Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 9: Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu tukio la Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto

Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto

Mtume alipokuwa mtoto, tukio hili la kupasuliwa kifua na kutolewa moyo wake na kusafishwa lilitokea. Yote haya yalitokea kipindi akiwa analelewa na Bi Halima katika kabila la Bani Sa'ad. Wanazuoni wa sirah wameeleza kwa urefu tukio hili jinsi lilivyotokea, na hapa tutaangalia kwa ufupi tu.

 

Ni kuwa siku moja Mtume (s.a.w) alikuwa anacheza na watoto wenzie. Ghafla akatokea mtu mmoja, naye ni Jibril, akamshika Muhammad na kumlaza chini kisha akamtoa moyo wake na kuuosha kwa maji ya zamzam na aliondoa uchafu wa shetani kisha akaurudisha kwenye kifua na kukifunika.

 

Watoto walokuwa wakicheza na Mtume (s.a.w) wakakimbia na kwenda kumueleza Bi Halima kuwa Muhammad kauliwa. Bi Halima akatoka kwa haraka kufika akamkuta Muhammad akiwa amebadilika rangi. Muhammad alikuwa mzima wa afya, hapa Bi Halima alipata mashaka makubwa mpaka akawa na hofu juu ya kuendelea kumlea kijana Muhammad.

 

Katika maelezo mengine, waandishi wa sirah wameeleza tukio hili kama kupasuliwa kwa tumbo. Kwani zimekuja nukuu kuwa siku moja watoto walipokuwa wakicheza pamoja nao alikuwepo Muhammad (s.a.w), basi ghafla wakaja wanaume wawili walovaa nguo nyeupe (malaika) wakaulizana, "Ni huyu?" Basi yule mwingine akajibu, "Ndiyo, ni huyu." Wakamlaza kisha wakampasua tumbo lake na kutoa uchafu wa shetani kisha wakafunika kama lilivyo. Basi watoto walokuwa wakicheza naye wakaenda mbio kusema kwa Bi Halima na alipokuja kuulizwa Muhammad (s.a.w), akasema kuwa watu wawili wamekuja na kunipasua tumbo langu. Utapata maelezo zaidi ya kisa hiki kwenye kitabu kiitwacho "Nurul-Yaqin."

 

Bi Halima aliendelea kumlea Mtume (s.a.w) kwa muda wa miaka miwili mingine hadi alipotimiza miaka minne. Alipoamua kumrudisha mtoto kwa mama yake. Alihofia kuendelea kumlea mtoto huyu huenda akapatwa na jambo. Miaka minne ilikuwa imemtosha mtoto huyu kuwa na mwili imara na kuweza kuzungumza lugha ya Kiarabu kwa ufasaha tofauti na watoto walolelewa maeneo mengine.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Historia ya Mtume Muhammad (s.a.w) Main: Dini File: Download PDF Views 392

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 70: Kuhama kwa Mtume Muhammad s.a.w kuelekea Madina

Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu safari ya Mtume Muhammad s.a.w kuelekea Madina. Utajifunza changamoto za safari alizokutana nazo.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 67: Mkataba wa 'Awa pili

Hii ni historia fupi ya makataba wa pili wa aqaba ambao ulifanywa kati ya Mtume wa Allah na waislamu wa Madina kutoka katika makbila ya aws na Khazraj

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 7: Kuzaliwa kwa Mtume MUhammad ﷺ

katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Mazazi ya Mtume MUhammad ﷺ na kupewa jina.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 3: Kufukuliwa upya wa kisima cha Zamzamm

Katika somo hili utakwend akujfunza historia ya kufukuliwa upya kwa kisima cha zamzam baada ya kutoweka kwa muda mrefu

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 39: Baraza la ushauri kuwazuia mahujaji kumfuata Muhammad ﷺ

Katika somo hili utakwenda ujifunza kuhusu uwamuzi wa Baraza la ushauri kuwazuia mahujaji kumfuata Muhammad ﷺ wakati wa msimu wa hija.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 17: Hadithi ya Mtume Muhammad ﷺ kukutana na Bahira akiwa na miaka 12

Katikasomo hili utakwenda kujifunza stori maarufu ya Bahira kuhusu kukutana na Mtume Muhammad ﷺ na kumtambuwa utume wake.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 68: Waislamu wanahamia Madina

Katika somo hili utakwend akujifunz ahistoria ya kuhamia Madina kwa waisalmau. Namna ambavyo walihama na mateso waliokuwa wakiyapata.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 24: Katika pango la Hira

Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu yaliyojiri katka pango la Hira kabla ya kupokea utume

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 4: Historia ya kuangamizwa kwa jeshi la Tembo

Katika soo hili utakwenda kujifunza historia ya jeshi la tembo na jinsi lilivyoangamizwa. Pia utajifunza namna ambavyo watu wa Makkah waliweza kujilinda.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 33: Mquraishi wanagunduwa kuhusu dini Mpya

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu namna ambavyo wito wa ulingano ulipoenea na kuwafikia maquraish na washirikina

Soma Zaidi...