hukumu ya ombaomba katika uchumi wa kiislamu

Suala la omba-ombaTukiliangalia suala la omba-omba kwa upana kidogo, ambalo hivi sasa linaongelewa katika vikao mbalimbali vya kitaifa na kimataifa, tutaona kuwa ni Uislamu pekee unaotoa namna bora ya kulishughulikia suala hili.

hukumu ya ombaomba katika uchumi wa kiislamu

5

Suala la omba-omba
Tukiliangalia suala la omba-omba kwa upana kidogo, ambalo hivi sasa linaongelewa katika vikao mbalimbali vya kitaifa na kimataifa, tutaona kuwa ni Uislamu pekee unaotoa namna bora ya kulishughulikia suala hili. Omba omba ni kitendo kibaya sana kikiwa kimefanywa na mtu binafsi au taifa na kinashusha hadhi ya mtu binafsi na hadhi ya taifa kwa ujumla. Hivyo Uislamu ambao ndio njia sahihi pekee ya maisha, hauwezi kamwe ukapalilia omba omba na wala Zaka na sadaka kazi yake si kupalilia omba-omba, bali kinyume chake zaka na sadaka ni miongoni mwa silaha zinazotumiwa kutokomeza omba omba. Uislamu unawashutumu vikali omba omba kama tunavyojifunza katika Hadithi ifuatayo:



Hubshi bin Junadah ameeleza kuwa Mtume wa Al-lah amesema: Kuomba-omba si halali kwa mwenye uwezo wala kwa mwenye uzima wa afya na mwenye nguvu (za kufanya kazi) ila kwa mwenye kupigwa ufakiri na mw enye deni kubw a (asilow eza kulilipa). Na yule anayeomba watu ili ajiongezee mali yake atakuwa na mkwaruzo usoni mwake katika siku ya Kiyama na atayala kwa ulafi mkubwa mawe ya moto kutoka motoni. Kwa hiyo anayetaka, mwache aombe kidogo, n a m w ache a om be k ingi. (Tirm idh)



Wanaoruhusiwa kuomba kwa mujibu wa Hadith ni:
(i)Mtu aliyesimama kumdhamini mtu mwingine ili kuleta suluhu kati ya wagomvi wawili. huyu anaruhusiwa kuomba hata akiwa tajiri. Kwa mnasaba huu, waumini wa misikitini, madarasa, na shughuli mbali mbali za Kiislamu wanaruhusiwa kuomba michango ya Waislamu ili kufanikisha shughuli hizo.



(ii)Mtu aliyepata ajali na kuharibikiwa kabisa na vitu vyake vyote kama vile ajali ya moto, mafuriko, nakadhalika.



(iii)Mtu ambaye amepigwa na ufakiri na amekosa kabisa mahitaji muhimu ya maisha kama vile chakula, malazi na makazi, lakini mtu akiwa na angalau chakula cha siku moja na malazi mkononi mwake haruhusiwi kuomba kama tunavyofahamishwa katika Hadithi zifu atazo:



Abdullah bin Mas 'ud ameeleza kuwa Mtume wa Al-lah amesema: Anayeomba omba watu na ilhali ana mahitaji muhimu ya maisha atakuja siku ya Kiyama na mikwaruzo, vidonda au majeraha usoni mwake. Iliulizwa: Ee Mtume wa Allah! Ni kiasi gani kinachomtosha mtu? Akajibu: Dirham 50 au thamani yake. (Abu Daud, Tirmidh, Nisai, Ibn Majah).



Sahl bin Haohaliyya ameeleza kuwa Mtume wa Al-lah amesema:Yeyote yule anayeomba na ilihali anajitosheleza kwa mahitaji muhimu, anaomba moto (Jahannam). Nufaili ambaye ni miongoni mwa wasimulizi wa Hadithi hii katika sehemu nyingine aliuliza: Ni yupi mwenye uwezo ambaye kuomba ni haramu? Alijibu (Mtume s.a.w.): Yule mwenye uwezo wa kupata chakula cha asubuhi na usiku. Mahali pengine amesema: Yule mwenye chakula cha siku moja (usiku na mchana) (Abu Daud).
Hivyo ikibidi mtu aombe, basi aombe kwa sababu hizo tatu zilizotajwa katika Hadithi hii. Kuomba omba bila ya sababu za msingi kumeharamishwa kwa sababu kuu tatu zifu atazo:



(i)Kuomba omba kunamfanya mtu apoteze moyoni mwake ile hali ya kumtegemea Allah (s.w.) na atajenga moyoni mwake hali ya kulalamika juu ya neema za Allah zilizomzunguka kila mahali. Kwa msingi huu hatima ya kuomba omba ni kumfanya mja awategemee wengine kwa mahitajio yake badala ya kumtegemea Allah (s.w.) na kumfanya ashindwe kushukuru neema za Allah (s.w.).



(ii)Kuomba omba humfanya mtu awe mnyonge na ajidhalilishe kwa wengine ambapo Muislamu anatakiwa ajidhalilishe kwa Allah (s.w.) peke yake.



(iii)Vile vile kuomba omba kumekatazwa kwa sababu kunamuweka yule anayeombwa katika hali ngumu. Wakati mwingine anayeombwa hali yake si nzuri vile vile lakini kwa kuombwa hulazimika kutoa jambo ambalo linaweza kumuathiri yeye na wale anaowaangalia. Uislamu haukuishia kwenye kukemea tu tabia ya omba omba bali umetoa njia za kutatua tatizo hili kama ifu atavyo:



(i)Kuwasaidia wale wote wenye matatizo na dhiki mbali mbali kwa kuwapa Sadaqa na zakati kabla hawajaomba.


(ii)Njia ya pili, ya kukomesha kuomba omba ni kujitegemea kwa kufanya kazi kwa kutumia juhudi na maarifa.




                   




Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 242


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Quran si maneno ya mwenye kifafa
Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII SULEIMAN
Soma Zaidi...

umuhimu wa swala katika uislamu
Soma Zaidi...

maana ya Eda na aina zake
Ni kipindi au muda wa kungojea mwanamke aliyepewa talaka (aliyeachwa) au kufiwa na mumewe kabla ya kuolewa na mume mwingine. Soma Zaidi...

Mchango wa Waislamu Katika Kuleta Uhuru Tanganyika
i. Soma Zaidi...

Amri ya Kuchinja Ng'ombe
Kutokana na kuishi kwao Misr kwa muda mrefu, Mayahudi waliathiriwa na ibada za kishirikina za Wamisr. Soma Zaidi...

Kwanini Uislamu umeipa Elimu nafasi ya kwanza?
Soma Zaidi...

Hadhi na haki za mwanamke katika uislamu
4. Soma Zaidi...

Maana ya Ndoa na Faida zake katika jamii
4. Soma Zaidi...

Haki na wajibu wa mke kwa mumewe na familia
Soma Zaidi...

Haki za kijamii za mwanamke katika uislamu
Soma Zaidi...

Uthibitisho Kuwa Qur'an ni Neno la Mwenyezi Mungu (s.w)
Soma Zaidi...