Funga za suna na funga za kafara na nadhiri: Masharti yake, nguzo zake na wakati wa kutekeleza

Funga za Sunnah.

Funga za suna na funga za kafara na nadhiri: Masharti yake, nguzo zake na wakati wa kutekeleza

Funga za suna na funga za kafara na nadhiri: Masharti yake, nguzo zake na wakati wa kutekeleza

Funga za Sunnah.
- Nia ya kufunga Sunnah inaweza kutiwa muda wowote ule kabla ya Adhuhuri
iwapo mfungaji hakuonja chochote tangu Alfajir.
- Kuna hiari ya kuvunja funga ya Sunnah muda wowote ule pindi itakapobidi.



Umuhimu wa funga za sunnah.
1.Ni kumtii na kumuiga Mtume (s.a.w).
2.Ni kujazilizia mapungufu ya funga ya faradhi.
3.Humuwezesha muumini kufikia lengo la funga (kuwa Wacha-Mungu).
oFunga za Sunnah na namna ya kutekeleza.
a)Kufunga siku tatu kila mwezi.
- Ni kufunga siku tatu mfululizo za mbalamwezi, mwezi 13, 14 na 15.



b)Kufunga ya siku ya Jumatatu na Al-khamisi.
- Jumatatu ni siku aliyozaliwa Mtume (s.a.w) na Al-khamisi ni siku kupandishwa amali za mja kwenda kwa Mola wake.



c)Kufunga siku sita za mwezi wa Shawwal.
- Ni kufunga sita mara baada ya mwezi wa Ramadhani kuisha.



d)Funga ya Arafa.
- Ni kufunga siku ya mwezi 9, Dhul-Hijj ambamo mahujaji wako katika kisimamo katika uwanja wa Arafa.

e)Funga ya Ashura.
- Ni kufunga siku ya mwezi 10, Muharram (mfungo nne). Ni siku aliyookolewa Nabii Musa na Bani Israil kutoka kwa utawala wa Firaun.



f) Funga katika mwezi Shaaban.
- Ni kufunga kwa wingi katika mwezi wa Shaaban bila ya kutimiza siku 30.



Funga za Kafara.
- Ni funga anazolazimika muislamu kufunga ili ziwe kitubio au fidia baada ya kutenda kosa fulani.

Aina za funga za kafara.
1. Kufunga miezi miwili mfululizo kwa muislamu aliyemuua mtu kwa bahati mbaya na akakosa mali ya kulipa fidia.
Rejea Qur’an (4:92).


2. Kufunga miezi miwili mfululizo kwa muislamu aliyemsusa mkewe kwa kumfananisha na mama mzazi wake.
Rejea Qur’an (58:1-4).



3. Kufunga siku tatu mfululizo kama kafara kwa muislamu aliyevunja kiapo.
Rejea Qur’an (5:89).



4. Kufunga miezi miwili mfululizo kwa mume na mke waliofanya jimai (tendo la ndoa) mchana wa mwezi wa Ramadhani.



5. Kufunga kama kitubio cha muislamu aliyewinda na hali yuko katika Ihram.
- Idadi ya siku inategemea na thamani ya kile alichokiua (alichokiwinda).
- Kama hana uwezo wa kufunga, atatoa fidia ya mbuzi au kondoo.
Rejea Qur’an (5:95).



6. Kufunga siku 10, tatu akiwa Makkah na 7 baada ya kurejea nyumbani kwa muislamu aliyevunja miiko ya Ihram.
- Kama hana uwezo wa kufunga, atafidia kwa kuchinja mbuzi au kondoo.
Rejea Qur’an (2:196).



Siku zilizoharamishwa kufunga Sunnah.
i. Siku ya Sikukuu ya Iddil-Fitri na Iddil-Hajj.
- Ni haramu kufunga siku za Idd mbili hizi kwa namna yeyote ile.
ii. Siku za Tashriiq.
- Siku za tashriiq ni tarehe 11 – 13, mwezi wa Dhul-Hajj.
iii. Siku ya shaka.
- Ni siku ya tarehe 29 au 30 mwezi Shaaban kabla ya mwezi wa Ramadhan.
iv. Siku ya Ijumaa.
- Haifai kufunga siku ya Ijumaa tu, isipokuwa kwa aliyekuwa na tabia ya kufunga Sunnah na ikatokea funga ya sunnah ni siku ya Ijumaa.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 3471

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Siku zilizoharamishwa kufunga Sunnah

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Kumswalia maiti, masharti ya swala ya maiti

Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Adhabu ya mzinifu katika jamii ya kiislamu

(iii) Adhabu ya UzinifuKatika Sheria ya Kiislamu mtu haadhibiwi mpaka atende kwa uwazi matendo yenye kuvuruga utaratibu na amani ya jamii.

Soma Zaidi...
Dhamana ya Kuchunga Ahadi Katika Uislamu

Kuchunga au kutekeleza ahadi ni miongoni mwa vipengele muhimu vya tabia ya muumini wa kweli.

Soma Zaidi...
Mambo anayofanyiwa mtu anayekaribia kufa

Haya ni maandalizi anayofanyiwa mtu aliye katika kilevi cha kifo yaani sakaratul maut

Soma Zaidi...
Taratibu za mahari katika uislamu

Hapa utajifunza taratibu za kutaja mahari katika uislamu.

Soma Zaidi...
Mgogoro wa kuandama kwa mwezi, Je mwezi wa Kimataifa ama kila Mji na mwezi wake?

Mwezi ukionekana sehemu moja, Waislamu wote ulimwenguni watalazimika kufunga?

Soma Zaidi...