Funga za suna na funga za kafara na nadhiri: Masharti yake, nguzo zake na wakati wa kutekeleza

Funga za Sunnah.

Funga za suna na funga za kafara na nadhiri: Masharti yake, nguzo zake na wakati wa kutekeleza

Funga za suna na funga za kafara na nadhiri: Masharti yake, nguzo zake na wakati wa kutekeleza

Funga za Sunnah.
- Nia ya kufunga Sunnah inaweza kutiwa muda wowote ule kabla ya Adhuhuri
iwapo mfungaji hakuonja chochote tangu Alfajir.
- Kuna hiari ya kuvunja funga ya Sunnah muda wowote ule pindi itakapobidi.



Umuhimu wa funga za sunnah.
1.Ni kumtii na kumuiga Mtume (s.a.w).
2.Ni kujazilizia mapungufu ya funga ya faradhi.
3.Humuwezesha muumini kufikia lengo la funga (kuwa Wacha-Mungu).
oFunga za Sunnah na namna ya kutekeleza.
a)Kufunga siku tatu kila mwezi.
- Ni kufunga siku tatu mfululizo za mbalamwezi, mwezi 13, 14 na 15.



b)Kufunga ya siku ya Jumatatu na Al-khamisi.
- Jumatatu ni siku aliyozaliwa Mtume (s.a.w) na Al-khamisi ni siku kupandishwa amali za mja kwenda kwa Mola wake.



c)Kufunga siku sita za mwezi wa Shawwal.
- Ni kufunga sita mara baada ya mwezi wa Ramadhani kuisha.



d)Funga ya Arafa.
- Ni kufunga siku ya mwezi 9, Dhul-Hijj ambamo mahujaji wako katika kisimamo katika uwanja wa Arafa.

e)Funga ya Ashura.
- Ni kufunga siku ya mwezi 10, Muharram (mfungo nne). Ni siku aliyookolewa Nabii Musa na Bani Israil kutoka kwa utawala wa Firaun.



f) Funga katika mwezi Shaaban.
- Ni kufunga kwa wingi katika mwezi wa Shaaban bila ya kutimiza siku 30.



Funga za Kafara.
- Ni funga anazolazimika muislamu kufunga ili ziwe kitubio au fidia baada ya kutenda kosa fulani.

Aina za funga za kafara.
1. Kufunga miezi miwili mfululizo kwa muislamu aliyemuua mtu kwa bahati mbaya na akakosa mali ya kulipa fidia.
Rejea Qur’an (4:92).


2. Kufunga miezi miwili mfululizo kwa muislamu aliyemsusa mkewe kwa kumfananisha na mama mzazi wake.
Rejea Qur’an (58:1-4).



3. Kufunga siku tatu mfululizo kama kafara kwa muislamu aliyevunja kiapo.
Rejea Qur’an (5:89).



4. Kufunga miezi miwili mfululizo kwa mume na mke waliofanya jimai (tendo la ndoa) mchana wa mwezi wa Ramadhani.



5. Kufunga kama kitubio cha muislamu aliyewinda na hali yuko katika Ihram.
- Idadi ya siku inategemea na thamani ya kile alichokiua (alichokiwinda).
- Kama hana uwezo wa kufunga, atatoa fidia ya mbuzi au kondoo.
Rejea Qur’an (5:95).



6. Kufunga siku 10, tatu akiwa Makkah na 7 baada ya kurejea nyumbani kwa muislamu aliyevunja miiko ya Ihram.
- Kama hana uwezo wa kufunga, atafidia kwa kuchinja mbuzi au kondoo.
Rejea Qur’an (2:196).



Siku zilizoharamishwa kufunga Sunnah.
i. Siku ya Sikukuu ya Iddil-Fitri na Iddil-Hajj.
- Ni haramu kufunga siku za Idd mbili hizi kwa namna yeyote ile.
ii. Siku za Tashriiq.
- Siku za tashriiq ni tarehe 11 – 13, mwezi wa Dhul-Hajj.
iii. Siku ya shaka.
- Ni siku ya tarehe 29 au 30 mwezi Shaaban kabla ya mwezi wa Ramadhan.
iv. Siku ya Ijumaa.
- Haifai kufunga siku ya Ijumaa tu, isipokuwa kwa aliyekuwa na tabia ya kufunga Sunnah na ikatokea funga ya sunnah ni siku ya Ijumaa.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 3258

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 web hosting    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Mtazamo wa uislamu juu ya ndoa ya mke zaidi ya mmoja

Je jamii inachukuliaje swala la kuoa mke zaidi ya mmoja.

Soma Zaidi...
Shart kuu nne za swala

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu masharti ya swala.

Soma Zaidi...
Sifa za kuwa maamuma kwenye swala na namna ya kumfuata imamu

Post hii inakwenda kukuelezea sifa za kuwa maamuma na taratibu za kumfuata imamu.

Soma Zaidi...
Jukumu la serikali katika kuzuia dhuluma

Serikali ina nafasi kubwa katika kuzuia dhulma na kufanya uchumibuwe huru kuyokana na dhulma.

Soma Zaidi...
Mambo muhimu ya kuzingatia katika kujenga uchumi wa kiislamu

Nazingatio muhimu katika uchumi unaofuata sheria za kiislamu.

Soma Zaidi...
Hatua za kinga za ugumba na Utasa.

Ugumba ni “ugonjwa wa mfumo wa uzazi unaofafanuliwa kwa kushindwa kupata ujauzito baada ya miezi 12 au zaidi ya kujamiiana bila kinga mara kwa mara. Utasa  kutoweza kwa kiumbe hai kufanya uzazi wa ngono au kutoweza kupata mimba au kuchangia mimba.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kusherehekea siku ya idi katika uislamu

Uislamu umeweka taratibu maalumu za kuzifata katika kusherehekea siku ya idi.

Soma Zaidi...