Mipaka katika kumtii mzazi, na mambo yasiyopasa kumtii mzazi

Mipaka katika kumtii mzazi, na mambo yasiyopasa kumtii mzazi

Mipaka katika kuwatii Wazazi



Pamoja na msisitizo huu mkubwa wa kuwatii wazazi, utii wetu kwao ni lazima ulandane na utii wetu kwa Mwenyezi Mungu (s.w) na Mtume wake. Endapo watatuamrisha tufanye jambo lolote lile Iinalokwenda kinyume na maamrisho ya Mwenyezi Mungu (s.w) na Mtume wake tutalazimika kutowatii na kubakisha utii wetu kwa Mwenyezi Mungu (s.w) na Mtume wake kama inavyobainishwa katika aya zifuatazo:



Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake; na kama wakikushurutiza kunishirikisha na yale usiyo na ilimu nayo, basi usiwatii, kwangu ndiyo marejeo yenu, basi nitakwambieni mliyokuwa mkiyatenda. (29:8).


Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii, lakini kaa nao kwa wema hapa duniani; shika njia ya wale wanaoelekea kwangu, kisha marejeo yenu ni kwangu, hapo nitakuambieni mliyokuwa mkiyatenda. (3 1:15).



Hata hivyo, pamoja na aya hizi kutukataza kuwa tusiwatii wazazi wetu endapo watatuamrisha kumshikirikisha Mwenyezi Mungu (utii kwa yeyote yule kinyume na Mwenyezi Mungu ni shiriki), bado tunasisitizwa tuwaheshimu, tuwahurumie na kuwatendea wema kwa kadiri ya uwezo wetu wote katika mambo yote ya kheri. Hana radhi ya Mwenyezi Mungu (s.w) yeyote yule atakayewavunjia heshima na kuwatendea visivyo wazazi wake na hata wazazi wa wengine. Hebu tuzingatie Hadith ifuatyo:



Abdallah bin Umar amesimulia kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema:Katika madhambi makubwa, ni mtu kuwatukana wazazi wake. Wakauliza (Maswahaba); Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Mtu anawezaje kuwatukana wazazi wake? "Ndio" al/ibu Mtume, anamtukana baba wa mwingine ambaye humrudishia kwa kumtukania baba yake na anamtukana mama wa mwingine ambaye humrudishia tusi hilo kwa mama yake. (Bukhari na Muslim).




                   




Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 142


Download our Apps
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Kitabu Cha Dua 120
Sifanjema zinamstahikia Allah Mola wa viumbe vyote. Soma Zaidi...

sadaka
Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII DAUD
Soma Zaidi...

.Mazingatio muhimu katika uchumi wa Kiislamu
3. Soma Zaidi...

Athari na faida za kumuamini Allah katika maisha ya mwanadamu duniani na akhera
Athari za Kumuamini Mwenyezi Mungu (s. Soma Zaidi...

Utoaji wa zaka katika Dhahabu, fedha ama silva na pesa
Soma Zaidi...

HISTORIA YA BI KHADIJA (HADIJA) MKE WA KWANZA WA MTUME MUHAMMAAD (S.A.W)
HISTORIA YA BI KHADIJABi Khadija jinalake halisi ni Khadija bint Khuwald bin Asab baba yake alikuwa ni mfanya biashara. Soma Zaidi...

kuwa mwenye kusamehe, na faida zake
27. Soma Zaidi...

Kiwango cha mahari katika uislamu
Kiasi gani Kinachojuzu kutolewa Mahari? Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Shu'ayb(a.s).
Kutokana na kisa cha Nabii Shu'ayb(a. Soma Zaidi...

Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Furqaan (25:64-76)
Soma Zaidi...

Aina za talaka, sharti zake na taratibu za kutaliki katika uislamu
Maana: ni utaratibu wa kuvunja mkataba wa ndoa baina ya mume na mke mbele ya mashahidi wawili kwa kuzingatia sheria ya Kiislamu. Soma Zaidi...