Dhana ya haki na uadilifu katika uislamu

HAKI NA UADILIFU KATIKA UISLAMU.

Dhana ya haki na uadilifu katika uislamu

HAKI NA UADILIFU KATIKA UISLAMU

HAKI NA UADILIFU KATIKA UISLAMU.
1. Dhana ya Haki na Uadilifu katika Uislamu.
Maana ya Haki kwa Mtazamo wa Uislamu.
Ni muunganiko wa sheria na maadili kwa lengo na madhumuni ya kuilea jamii katika amani, furaha, udugu wa kweli na mahusiano mema kati ya wanaadamu.


Misingi ya Haki na Uadilifu katika Uislamu.
Maisha ya furaha na amani ya kweli hupatikana kwa kusimama misingi ya haki na Uadilifu katika jamii kama ifuatavyo;
i.Tawhiid.
Haki na Uadilifu wa kweli hupatikana kwa kumuamini na kumpwekesha Mwenyezi Mungu (s.w) ipasavyo katika maamrisho na makatazo yake.

ii.Utume.
Katika kumuamini na kumpwekesha Mwenyezi Mungu (s.w) ni kufuata misingi ya miongozo ya mitume wake wote kupitia vitabu vyao.

iii.Siku ya Mwisho.
Kumpwekesha Mwenyezi Mungu (s.w) katika maisha yetu ni kuzingatia kuwa kila kitendo kitahukumiwa na kulipwa kwa haki siku ya Kiyama.


Aina au migawanyo mbali mbali ya Haki katika Uislamu.
1.Haki za Allah.
2.Haki za Nafsi.
3.Haki za Viumbe na Mazingira.
4.Haki za Binadamu kwa ujumla.
5.Haki za Raia katika Dola ya Kiislamu.
6.Haki za Maadui katika Vita (mateka).

1.Haki za Mwenyezi Mungu (s.w).
Katika Uislamu haki za Mwenyezi Mungu ziko makundi mawili;
i.Haki ya Uungu.
Ni kumsifu na kumtii kwa sifa zake kama za uumbaji, umilikaji na ulezi wa viumbe vyote na ukamilifu wake tofauti na viumbe alivyoviumba.
Rejea Qur'an (45:23), (25:68), (9:31) na (31:13).

ii.Haki ya Kuabudiwa.
Ni Mwenyezi Mungu (s.w) peke yake ndiye anayestahiki kuabudiwa na viumbe vyake muda wote, na ndio lengo kuu la kuumbwa mwanaadamu.
Rejea Qur'an (51:56), (5:44), (11:25-26) na (29:16-17).

2.Haki za Nafsi.
Haki za nafsi imekokotezwa kuanzia binafsi, familia, wazazi, n.k kama ifuatavyo;
(a)Mtu Binafsi.
Haki za msingi ni chakula, makazi, malezi, elimu, mavazi, matibabu na kufanyia kazi vipaji na neema alizonazo inavyostahiki ikiwemo;


Haki ya Macho.
Ni kutazama yaliyoamrishwa na kuyaepusha na yaliyoharamishwa.
Rejea Qur'an (17:36), (41:20), (24:30-31) na (20:131).

Haki ya Masikio.
Ni kusikiliza yaliyoamrishwa na kutosikiliza yaliyoharamishwa pia.
Rejea Qur'an (8:22) na (6:25).

Haki ya Midomo na Ulimi.
Ni kula, kunywa na kuzungumza yaliyohalalishwa na sio yaliyoharamu.
Rejea Qur'an (16:114), (17:26-29), (17:53), (41:33) na (31:6).

Haki ya Mikono na Miguu.
Ni kushika na kuendea vyote vilivyoamrishwa na kuacha vilivyokatazwa.
Rejea Qur'an (25:72) na (31:18).

(b) Haki za Familia.
Ni kusimamia malezi, elimu, uadilifu na wajibu wa kila mmoja katika familia kwa muongozo wa Qur'an na Sunnah ili kuleta kufikia lengo la kuumbwa.
Rejea Qur'an (52:21).

