Aina ya kisukari inayojulikana kama Diabety type 1
Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kisukari Aina ya kwanza ambapo kwa kitaalamu huitwa Diabetes type 1, ni hali ambayo utokea ambapo mwili ushindwa kutengeneza insulini ambayo uweka sukari kwenye hali ya usawa.
Aina ya kwanza ya kisukari.
1.Ugonjwa huu wa kisukari utokea kwa Aina kuu mbili, Aina ya kwanza ni pale ambapo mwili inashindwa kabisa kuzalisha insulin kwa hiyo mgonjwa maisha yake yote anaishi kwa kuchomwa insulin, kwa hiyo mgonjwa anaishi kwa kutumia insulin maisha yake yote, hii Aina ya kisukari pengine mtu anazaliwa nayo na maisha yake yote anaishi kwa kutumia insulini Ili iweze kuweka kiwango Cha sukari katika usawa. Kwa hiyo mgonjwa anapaswa kujua hali yake kwa ujumla Ili kuweza kushika masharti yabayohitajika.
2. Ugonjwa huu wa kisukari Aina ya kwanza usababishwa na kuaribika kwa seli ambazo zimo kwenye kongosho seli hizi kwa kitaamu huitwa beta seli na Alfa seli ambazo kazi zake ni kuweka kiwango Cha sukari kwenye hali ya usawa, kwa hiyo hii Aina ya kisukari ni shida kuiweka sawa bila kutumia insulini, kwa hiyo tunapaswa kuwa waaminifu katika kutumia insulin mara nyingi hii Aina ya kisukari kama mtu hajazaliwa nayo ugundulika pale mtu akiwa na miaka chini ya thelathini.
3. Kuna sababu ambao upelekea kuwepo kwa ugonjwa huu kama vile , Kuna wakati mwingine mwili uzalisha antibodies ambazo uharibu beta seli zinazokuwepo kwenye kongosho kwahiyo antibodies hizi zinafanya seli ambazo zimo kwenye kongosho kushindwa kufanya kazi yake na baadae sukari kwenye mwili inashindwa kuwa sawa na hatimaye insulin utumika kila siku kwa mgonjwa na kusaidia kuweka sukari katika hali ya usawa. Na kufanya maisha ya mtu kuendelea kuwa kawaida.
4.pengine hali hii ya kuwepo kwa Aina hii ya kwanza ni kwa sababu za kuurithi kutoka kwenye familia kwa sababu Kuna familia ambapo Kuna Aina hii ya sukari Aina ya kwanza kwa sababu ya gene pengine Kuna shida katika kufanya kazi katika kongosho ambalo usababisha seli zinashindwa kufanya kazi yake kwa sababu ya kuridhi kutoka katika familia. Kwa hiyo tunapaswa kuwa macho na kuchunguza matatizo haya kama yako kwenye ukoo na kuyafanyia kazi.
5. Sababu nyingine ya chanzi Cha kuwepo kwa Aina ya kwanza ya sukari ni Ile hali ya kumpatia mtoto mapema kuanza kutumia maziwa ya ngombe na kutumia madini ya nitrate usababisha kuaribika kwa seli ambazo zimo kwenye kongosho kwa hiyo watoto wanapaswa kula kwa mda mwafaka na kuzuia kutumia maji yenye nitrate na mtoto kama hakufanikiwa kupata maziwa ya Mama kwa sababu mbalimbali anapaswa kuonana na wataalam wa afya Ili kumwonyesha maziwa anavyopaswa kutumia siyo kutumia maziwa ya ngombe kwa mda mrefu.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 ai web app 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Zifahamu sofa za seli
Seli ni chembechembe hai ambazo zimo ndani ya mwili wa binadamu na hufanya kazi mbalimbali kwenye mwili, binadamu hawezi kuishi bila seli.
Soma Zaidi...NINI SABABU YA VIDONDA VYA TUMBO
NENO LA AWALI Hapa utaweza kujifunza mambo mengi kuhusu vidonda vyatumbo.
Soma Zaidi...Fahamu Ugonjwa unaosababisha madhara kwenye mapafu
Posti hii inaelezea kuhusiana na Magonjwa yanayosababisha madhara kwenye mapafu na kitaalamu hujulikana Ugonjwa wa Acute Respiratory Distress Syndrome (ARDS) hutokea wakati Majimaji yanapojaa kwenye vifuko vidogo vya hewa nyororo (alveoli) kwenye mapafu
Soma Zaidi...Ukiwa na aleji , afu kupata muwasho korodani unapo jikuna unga kutoka nayo fangasi?
Swali langu: Ukiwa na areji , afu kupata muwasho korodani unapo jikuna unga kutoka nayo fangasi?
Soma Zaidi...Dalili za za kuwepo kwa maambukizi chini ya kitovu
Posti hii inahusu zaidi dalili za kuonyesha kuwa Kuna maambukizi kwenye kitovu hasa hasa chini ya kitovu.
Soma Zaidi...Maumivu ya tumbo kwa chini upande wa kushoto
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo chini upande wa kushoto
Soma Zaidi...