picha

Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 9: Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu tukio la Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto

Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto

Mtume alipokuwa mtoto, tukio hili la kupasuliwa kifua na kutolewa moyo wake na kusafishwa lilitokea. Yote haya yalitokea kipindi akiwa analelewa na Bi Halima katika kabila la Bani Sa'ad. Wanazuoni wa sirah wameeleza kwa urefu tukio hili jinsi lilivyotokea, na hapa tutaangalia kwa ufupi tu.

 

Ni kuwa siku moja Mtume (s.a.w) alikuwa anacheza na watoto wenzie. Ghafla akatokea mtu mmoja, naye ni Jibril, akamshika Muhammad na kumlaza chini kisha akamtoa moyo wake na kuuosha kwa maji ya zamzam na aliondoa uchafu wa shetani kisha akaurudisha kwenye kifua na kukifunika.

 

Watoto walokuwa wakicheza na Mtume (s.a.w) wakakimbia na kwenda kumueleza Bi Halima kuwa Muhammad kauliwa. Bi Halima akatoka kwa haraka kufika akamkuta Muhammad akiwa amebadilika rangi. Muhammad alikuwa mzima wa afya, hapa Bi Halima alipata mashaka makubwa mpaka akawa na hofu juu ya kuendelea kumlea kijana Muhammad.

 

Katika maelezo mengine, waandishi wa sirah wameeleza tukio hili kama kupasuliwa kwa tumbo. Kwani zimekuja nukuu kuwa siku moja watoto walipokuwa wakicheza pamoja nao alikuwepo Muhammad (s.a.w), basi ghafla wakaja wanaume wawili walovaa nguo nyeupe (malaika) wakaulizana, "Ni huyu?" Basi yule mwingine akajibu, "Ndiyo, ni huyu." Wakamlaza kisha wakampasua tumbo lake na kutoa uchafu wa shetani kisha wakafunika kama lilivyo. Basi watoto walokuwa wakicheza naye wakaenda mbio kusema kwa Bi Halima na alipokuja kuulizwa Muhammad (s.a.w), akasema kuwa watu wawili wamekuja na kunipasua tumbo langu. Utapata maelezo zaidi ya kisa hiki kwenye kitabu kiitwacho "Nurul-Yaqin."

 

Bi Halima aliendelea kumlea Mtume (s.a.w) kwa muda wa miaka miwili mingine hadi alipotimiza miaka minne. Alipoamua kumrudisha mtoto kwa mama yake. Alihofia kuendelea kumlea mtoto huyu huenda akapatwa na jambo. Miaka minne ilikuwa imemtosha mtoto huyu kuwa na mwili imara na kuweza kuzungumza lugha ya Kiarabu kwa ufasaha tofauti na watoto walolelewa maeneo mengine.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-07-28 14:52:47 Topic: Historia ya Mtume Muhammad (s.a.w) Main: Masomo File: Download PDF Views 1087

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Simulizi za Hadithi Audio     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 34: Amri ya kulingnia dini kwa uwazi

Katika somo hili utajifunz akuhusu amri ya kulingania dini bila ya kificho, baada ya kulingania kwa siri kwa miaka mitatu

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 25 Jibril analeta Wahyi kwa Mtume Muhammad ﷺ

Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu historia ya Mwanzoni mwa Wahyi aliouleta Jibril kwa Mtume Muhammad ﷺ

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 32: Mwanzoni mwa ibada ya Swala

Katika somo hili utakwenda kujifunz akuhusu mwanzoni mwa kuamrishwa ibada ya swala na vipi iliswaliwa.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 26: Kusimama kwa Wahy

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu kusimama kwa Wahyi kuja kwa Mtume Muhammad ﷺ

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 30: Miaka mitatu ya kulingania kwa siri

Katika somo hili utakwenda kujifunz akuhusu miaka mitatu ya kulingania dini kwa siri na mambo yaliyojitokeza.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 22: Kujengwa upya kwa Al-Kaabah

Katika somo hili utakwenda kujifunza tukio la kujengwa upya kwa Al-Kaabah tukufu

Soma Zaidi...