Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 9: Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu tukio la Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto
Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto
Mtume alipokuwa mtoto, tukio hili la kupasuliwa kifua na kutolewa moyo wake na kusafishwa lilitokea. Yote haya yalitokea kipindi akiwa analelewa na Bi Halima katika kabila la Bani Sa'ad. Wanazuoni wa sirah wameeleza kwa urefu tukio hili jinsi lilivyotokea, na hapa tutaangalia kwa ufupi tu.
Ni kuwa siku moja Mtume (s.a.w) alikuwa anacheza na watoto wenzie. Ghafla akatokea mtu mmoja, naye ni Jibril, akamshika Muhammad na kumlaza chini kisha akamtoa moyo wake na kuuosha kwa maji ya zamzam na aliondoa uchafu wa shetani kisha akaurudisha kwenye kifua na kukifunika.
Watoto walokuwa wakicheza na Mtume (s.a.w) wakakimbia na kwenda kumueleza Bi Halima kuwa Muhammad kauliwa. Bi Halima akatoka kwa haraka kufika akamkuta Muhammad akiwa amebadilika rangi. Muhammad alikuwa mzima wa afya, hapa Bi Halima alipata mashaka makubwa mpaka akawa na hofu juu ya kuendelea kumlea kijana Muhammad.
Katika maelezo mengine, waandishi wa sirah wameeleza tukio hili kama kupasuliwa kwa tumbo. Kwani zimekuja nukuu kuwa siku moja watoto walipokuwa wakicheza pamoja nao alikuwepo Muhammad (s.a.w), basi ghafla wakaja wanaume wawili walovaa nguo nyeupe (malaika) wakaulizana, "Ni huyu?" Basi yule mwingine akajibu, "Ndiyo, ni huyu." Wakamlaza kisha wakampasua tumbo lake na kutoa uchafu wa shetani kisha wakafunika kama lilivyo. Basi watoto walokuwa wakicheza naye wakaenda mbio kusema kwa Bi Halima na alipokuja kuulizwa Muhammad (s.a.w), akasema kuwa watu wawili wamekuja na kunipasua tumbo langu. Utapata maelezo zaidi ya kisa hiki kwenye kitabu kiitwacho "Nurul-Yaqin."
Bi Halima aliendelea kumlea Mtume (s.a.w) kwa muda wa miaka miwili mingine hadi alipotimiza miaka minne. Alipoamua kumrudisha mtoto kwa mama yake. Alihofia kuendelea kumlea mtoto huyu huenda akapatwa na jambo. Miaka minne ilikuwa imemtosha mtoto huyu kuwa na mwili imara na kuweza kuzungumza lugha ya Kiarabu kwa ufasaha tofauti na watoto walolelewa maeneo mengine.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Historia ya Mtume Muhammad (s.a.w) somo la 1: Asili ya Waarabu
Katika somo hili utakwenda kujifunza Asili ya waarabu na kusambaa kwao katika bara arab
Soma Zaidi...Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 54: Kusilimu kwa Umar bin Al- Khattab
Hii ni historia fupi ya kuslimu kwa Umar na kuanza kwa taswira mpya ya waislamu na uislamu katika mji wa makkah
Soma Zaidi...Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 38: Taharuki yaingia Mjini Mkkah
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu yaliyotokea baada ya watu wa Mkkah kulinganiwa kwenye dini kwa mara ya kwanza
Soma Zaidi...Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 67: Mkataba wa 'Awa pili
Hii ni historia fupi ya makataba wa pili wa aqaba ambao ulifanywa kati ya Mtume wa Allah na waislamu wa Madina kutoka katika makbila ya aws na Khazraj
Soma Zaidi...Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 29: Amri za kwanza alizopewa Mtume Muhammad ﷺ
Katika somo hili utajifunza amri ambazo alipewa Mtume Muhammad ﷺ mwanzoni kabisa mwa kazi yake ya Kulingania dini
Soma Zaidi...Historia ya Mtume Muhammad (s.a.w) somo la 21: Ndoa ya Mtume Muhammad na Bi khadija
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu ndoa ya Mtume Muhammad ﷺ na Bi Khadija
Soma Zaidi...