picha

Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 9: Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu tukio la Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto

Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto

Mtume alipokuwa mtoto, tukio hili la kupasuliwa kifua na kutolewa moyo wake na kusafishwa lilitokea. Yote haya yalitokea kipindi akiwa analelewa na Bi Halima katika kabila la Bani Sa'ad. Wanazuoni wa sirah wameeleza kwa urefu tukio hili jinsi lilivyotokea, na hapa tutaangalia kwa ufupi tu.

 

Ni kuwa siku moja Mtume (s.a.w) alikuwa anacheza na watoto wenzie. Ghafla akatokea mtu mmoja, naye ni Jibril, akamshika Muhammad na kumlaza chini kisha akamtoa moyo wake na kuuosha kwa maji ya zamzam na aliondoa uchafu wa shetani kisha akaurudisha kwenye kifua na kukifunika.

 

Watoto walokuwa wakicheza na Mtume (s.a.w) wakakimbia na kwenda kumueleza Bi Halima kuwa Muhammad kauliwa. Bi Halima akatoka kwa haraka kufika akamkuta Muhammad akiwa amebadilika rangi. Muhammad alikuwa mzima wa afya, hapa Bi Halima alipata mashaka makubwa mpaka akawa na hofu juu ya kuendelea kumlea kijana Muhammad.

 

Katika maelezo mengine, waandishi wa sirah wameeleza tukio hili kama kupasuliwa kwa tumbo. Kwani zimekuja nukuu kuwa siku moja watoto walipokuwa wakicheza pamoja nao alikuwepo Muhammad (s.a.w), basi ghafla wakaja wanaume wawili walovaa nguo nyeupe (malaika) wakaulizana, "Ni huyu?" Basi yule mwingine akajibu, "Ndiyo, ni huyu." Wakamlaza kisha wakampasua tumbo lake na kutoa uchafu wa shetani kisha wakafunika kama lilivyo. Basi watoto walokuwa wakicheza naye wakaenda mbio kusema kwa Bi Halima na alipokuja kuulizwa Muhammad (s.a.w), akasema kuwa watu wawili wamekuja na kunipasua tumbo langu. Utapata maelezo zaidi ya kisa hiki kwenye kitabu kiitwacho "Nurul-Yaqin."

 

Bi Halima aliendelea kumlea Mtume (s.a.w) kwa muda wa miaka miwili mingine hadi alipotimiza miaka minne. Alipoamua kumrudisha mtoto kwa mama yake. Alihofia kuendelea kumlea mtoto huyu huenda akapatwa na jambo. Miaka minne ilikuwa imemtosha mtoto huyu kuwa na mwili imara na kuweza kuzungumza lugha ya Kiarabu kwa ufasaha tofauti na watoto walolelewa maeneo mengine.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-07-28 Topic: Historia ya Mtume Muhammad (s.a.w) Main: Dini File: Download PDF Views 953

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 web hosting    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 ai web app    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 13: Historia fupi ya Abd al-Muttalib

Katika somo hili utakwenda kujifunza historia ya mzee Abdul al MUttalib. Historia hii inaweza kutofautiana kidogo na ambayo umeshajifunza. na hii ni kutokana kutofautiana kwa mapokeo.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 62: Kurudi Makkah

Hatimaye Mtume Muhammad ﷺ anarejea Makkah na kuendelea na kazi yake

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 44: Historia fupi ya Mke wa Abu Lahab - Arwā bint Ḥarb

Katika somo hili utakwenda kujifunza kwa ufupi historia ya mmoja katika maadui wakubwa wa Uislamu wakati Mtume alipokuwa analingania dini.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 47: Nyumba ya Arqam Ibn Abi Al Arqam na kazi zake

Katika somo hili utakwenda kujifunza mchango mkubwa wa nyumba ya Arqam Ibn Abi AL Arqam katika historia nzima ya Uislamu

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 18: Historia ya vita vya Fijar

Hapa utajifunza chanzo vya vita vya al fijar na vipi Mtume Muhammad ﷺ alishiriki katika vita hivyo.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 43: Mateso walyoyapata waslamu

Katka somo hili utakwenda kujifunza kuhusu mateso ambayo wamepewa Waislamu ili kuachana na uislamu wao

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 56: Abu Talib Awaunganisha Bani Hashim na Bani Al-Muttalib kwa Ulinzi wa Mtume (SAW)

Wana wa Abd Manaf wanaungana kumlinda Mtume Muhammad isipokuwa Abu Lahab yeye amekataa kuungana na ndugu zake.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 17: Hadithi ya Mtume Muhammad ﷺ kukutana na Bahira akiwa na miaka 12

Katikasomo hili utakwenda kujifunza stori maarufu ya Bahira kuhusu kukutana na Mtume Muhammad ﷺ na kumtambuwa utume wake.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 39: Baraza la ushauri kuwazuia mahujaji kumfuata Muhammad ﷺ

Katika somo hili utakwenda ujifunza kuhusu uwamuzi wa Baraza la ushauri kuwazuia mahujaji kumfuata Muhammad ﷺ wakati wa msimu wa hija.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 31: Watu wa Mwanzoni kuingia katika uislamu

Katika somo hili utakwenda kujifunz akuhusu watu wa mwanzoni kuingia katika Uislamu

Soma Zaidi...