image

Tafsir ya suratul quraysh na mafuzoyake

Tafsir ya suratul quraysh na mafuzoyake

Naomba Tafsir ya suratul quraysh na mafuzoyake



Namba ya swali 000

Suratul-Quraysh (106)

Kwa jina la Allah,mwingi wa Rehma, Mwenye Kurehemu.
1.Ili kuwafanya Makurayshi waendelee.


2.Waendelee na Safari zao za wakati wa kusi (kwenda Yemen) na wakati wa kaskazi (kwenda Shamu).


3.Basi nawamuabudu Bwana wa nyumba hii (Al-Kaaba).


4.Ambaye anawalisha (wakati Waarabu wenzao wamo) katika njaa, na anawapa amani (wakati wenzao wamo) katika khofu.



Namba ya swali 000

Mafunzo yake je?



Namba ya swali 000

Mafunzo kwa Muhtasari



Kutokana na sura hii kwa muhtasari tunajifunza yafuatayo:
(1 )Neema zote zilizotuzunguka zinatoka kwa Allah (s.w).



(2)Amani, usalama na ustawi wa kweli hupatikana kwa kumtii Allah (s.w) ipasavyo. Kwa mfano amani na ustawi wa Makka ulipatikana kutokana na dua ya Nabii Ibrahim (a.s) ambaye kwa kumtii Mola wake aliacha familia yake mahali pakavu na papweke pasipo na msaada wowote wa kibinaadamu. Wakati anatekeleza amri ya Allah (s.w) ya kuiacha familia yake pale, Nabii Ibrahim (a.s) aliomba:



"Mola wetu! Hakika mimi nimewaweka baadhi ya kizazi changu (mwanangu Ismail na mama yake, Hajar) katika bonde (hili la Makka) lisilokuwa na mimea yoyote katika nyumba yako takatifu. Mola wetu! Wajaalie (wawe) wasimamishaji swala. Na ujaalie nyoyo za watu zielekee kwao na uwaruzuku matunda ili wapate kushukuru" (14:37)



3)Mahusiano, maingiliano na mawasiliano baina ya mataifa katika nyanja mbalimbali za kijamii ni katika neema za Allah (s.w)



Namba ya swali 000

Shukraa, Allah akuzidishie Elimu



Namba ya swali 000

Aaamin Nawe pia ndugu yangu, Allah akupe Neema nyingi



Namba ya swali 000





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 970


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Quran si maneno ya shetani
Soma Zaidi...

Hukumu za Tajwid katika usomaji wa bismillah (basmalah)
Hapa utajifunza kanuni za tajwid katika kusoma bismillah au basmalah. Soma Zaidi...

Asbab nuzul surat at Tin, Sababu za kushuka surat at Tin (watin wazaitun)
Post hii itakwenda kukufundisha sababu za kushuka kwa surat at Tin (watin wazaitun). Soma Zaidi...

Mtume hakufundishwa quran na Jabir na Yasir
Soma Zaidi...

Naman ya kuiendea quran na kuifanyia kazi baada ya kuisoma
Soma Zaidi...

sura ya 11
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Sababu za kushushwa kwa surat al-kafirum
SURATUL-KAFIRUN Imeteremshwa maka na inaelezwa katika sababu za kushuka kwake ni kuwa Kundi la makafiri lilimfuata mtume (s. Soma Zaidi...

Uthibitisho kuwa Qur-an ni neno la Allah (s.w)
Uthibitisho kuwa Qur-an ni neno la Allah (s. Soma Zaidi...

Faida za kujuwa Quran tajwid
Hapa nitakufindisha faida za kusoma quran kwa Tajwid. Soma Zaidi...

surat al mauun
SURATUL-MAM’UUN Imeteremshwa Maka, anasimulia Ibn Jurayj kuwa Abuu Sufyan ibn Harb alikuwa na kawaida ya kuchinja ngamia wawili kila wiki, hivyo siku moja yatima mmoja alikuja kwake na kumlilia shida, na hakumsaidia kwa chochote na hatimaye akampiga yat.. Soma Zaidi...

Adabu za kusikiliza quran
ADABU ZA KUSIKILIZA QURANI 1. Soma Zaidi...

Ni nini maana ya Tajwid, na ni ipi nafasi yake kwenye uislamu
Hapa utajifunza maana ya Tajwid kilugha na kisheria. Pia nitakujuza jukumu ya kusoma tajwid. Soma Zaidi...