Funga za suna na funga za kafara na nadhiri: Masharti yake, nguzo zake na wakati wa kutekeleza

Funga za Sunnah.

Funga za suna na funga za kafara na nadhiri: Masharti yake, nguzo zake na wakati wa kutekeleza

Funga za suna na funga za kafara na nadhiri: Masharti yake, nguzo zake na wakati wa kutekeleza

Funga za Sunnah.
- Nia ya kufunga Sunnah inaweza kutiwa muda wowote ule kabla ya Adhuhuri
iwapo mfungaji hakuonja chochote tangu Alfajir.
- Kuna hiari ya kuvunja funga ya Sunnah muda wowote ule pindi itakapobidi.



Umuhimu wa funga za sunnah.
1.Ni kumtii na kumuiga Mtume (s.a.w).
2.Ni kujazilizia mapungufu ya funga ya faradhi.
3.Humuwezesha muumini kufikia lengo la funga (kuwa Wacha-Mungu).
oFunga za Sunnah na namna ya kutekeleza.
a)Kufunga siku tatu kila mwezi.
- Ni kufunga siku tatu mfululizo za mbalamwezi, mwezi 13, 14 na 15.



b)Kufunga ya siku ya Jumatatu na Al-khamisi.
- Jumatatu ni siku aliyozaliwa Mtume (s.a.w) na Al-khamisi ni siku kupandishwa amali za mja kwenda kwa Mola wake.



c)Kufunga siku sita za mwezi wa Shawwal.
- Ni kufunga sita mara baada ya mwezi wa Ramadhani kuisha.



d)Funga ya Arafa.
- Ni kufunga siku ya mwezi 9, Dhul-Hijj ambamo mahujaji wako katika kisimamo katika uwanja wa Arafa.

e)Funga ya Ashura.
- Ni kufunga siku ya mwezi 10, Muharram (mfungo nne). Ni siku aliyookolewa Nabii Musa na Bani Israil kutoka kwa utawala wa Firaun.



f) Funga katika mwezi Shaaban.
- Ni kufunga kwa wingi katika mwezi wa Shaaban bila ya kutimiza siku 30.



Funga za Kafara.
- Ni funga anazolazimika muislamu kufunga ili ziwe kitubio au fidia baada ya kutenda kosa fulani.

Aina za funga za kafara.
1. Kufunga miezi miwili mfululizo kwa muislamu aliyemuua mtu kwa bahati mbaya na akakosa mali ya kulipa fidia.
Rejea Qur'an (4:92).


2. Kufunga miezi miwili mfululizo kwa muislamu aliyemsusa mkewe kwa kumfananisha na mama mzazi wake.
Rejea Qur'an (58:1-4).



3. Kufunga siku tatu mfululizo kama kafara kwa muislamu aliyevunja kiapo.
Rejea Qur'an (5:89).



4. Kufunga miezi miwili mfululizo kwa mume na mke waliofanya jimai (tendo la ndoa) mchana wa mwezi wa Ramadhani.



5. Kufunga kama kitubio cha muislamu aliyewinda na hali yuko katika Ihram.
- Idadi ya siku inategemea na thamani ya kile alichokiua (alichokiwinda).
- Kama hana uwezo wa kufunga, atatoa fidia ya mbuzi au kondoo.
Rejea Qur'an (5:95).



6. Kufunga siku 10, tatu akiwa Makkah na 7 baada ya kurejea nyumbani kwa muislamu aliyevunja miiko ya Ihram.
- Kama hana uwezo wa kufunga, atafidia kwa kuchinja mbuzi au kondoo.
Rejea Qur'an (2:196).



Siku zilizoharamishwa kufunga Sunnah.
i. Siku ya Sikukuu ya Iddil-Fitri na Iddil-Hajj.
- Ni haramu kufunga siku za Idd mbili hizi kwa namna yeyote ile.
ii. Siku za Tashriiq.
- Siku za tashriiq ni tarehe 11 ' 13, mwezi wa Dhul-Hajj.
iii. Siku ya shaka.
- Ni siku ya tarehe 29 au 30 mwezi Shaaban kabla ya mwezi wa Ramadhan.
iv. Siku ya Ijumaa.
- Haifai kufunga siku ya Ijumaa tu, isipokuwa kwa aliyekuwa na tabia ya kufunga Sunnah na ikatokea funga ya sunnah ni siku ya Ijumaa.



                   



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 603


Download our Apps
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Twahara na namna ya kujitwaharisha, nguzo zake na sunna zake
Soma Zaidi...

NAMNA ZA ZAKA (AINA NA MGAWANYIKO WA ZAKA) ZAKA IPO MAKUNDI MANGAPI?
Soma Zaidi...

Maana ya Swaumu na Lengo la kufunga
Soma Zaidi...

Ibrahiim(a.s) Aomba Kupata Kizazi Chema
Nabii Ibrahiim na mkewe Sarah walikaa mpaka wakawa wazee bila ya kupata mtoto. Soma Zaidi...

Kujiepusha na Shirk
Shirki ni kitendo chochote cha kukipa kiumbe nafasi ya Allah (s. Soma Zaidi...

HISTORIA YA MTUME YUNUS(A.S)
Nabii Yunus(a. Soma Zaidi...

Uovu wa kumzulia Muumini Uzinifu na Maovu mengine na Hukumu dhidi ya Wazuaji
Kumzulia mtu mtwahirifu kuwa amefanya tendo la zinaa pasina kuleta ushahidi stahiki ni tendo ovu mno mbele ya Allah (s. Soma Zaidi...

Makemeo juu ya Zinaa na Hukumu kwa Wazinifu.
Tendo la zinaa ni tendo chafu kimaadili na Allah (s. Soma Zaidi...

Ni kwa nini lengo la Funga na swaumu halifikiwi na wafungaji?
Kwa nini Lengo la Funga halifikiwi na Wafungaji Wengi? Soma Zaidi...

Nini maana ya Husda, na ni yapi madhara yake
34. Soma Zaidi...

TAREKH, HISTORIA NA SIRA YA UISLAMU NA MTUME MUHAMMAD KUTOKA KUZALIWA MPAKA KUFARIKI NA HARAKATI ZAKE
1. Soma Zaidi...

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEPANDWA NA PRESHA
Presha ya kupanda hutokea pale kipimo kinaposoma zaidi ya 120/80mm Hg. Soma Zaidi...