1.
1.SURAT AL-FATIHA.
Muhadithina wengi wanaeleza ya kuwa sura hii nzima ilishuka Makka, na toka mwanzo ilikuwa ni sehemu ya maombi ya Waislamu. Hii ndiyo sura iliyotajwa katika aya ya Qur'an, Na kwa yakini Tumekwisha kupa (Aya) saba zisomwazo mara kwa mara na Qur'an kubwa (sura 15:88), ambayo ilishuka Makka. Habari zingine zinaeleza ya kuwa sura hii iliteremshwa tena mara ya pili, Madina. Sura hii ilishuka mapema tu Mtume s.a.w. alipoanza kazi.
MAJINA YA SURA HII NA MAANA YAO.
Jina maarufu la sura hii ni Faatihat-ul-Kitaab (Inayofungua Kitabu) (Tirmidhi na Muslim). Baadaye jina hilo lilifupishwa kuwa Surat-ul-Faatihah, au Al-Faatiha. Sura hii imepewa majina mengi, na haya kumi ndiyo yaliyo sahihi zaidi: Al-Faatiha, As-Salaat (Sala), Al-Hamdu (Sifa njema), Ummul-Qur'aan (Mama ya Qur'an), Al-Qur'aan-ul-Adhiim (Qur'an Kubwa) As-Sab'ul-Mathaani (Aya saba zinazosomwa mara kwa mara), Ummul-Kitaab (Mama ya Kitabu), Ash-Shifaa (Ponyo), Ar-Ruqya (Kago), Al-Kanz (Hazina).
Maulamaa wa elimu za Qurani hawakutoa zaidi ufafanuzi wa sababu ya kushuka kwa sura hii. Au jambo hili halikuwashughulisha kabisa.
FADHILA ZA SURA HII
Amesimulia Ibn ‘Abas kuwa “wakati ambao jibril alikuwa amekaa na Mtume akasikia sauti ya mlango uliofunguliwa juu yake akanyanyu kichwa chake kisha akasema “hiyo ni nsauti ya mlango uliopo mbinguni umefunguliwa siku ya leo, na katu haujawahi kufunguliwa ila ni leo tu (ndio mara ya kwanza kufunguliwa). Basi akashuka Malaika kutoka kwenye mlango huu akasema (Jibril) huyu ni malaika ameshuka duniani na hajawahi kushuka kamwe ila ni leo tu akatoa salamu (malaika huyo) kisha akasema (kumwambia mtume) tuo habari za furaha kwa nuru mbili ulizopewa na hakuwahi kupewa mtume yeyote kabla yako kamwe (ambazo ni) surat al-fatiha na aya za mwisho za surat al-baqarah hatusoma herufi yeyote isipokuwa utapewa” (amepokea Muslim). Amesema Mtume “surat al-fatiha ni dawa ya kila gonjwa” amepokea Bayhaqiy)
Umeionaje Makala hii.. ?
Surat Al-Asri imeteremshwa Makka, na hapa utazujuwa sababu za kushuka kwa sura hii
Soma Zaidi...MGAWANYIKO KATIKA QURAN Juzuu, Sura, Aya, Manzil, Qara Wataalamu wa elimu za Qurani katika fani za uandishi na usomaji wameigawanya Qurani katika mafungu ili kuwezesha urahisi kwa wasomaji wa qurani.
Soma Zaidi...Asbsb nuzul surat al alaqa, sababu za kushuka surat alaqa. Sura hii imeshuka Makka na ina aya 19. Ni sura ya 96 katika mpangilio wa Quran.
Soma Zaidi...Surat Al qariah, ni moja katika sura zilizochuka miaka ya mwanzoni mwa utume.
Soma Zaidi...Mada zipo katika makundi mawili ambayo ni madda far-iy na mdada twab-iy.
Soma Zaidi...SURAT AL-FIILSura hii imeteremshwa Makkah na ina Aya Sita pamoja na Basmallah.
Soma Zaidi...