haki na wajibu kwa watumishi wa nyumbani (house boy and house girl)

haki na wajibu kwa watumishi wa nyumbani (house boy and house girl)

Wajibu kwa Watumishi wa Nyumbani



Mara nyingi katika familia panakuwa na watumishi wanaoajiriwa kusaidia kufanya kazi mbali mbali za nyumbani kama vile uyaya, upishi, utunzaji bustani, udobi, na kadhalika. Uislamu umetukumbusha kuwa mtu kupata wasaa wa kuweka mtumishi wa nyumbani au katika sehemu yeyote ile, sikuwa yeye ni bora kuliko huyo mtumishi, bali ni katika utaratibu wa Allah (s.w) kuwa amewafadhilisha baadhi ya watu juu ya wengine ili wapate kutegemeana. Kama hivi, tajiri anamuhitajia mtumishi na mtumishi anamuhitajia tajiri. Kila mmoja ni muhimu kwa mwingine. Ni katika msingi huu tunawajibika kuwatendea wema watumishi kama ndugu zetu kama inavyohimizwa katika Hadith zifuatazo:
Abdullah bin Omar (r.a) ameeleza kuwa alikuja mtu mmoja kwa Mtume wa Allah na kuuliza, "Ee Mtume wa Allah ni mara ngapi tutamsamehe mtumishi? Mtume alinyamaza kimya. Kisha akamuuliza tena swali lile lakini Mtume (s.a.w) alibaki kuwa kimya. Lilpoulizwa swali lile kwa mara ya tatu Mtume al/ibu: "Msamehe mara sabini (70) kila si/cu." (Abu Daud)



Abu Dharr ameripoti kuwa Mtume wa Allah amesema: "Allah (s.w) amewajaalia ndugu zenu kuwa chini ya mikono (mamlaka) yenu. Yeyote yule atakayejaaliwa kuwa na mamlaka juu ya ndugu yake, basi na amlishe chakula anachokula yeye, na amvishe kivazi anachovaa yeye na asimpe kazi zinazomzidi kimo (uwezo). Kama atampa kazi zilizo nje ya uwezo wake basi na amsaidie." (Bukhari na Muslim)



Hadithi hizi zinatufundisha kuwa tuishi vizuri na watumishi wetu na wale tunaoishi nao katika familia walio chini ya milki yetu. Tunafundishwa kuwa wakitukosea tusiwanyanyase na kuwapatiliza bali tuwasamehe na kuwaongoza. Vile vile tunawajibika kuwalipa watumishi wetu kwa uadilifu kwa mujibu wa mkataba wa kazi na tusiwaongezee kazi nje ya zile zilizo katika mkataba. Kwa ujumla, tunawajibika kuishi kindugu na wale walio katika miliki zetu katika familia kwa kuwapa kazi zinazolingana na uwezo wao, kuwapa msaada katika kazi zilizo wazidi kimo na kuwahudumia kwa chakula, mavazi na malazi katika kiwango kile kile tunachojihudumia wenyewe na watoto wetu.



Kuwanyanyasa na kuwafanyia ukatili watumishi wetu na wale tunaokaanao chini ya milki zetu ni katika makosa makubwa mbele ya Allah (s.w) na ni mkosi kama tunavyojifunza katika Hadith zifuatazo: Abu Bakr Siddiq (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: "Hataingia peponi yule anayewatendea vibaya (anayewafanyia ukatili) wale walio chini ya mamlaka yake." (Tirmidh, Ibn Majah).



Raafi 'I bin Makiith (r. a) arneeleza kuwa Mturne wa Allah am eserna: "Kuwatendea wema watu waliochini ya mamlaka yako huleta baraka(fortunes) na kuwafanyia ukatili vi urn be chini ya mamlaka yako, huleta rnikosi (misfortunes)" (Abu Daud). Pamoja na kuzingatia mafundisho ya Hadithi hizi hatunabudi kumuangalia Mtume (s.a.w) ambaye ni kiigizo chetu, namna alivyokuwa akiwatendea wema watumishi wake, katika Hadith zifuatazo:



Anas (r. a) ameeleza: "Nilianza kumtumikia Mtume wa Allah nilipokuwa mvulana wa miaka tisa. Nilimtumikia kwa miaka kumi. Hakunigombeza kwa chombo chochote nilichovunja. Pale yeyote katika familia yake alponigombeza kwa hili au lile alikuwa akimwambia: Mwache kwa sababu, kila kitu kimekadiriwa mwisho wake, ni lazima kiondoke." (Baihaqi).


