Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu tukio la Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto
Mtume alipokuwa mtoto, tukio hili la kupasuliwa kifua na kutolewa moyo wake na kusafishwa lilitokea. Yote haya yalitokea kipindi akiwa analelewa na Bi Halima katika kabila la Bani Sa'ad. Wanazuoni wa sirah wameeleza kwa urefu tukio hili jinsi lilivyotokea, na hapa tutaangalia kwa ufupi tu.
Ni kuwa siku moja Mtume (s.a.w) alikuwa anacheza na watoto wenzie. Ghafla akatokea mtu mmoja, naye ni Jibril, akamshika Muhammad na kumlaza chini kisha akamtoa moyo wake na kuuosha kwa maji ya zamzam na aliondoa uchafu wa shetani kisha akaurudisha kwenye kifua na kukifunika.
Watoto walokuwa wakicheza na Mtume (s.a.w) wakakimbia na kwenda kumueleza Bi Halima kuwa Muhammad kauliwa. Bi Halima akatoka kwa haraka kufika akamkuta Muhammad akiwa amebadilika rangi. Muhammad alikuwa mzima wa afya, hapa Bi Halima alipata mashaka makubwa mpaka akawa na hofu juu ya kuendelea kumlea kijana Muhammad.
Katika maelezo mengine, waandishi wa sirah wameeleza tukio hili kama kupasuliwa kwa tumbo. Kwani zimekuja nukuu kuwa siku moja watoto walipokuwa wakicheza pamoja nao alikuwepo Muhammad (s.a.w), basi ghafla wakaja wanaume wawili walovaa nguo nyeupe (malaika) wakaulizana, "Ni huyu?" Basi yule mwingine akajibu, "Ndiyo, ni huyu." Wakamlaza kisha wakampasua tumbo lake na kutoa uchafu wa shetani kisha wakafunika kama lilivyo. Basi watoto walokuwa wakicheza naye wakaenda mbio kusema kwa Bi Halima na alipokuja kuulizwa Muhammad (s.a.w), akasema kuwa watu wawili wamekuja na kunipasua tumbo langu. Utapata maelezo zaidi ya kisa hiki kwenye kitabu kiitwacho "Nurul-Yaqin."
Bi Halima aliendelea kumlea Mtume (s.a.w) kwa muda wa miaka miwili mingine hadi alipotimiza miaka minne. Alipoamua kumrudisha mtoto kwa mama yake. Alihofia kuendelea kumlea mtoto huyu huenda akapatwa na jambo. Miaka minne ilikuwa imemtosha mtoto huyu kuwa na mwili imara na kuweza kuzungumza lugha ya Kiarabu kwa ufasaha tofauti na watoto walolelewa maeneo mengine.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Baada ya Baini Abd Manaf kukubaliana kumlinda Mtume Muhammad basi Maquraish wakaweka mkataba wa udhalimu utakaozuia kutoshirikiana na banu abd Manaf kwa lolote lile.
Soma Zaidi...Baadhi ya matukio mengine yaliyoteokea kweye safari hii ya Tfai
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunz akuhusu amri ya kulingania dini bila ya kificho, baada ya kulingania kwa siri kwa miaka mitatu
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu historia ya Amina mama wa Mtume Muhammad ﷺ
Soma Zaidi...Hapa tutakwend akujifunz akwa urefu zaidi kuhusu safari hii ya kwanz aya kuelekea Ethiopia inayojulkana kama Hijra ya kwanza.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujfunz akuhusu historia ya Bi Khada mke wa kwanz awa Mtume Muhammad ﷺ
Soma Zaidi...Baada ya Waislamu kuhama Maquraish hawakupendezwa na jambo hilo, hivyo wakaanza kufanya hila ili Warejeshwe kutoka walipohamia
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu safari ya Mtume Muhammad s.a.w kuelekea Madina. Utajifunza changamoto za safari alizokutana nazo.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunz ahistoria ya kuhamia Madina kwa waisalmau. Namna ambavyo walihama na mateso waliokuwa wakiyapata.
Soma Zaidi...Baada ya Maquraish kufeli mpango wao wa kuwarejesha Wahamiaji, wakaamuwa wafanye mbinu nyingine kwa ajili ya kuzuia harakati za Mtume Muhammad
Soma Zaidi...