhammad ﷺ kulelewa na Kufarki kwa babu yake na kulelewa na baba yake mkubwa:
Soma Zaidi...Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 65: Safari ya Israa na Miraj
Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu historia ya safari ya sira na miraji na yanayopatikana katika safari hiyo
Soma Zaidi...Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 57: Mkataba wa udhalimu
Baada ya Baini Abd Manaf kukubaliana kumlinda Mtume Muhammad basi Maquraish wakaweka mkataba wa udhalimu utakaozuia kutoshirikiana na banu abd Manaf kwa lolote lile.
Soma Zaidi...Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 37: Amri ya kulingania watu wote kwenye Mlima As-Safa
Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu amri ya kulingania wtu wote, yale yaliyojiri katika mkutano wa kwanza na laana ya Abu Lhab. TUkio hili lilianyika katika mlima As-safa
Soma Zaidi...