Vile vile katika Hadithi nyingine Anas (r.a) anaeleza:
Mtume wa Allah alikuwa mbora wa watu katika tabia. Siku moja alinituma mahali. Kwa jina la Allah nilisema, 'Sitaenda' lakini, katika mawazo yangu nikaona sinabudi kwenda aliponituma Mtume wa Allah. Kisha nilitoka kwenda. Njiani nikakutana na watoto waliokuwa wakicheza katika maeneo ya sokoni.Nikiwa pale, Mtume wa Allah alikuja nyuma yangu na kunishika mkono.Nilipogeuka na kutazama nikaona ni Mtume wa Allah Akaniuliza, huku akitabasamu, "Ee mpendwa Anas! Umeshakwenda kule nilikokutuma?" Nil j/ibu: "Ndio Ee Mtume wa Allah, ninakwenda" (Muslim)



Tunajifunza kutokana na Hadith hizi kuwa hatunabudi kuwatendea wema watumishi wetu na wale wote waliochini ya mamlaka yetu katika familia. Katika kusisitiza hili turejee tena Hadithi aliyosimulia Aysha (r.a) kuwa amemsikia Mtume (s.a.w) akisema:
Mbora miongoni mwenu ni yule aliye mbora katika (kuwatendea wema) familia yake na (mimi) ni mbora wenu katikafamilia yangu..." (Ibn Majah)




                   




Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 218


Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Hekma katika hukumu za mirathi katika uislamu, na ni kwa nini wanaume wanazidi katika kurithi katika uislamu
Soma Zaidi...

Neema za Allah(s.w) Juu ya Bani Israil
Katika Qur'an tunakumbushwa neema mbali mbali walizotunukiwa Bani Israil (Mayahudi) na Mola wao ili kuwawezesha kusimamisha Ufalme wa Allah(s. Soma Zaidi...

NGUZO ZA IMAN
Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala Soma Zaidi...

Kujiepusha na Shirk
Shirki ni kitendo chochote cha kukipa kiumbe nafasi ya Allah (s. Soma Zaidi...

Harun(a.s), Achaguliwa Kuwa Msaidizi Musa(a.s) na kumkabili (kumlingania) firauni
Nabii Musa(a. Soma Zaidi...

quran na sayansi
2; mbegu ya uhai uliyo changanyikaUmbile la mwanadamu limepitia hatua nyingi sana kama tutakavyoendelea mbele kuonalakini ukiachilia mbali na hatua zote alizopitia mwanadamu wakati wa kuumbwa lakiniumbile la mwanadamu bado limebakia kuwa dhalili kama ALLA Soma Zaidi...

WAQFU WAL-IBTIDAAI
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Tofauti ya uchumi wa kiislamu na usio wa kiisalmu
Tofauti kati ya mfumo wa uchumi wa Kiislamu na ile ya Kitwaghuti (i) Dhana ya mafanikioKatika mtazamo wa uchumi wa Kiislamu mafanikio yanatazamwa kwa kuzingatia hatima ya ama mtu kupata radhi za Mwenyezi Mungu au kubeba laana ya Mwenyezi Mungu. Soma Zaidi...

Quran na sayansi
3; Mchujo wa maji dhaliliKatika aya nyingine tunakuja kupata funzo kuwa maji aliyoumbiwa mwanadamu licha yakuwa na sifa zilizotajwa katika kurasa zilizopita ila pia maji haya yanasifa kuwa ni madhalilina pia na yamechujwa kama tunavyoelezwa katika quran?? Soma Zaidi...

Uchambuzi wa Neema Alizopewa Nabii Sulaiman(a.s)
(i) Kutiishiwa Upepo Qur'an inatufahamisha kuwa Nabii Sulaiman alitiishiwa upepo akaweza kuutumia apendavyo kwa amri yake. Soma Zaidi...

njia ya maandishi
Soma Zaidi...

As-Sab nuzul
Sababu za kuteremshwa baadhi ya sura Katika darsa hii tutaangalia sababu za kushuka kwa aya na sura ndani ya quran. Soma Zaidi...