Fadhila za surat al-fatiha na sababu za kushuka kwake

1.

Fadhila za surat al-fatiha na sababu za kushuka kwake

Fadhila za surat al-Fatiha

1.SURAT AL-FATIHA.
Muhadithina wengi wanaeleza ya kuwa sura hii nzima ilishuka Makka, na toka mwanzo ilikuwa ni sehemu ya maombi ya Waislamu. Hii ndiyo sura iliyotajwa katika aya ya Qur'an, Na kwa yakini Tumekwisha kupa (Aya) saba zisomwazo mara kwa mara na Qur'an kubwa (sura 15:88), ambayo ilishuka Makka. Habari zingine zinaeleza ya kuwa sura hii iliteremshwa tena mara ya pili, Madina. Sura hii ilishuka mapema tu Mtume s.a.w. alipoanza kazi.



MAJINA YA SURA HII NA MAANA YAO.
Jina maarufu la sura hii ni Faatihat-ul-Kitaab (Inayofungua Kitabu) (Tirmidhi na Muslim). Baadaye jina hilo lilifupishwa kuwa Surat-ul-Faatihah, au Al-Faatiha. Sura hii imepewa majina mengi, na haya kumi ndiyo yaliyo sahihi zaidi: Al-Faatiha, As-Salaat (Sala), Al-Hamdu (Sifa njema), Ummul-Qur'aan (Mama ya Qur'an), Al-Qur'aan-ul-Adhiim (Qur'an Kubwa) As-Sab'ul-Mathaani (Aya saba zinazosomwa mara kwa mara), Ummul-Kitaab (Mama ya Kitabu), Ash-Shifaa (Ponyo), Ar-Ruqya (Kago), Al-Kanz (Hazina).

Maulamaa wa elimu za Qurani hawakutoa zaidi ufafanuzi wa sababu ya kushuka kwa sura hii. Au jambo hili halikuwashughulisha kabisa.



FADHILA ZA SURA HII

Amesimulia Ibn 'Abas kuwa 'wakati ambao jibril alikuwa amekaa na Mtume akasikia sauti ya mlango uliofunguliwa juu yake akanyanyu kichwa chake kisha akasema 'hiyo ni nsauti ya mlango uliopo mbinguni umefunguliwa siku ya leo, na katu haujawahi kufunguliwa ila ni leo tu (ndio mara ya kwanza kufunguliwa). Basi akashuka Malaika kutoka kwenye mlango huu akasema (Jibril) huyu ni malaika ameshuka duniani na hajawahi kushuka kamwe ila ni leo tu akatoa salamu (malaika huyo) kisha akasema (kumwambia mtume) tuo habari za furaha kwa nuru mbili ulizopewa na hakuwahi kupewa mtume yeyote kabla yako kamwe (ambazo ni) surat al-fatiha na aya za mwisho za surat al-baqarah hatusoma herufi yeyote isipokuwa utapewa' (amepokea Muslim). Amesema Mtume 'surat al-fatiha ni dawa ya kila gonjwa' amepokea Bayhaqiy)



                   



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 421


Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Madhara ya matusi katika jamii, na Kujiepusha na Matusi
15. Soma Zaidi...

hukumu na taratibu za biashara ya ushirika na hisa katika uislamu
Soma Zaidi...

Sifa za waumini katika quran
Soma Zaidi...

tawhid
Soma Zaidi...

HUYU NDIYE MUUMINI WA KWELI KATIKA UISLAMU
' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ?... Soma Zaidi...

MTUME MUHAMMAD (S.A.W)ANAKUTANA NA BAHIRA (MTAWA WA KIYAHUDI)
KUKUTANA NA BAHIRA (MTAWA) WA KIYAHUDIMzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara. Soma Zaidi...

Hadhi na Haki za mwanamke katika jamii za kiafrika hapo zamani
3. Soma Zaidi...

Dalili (Alama) za Qiyama
Soma Zaidi...

Nini maana ya twahara katika uislamu, na ni zipi njia za kujitwharisha
1. Soma Zaidi...

SWALA
1. Soma Zaidi...

AINA KUU ZA VYAKULA: vyakula vya protini, wanga, fat na mafuta, vitamini, madini na maji
Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote Soma Zaidi...

UANDISHI WA HADITHI WAKATI WA MASWAHABA
Wakati wa Masahaba wa Mtume (s. Soma Zaidi...