Hadithi Ya 40: Kuwa Duniani Kama Vile Mgeni Au Mpita Njia
Hadithi Ya 40: Kuwa Duniani Kama Vile Mgeni Au Mpita Njia
الحديث الأربعون
"كن في الدنيا كأنك غريب أو عابر سبيل"
عن ابنِ عُمَرَ رضي اللهُ عنهما قال: أَخَذَ رسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم بِمَنْكِبيَّ فقال : ((كُنْ في الدُّنْيا كأنَّكَ غَرِيبٌ، أو عابرُ سبِيلٍ)).
وكانَ ابنُ عُمَرَ رَضي اللهُ عنهما يقولُ: إذا أمْسَيْتَ فلا تَنْتظِرِ الصبَّاحَ، وإذا أصْبَحْتَ فلا تَنْتَظِرِ الَمسَاءَ، وخُذْ مِنْ صِحَّتِكَ لِمَرضِكَ، ومِنْ حَياتِكَ لِمَوْتِكَ.
رَوَاهُ الْبُخَارِيُّ
HADITHI YA 40 KUWA DUNIANI KAMA VILE MGENI AU MPITA NJIA
Kutoka kwa Ibn 'Umar رضي الله عنهما ambaye alisema:
Mtume صلى الله عليه وسلم alinishika bega na akasema: Kuwa (ishi) duniani kama vile mgeni au mpita njia.
Naye Ibn 'Umar رضي الله عنه alikuwa akisema : Ukishinda hadi jioni usitaraji kuishi mpaka asubuhi, na ukiamka asubuhi usitaraji kuishi mpaka jioni, chukua uzima wako kwa ugonjwa wako (yaani fanya yale yote mema uwezayo wakati bado una afya nzuri kwani siku ukiumwa hutoweza kuyafanya), na uhai wako kwa kifo chako (tumia maisha yako vizuri kwa kufanya amali njema maana ukishafariki hakuna tena uwezalo kulifanya).
Imesimuliwa na Al-Bukhari
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 ai web app 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Dua za kuwaombea wazazi
Kwenye Quran kuna duaambazo Allah ametufundisha tuziombe kwa ajili ya wazazi, familia na kwa ajili yetu wenyewe.
Soma Zaidi...Uandishi wa hadithi wakati wa Matabii tabiina (tabiitabiina)
Hii ni historia ya uandishi wa hadithi wakati wa tabii tabiina. Yaani wafuasi wa wale wafuasi wa Masahaba
Soma Zaidi...