Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 9: Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu tukio la Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto

Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto

Mtume alipokuwa mtoto, tukio hili la kupasuliwa kifua na kutolewa moyo wake na kusafishwa lilitokea. Yote haya yalitokea kipindi akiwa analelewa na Bi Halima katika kabila la Bani Sa'ad. Wanazuoni wa sirah wameeleza kwa urefu tukio hili jinsi lilivyotokea, na hapa tutaangalia kwa ufupi tu.

 

Ni kuwa siku moja Mtume (s.a.w) alikuwa anacheza na watoto wenzie. Ghafla akatokea mtu mmoja, naye ni Jibril, akamshika Muhammad na kumlaza chini kisha akamtoa moyo wake na kuuosha kwa maji ya zamzam na aliondoa uchafu wa shetani kisha akaurudisha kwenye kifua na kukifunika.

 

Watoto walokuwa wakicheza na Mtume (s.a.w) wakakimbia na kwenda kumueleza Bi Halima kuwa Muhammad kauliwa. Bi Halima akatoka kwa haraka kufika akamkuta Muhammad akiwa amebadilika rangi. Muhammad alikuwa mzima wa afya, hapa Bi Halima alipata mashaka makubwa mpaka akawa na hofu juu ya kuendelea kumlea kijana Muhammad.

 

Katika maelezo mengine, waandishi wa sirah wameeleza tukio hili kama kupasuliwa kwa tumbo. Kwani zimekuja nukuu kuwa siku moja watoto walipokuwa wakicheza pamoja nao alikuwepo Muhammad (s.a.w), basi ghafla wakaja wanaume wawili walovaa nguo nyeupe (malaika) wakaulizana, "Ni huyu?" Basi yule mwingine akajibu, "Ndiyo, ni huyu." Wakamlaza kisha wakampasua tumbo lake na kutoa uchafu wa shetani kisha wakafunika kama lilivyo. Basi watoto walokuwa wakicheza naye wakaenda mbio kusema kwa Bi Halima na alipokuja kuulizwa Muhammad (s.a.w), akasema kuwa watu wawili wamekuja na kunipasua tumbo langu. Utapata maelezo zaidi ya kisa hiki kwenye kitabu kiitwacho "Nurul-Yaqin."

 

Bi Halima aliendelea kumlea Mtume (s.a.w) kwa muda wa miaka miwili mingine hadi alipotimiza miaka minne. Alipoamua kumrudisha mtoto kwa mama yake. Alihofia kuendelea kumlea mtoto huyu huenda akapatwa na jambo. Miaka minne ilikuwa imemtosha mtoto huyu kuwa na mwili imara na kuweza kuzungumza lugha ya Kiarabu kwa ufasaha tofauti na watoto walolelewa maeneo mengine.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Historia ya Mtume Muhammad (s.a.w) Main: Dini File: Download PDF Views 391

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 70: Kuhama kwa Mtume Muhammad s.a.w kuelekea Madina

Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu safari ya Mtume Muhammad s.a.w kuelekea Madina. Utajifunza changamoto za safari alizokutana nazo.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 66: Mkataba wa Aqaba wa kwanza

Katika somo hili utajifunza kuhusu historia ya Mkataba wa Aqaba wa kwanza

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 22: Kujengwa upya kwa Al-Kaabah

Katika somo hili utakwenda kujifunza tukio la kujengwa upya kwa Al-Kaabah tukufu

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 7: Kuzaliwa kwa Mtume MUhammad ﷺ

katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Mazazi ya Mtume MUhammad ﷺ na kupewa jina.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 41: Mbinu za kukomesha kuenea kwa uislamu

Katika somo hili utakwenda kujifunza mambo yaliyofanyika katika harakati za kukomesha kuenea kwa uislamu.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 65: Safari ya Israa na Miraj

Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu historia ya safari ya sira na miraji na yanayopatikana katika safari hiyo

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 35: Amriya kulingania watu wa karibu

Katika somo hili utakwenda kujifunz akuhusu amri ya kulingania watu wa karibu

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 14: Historia ya Amina mama wa Mtume Muhammad

Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu historia ya Amina mama wa Mtume Muhammad ﷺ

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 46: Historia fupi ya Al-Arqam ibn Abi al-Arqam

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuusu historia ya mmoja katika maswahaba wa mwanzoni na mwenye mchango mkubwa sana katika uislamu ambaye ni Al-Arqam ibn Abi al-Arqam

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad (s.a.w) somo la 1: Asili ya Waarabu

Katika somo hili utakwenda kujifunza Asili ya waarabu na kusambaa kwao katika bara arab

Soma Zaidi...