Kuepuka Maongezi yasiyo na Maana

12.

Kuepuka Maongezi yasiyo na Maana

12. Kuepuka Maongezi yasiyo na Maana


Maongezi au mazungumzo yasiyo na maana ni yale yasiyoleta manufaa au kheri yoyote ila hasara tu. Mazungumzo haya yapo katika kupiga soga, kupiga porojo, kupiga hadithi za pauka pakawa, kutaniana, kubishana, na mengine ya namna hiyo. Mara zote mazungumzo ya aina hii huwapelekea watu kusengenya, kusema uwongo, kufitinisha, kugombana na kupoteza muda. Aidha mazungumzo ya aina hii huwasahaulisha watu kumkumbuka Allah (s.w).
Muumini hana budi kujiepusha na tabia hii ya kujiingiza kwenye mazungumzo ya upuuzi. Miongoni mwa sifa za waumini ni pamoja na kujiepusha na mambo ya upuuzi kama tunavyojifunza katika Quran:


'Hakika wamefuzu Waumini. Ambao katika Sw ala zao ni wanyenyekevu. Na ambao hujiepusha na mambo ya upuuzi'. (23:1-3).
Waja wema mbele ya Allah ni pamoja:

'Na wale ambao hawashuhudii uwongo na wanapopita penye upuuzi hupita kwa heshima (zao). (25:72).
Muislamu anashauriwa daima abaki kimya kama hana la maana la kuzungumza. Mtume (s.a.w) ametuusia:
'Kuwa kimya. Hii ni njia ya kumfukuza shetani na kuimarisha dini yako' (Ahm ad).

'Anayekuwa kimya (anayenyamaza wakati hana la maana la kuzungumza) atakuw a salama '. (Ahmad, tirmidh).
'Ni jambo bora mno kwa Muumini kuacha yasiyomhusu' (Ma lik, Ahm ad, Tirm idh).
'Ni katika ubora wa Imani ya mtu kwa kuacha kujihusisha na mambo ya upuuzi'. (Tirm idh).



                   



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 156


Download our Apps
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

kuwa na ikhlas
Ikhlas ni kufanya kila jambo jema kwa ajili ya Allah (s. Soma Zaidi...

Haki na Hadhi za Mwanamke katika jamii za mashariki: China, India na Japani hapo zamani
2. Soma Zaidi...

Mtazamo na Msimamo wa Uislamu Juu ya Kudhibiti Uzaz (uzazi wa mpango) na hukumu yake
Soma Zaidi...

Ni nini maana ya ndoa?
Soma Zaidi...

AMRI YA KUMFUATA MTUME (s.a.w9)
Amri ya Kumfuata Mtume (s. Soma Zaidi...

Sababu za kushuka kwa Surat Al-Asr
Surat Al-Asri imeteremshwa Makka, na hapa utazujuwa sababu za kushuka kwa sura hii Soma Zaidi...

Mitume waliosimuliwa katika Qur-an ni hawa ishirini na tano (25) wafuatao:
Adam (a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII ADAM
Soma Zaidi...

Kitabu Cha Darsa za Quran
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

Kuporomoka kwa Dola ya Kiislamu
Soma Zaidi...

Vinywaji salama kwa mwenye kisukari
Vijuwe vinywaji salama kwa mgonjwa wa kisukari Soma Zaidi...

Quran si maneno ya mwenye kifafa
Soma Zaidi...