(c) Haki za Watoto.
Watoto wana haki ya kupata malezi na makuzi bora kulingana na mahitaji yao kwa mujibu wa mafundisho ya Qur'an na Sunnah katika sehemu zifuatazo;

Haki ya Uhai.
Uhai wa mtoto ni haki itokayo kwa Mwenyezi Mungu (s.w) kupitia malezi na makuzi ya wazazi.

Haki ya Nasaba.
Mtoto kupata nasaba ni haki kisheria ili kuwa mwanafamilia halali.
Rejea Qur'an (33:4).

Haki ya Makuzi na Malezi bora.
Makuzi na malezi bora ya mtoto ni kupata haki zake za msingi na elimu inayomuwezesha kumuabudu Mwenyezi Mungu (s.w) ipasavyo.
Rejea Qur'an (66:6).

(d) Haki za Wazazi.
Ni kuwahurumia, kuwaheshimu, kuwafanyia wema, kuwahudumia na kuwalea ipasavyo.
Rejea Qur'an (31:14), (17:23-24), (4:36), (6:151), (19:14) na (19:32).

(e) Haki za Jamaa na Majirani.
Ni kutunza uhusiano na kusaidiana pale inapohitajika kwa kuzingatia mipaka.
Rejea Qur'an (2:215).

(f) Haki za Mayatima, Wajane na Masikini.
Ni kuwahifadhi na kuwasaidia wanapokuwa na shida na mahitaji ya kimaisha.
Rejea Qur'an (2:220), (4:2), (4:10), (2:262) na (2:267).

(g) Haki za Udugu wa Kiimani na za Watu wengine.
Udugu wa kiimani ni haki na bora zaidi kuliko udugu wa damu au nasaba.
Rejea Qur'an (49:10), (49:13), (7:172-173), (4:7) na (5:8).

3.Haki za Viumbe na Mazingira.
Uislamu umeweka kipaumbele katika kuhifadhi mazingira na kutunza viumbe hai na visivyo hai kupitia sera mbali mbali zikiwemo;
?Haki ya Hifadhi ya Mazingira na misitu.
Rejea Qur'an (6:38), (27:60), (16:10-13), (50:7-9), (56:63-64) na (39:62).

Mazingira ni amana katika kulinda uhai wetu na wa viumbe wengine.
Rejea Qur'an (7:10) na (16:112).

Sera na Mafundisho ya Mtume (s.a.w) juu ya hifadhi ya mazingira katika kuleta ustawi wa jamii.

Sera ya mapinduzi ya kitabia katika kutunza na kuhifadhi mazingira yote yanayotuzunguka.

Sera ya usafi na uhifadhi wa mazingira ili kuleta ustawi wa viumbe hai.
Rejea Qur'an (6:141) na (25:2).

4.Haki za Binaadamu kwa Ujumla (Basic Human Rights).
Uislamu umezingatia, kulinda na kusimamia haki za msingi za kibinaadamu bila kujali tofauti zao. Haki hizo ni pamoja na;
1. Haki za kuishi (maisha).
Rejea Qur'an (5:32), (6:151) na (17:33).

2. Haki ya Usalama wa Maisha.
Rejea Qur'an (5:32).

3. Haki ya kulinda na kuheshimu hadhi na usafi wa mwanamke.
Rejea Qur'an (17:32) na (24:2).

4. Haki ya kupata mahitaji ya lazima ya maisha.
Rejea Qur'an (70:24-25).

5. Haki ya Uadilifu na Usawa katika Hukumu (Righ to justice).
Rejea Qur'an (5:8), (49:13) na (4:135).

6. Haki ya Uhuru (kila mtu kuwa huru).
Uislamu umezingatia kila mtu kuwa huru kifikra na kutomilikiwa kama bidhaa ya baishara.

5.Haki za Raia katika Dola ya Kiislamu.
1. Haki za msingi za raia waislamu na wasiokuwa waislamu katika Dola ya Kiislamu ni pamoja na;
2. Haki ya kuendesha maisha binafsi bila kuingiliwa na mtu yeyote.
3. Haki na uhuru wa kutoa maoni na kuamrisha mema na kukataza mabaya.
Rejea Qur'an (3:104), (9:71), (9:67).

4. Haki na Uhuru katika kufuata na kuabudu dini yeyote aipendayo mtu.
Rejea Qur'an (2:256), (6:108), (29:46) na (16:125).

5. Haki ya Kuwashtaki Viongozi wa juu wa Dola bila upendeleo na ubaguzi wowote.
6. Haki ya kumiliki mali au rasilimali zozote za halali na zisizoleta madhara kwa raia na Dola kwa ujumla.
Rejea Qur'an (2:262), (2:267) na (18:32-43).


6.Haki za Maadui Katika Vita (mateka wa Kivita).
Uislamu unajali, kusimamia na kulinda haki ya kila mtu hata kwa maadui waliokamatwa katika vita (mateka) walifanyiwa haki na uadilifu kama ifuatavyo;

1. Kuhurumiwa na kutofanyiwa ukatili wowote maadamu wamedhibitiwa.
2. Kuwapa mahitaji yao ya lazima ya kibinaadamu na kimaisha pia.
3. Kulinda uhai na usalama wa maisha yao mpaka mwisho wa uhasama.
4. Mateka wa kivita walikuwa na haki ya kujikomboa kwa njia zifuatazo;
5. Kulipa kiasi fulani cha pesa au mali yeyote inayokubalika.
6. Kubadilishana na mateka Waislamu waliokamatwa na maadui.
7. Kulipa fidia kwa kufanya jambo fulani lenye manufaa kwa jamii ya waislamu.
Rejea Qur'an (47:4).

Masuria na mateka wanawake walikuwa na haki ya kulindwa na kuhifadhiwa kwa kupewa wanaume waliokwenda vitani na kuishi nao katika maisha ya ndoa ili kupata mahitaji yao ya msingi.

Haki ya kumiliki mali au uchumi ulio wa halali na usio leta madhara yeyote katika Dola ya Kiislamu.



                   



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 285


Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

MAANA NA FADHILA ZA KUOMBA DUA
DUA Kwa ufupi dua ni kumuomba Allah akuondoshee lililobaya, ama linalo kuudhi ama akupe jambo fulani. Soma Zaidi...

Haki na wajibu wa mtoto kwa wazazi na katika jamii
Soma Zaidi...

Yanayofaa kwa maamuma katika kumfata imamu kwenye swala ya jamaa
Soma Zaidi...

Historia ya Mwanadamu
Soma Zaidi...

Mtume Muhammad hakujuwa kusoma wala kuandika ni hoja na kuna hekima zake
(i)Mtume Muhammad (s. Soma Zaidi...

malezi ya mtoto mchanga baada ya talaka
Soma Zaidi...

haki na wajibu kwa watumishi wa nyumbani (house boy and house girl)
Soma Zaidi...

Kujiepusha na Shirk
Shirki ni kitendo chochote cha kukipa kiumbe nafasi ya Allah (s. Soma Zaidi...

SWALA YA MTUME (s.a.w)
SWALA YA MTUME Kumswalia Mtume (s. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII IBRAHIIM(A.S) NA KUANDALIWA KWAKE:
Nabii Ibrahiim(a. Soma Zaidi...

haki za mwanamke za kisiasa katika uislamu
Haki ya Kushiriki Katika Siasa. Soma Zaidi...

Sababu za kushushwa kwa surat al-kafirum
SURATUL-KAFIRUN Imeteremshwa maka na inaelezwa katika sababu za kushuka kwake ni kuwa Kundi la makafiri lilimfuata mtume (s. Soma Zaidi...