Tafsir ya suratul quraysh na mafuzoyake

Tafsir ya suratul quraysh na mafuzoyake

Naomba Tafsir ya suratul quraysh na mafuzoyake



Namba ya swali 000

Suratul-Quraysh (106)

Kwa jina la Allah,mwingi wa Rehma, Mwenye Kurehemu.
1.Ili kuwafanya Makurayshi waendelee.


2.Waendelee na Safari zao za wakati wa kusi (kwenda Yemen) na wakati wa kaskazi (kwenda Shamu).


3.Basi nawamuabudu Bwana wa nyumba hii (Al-Kaaba).


4.Ambaye anawalisha (wakati Waarabu wenzao wamo) katika njaa, na anawapa amani (wakati wenzao wamo) katika khofu.



Namba ya swali 000

Mafunzo yake je?



Namba ya swali 000

Mafunzo kwa Muhtasari



Kutokana na sura hii kwa muhtasari tunajifunza yafuatayo:
(1 )Neema zote zilizotuzunguka zinatoka kwa Allah (s.w).



(2)Amani, usalama na ustawi wa kweli hupatikana kwa kumtii Allah (s.w) ipasavyo. Kwa mfano amani na ustawi wa Makka ulipatikana kutokana na dua ya Nabii Ibrahim (a.s) ambaye kwa kumtii Mola wake aliacha familia yake mahali pakavu na papweke pasipo na msaada wowote wa kibinaadamu. Wakati anatekeleza amri ya Allah (s.w) ya kuiacha familia yake pale, Nabii Ibrahim (a.s) aliomba:



"Mola wetu! Hakika mimi nimewaweka baadhi ya kizazi changu (mwanangu Ismail na mama yake, Hajar) katika bonde (hili la Makka) lisilokuwa na mimea yoyote katika nyumba yako takatifu. Mola wetu! Wajaalie (wawe) wasimamishaji swala. Na ujaalie nyoyo za watu zielekee kwao na uwaruzuku matunda ili wapate kushukuru" (14:37)



3)Mahusiano, maingiliano na mawasiliano baina ya mataifa katika nyanja mbalimbali za kijamii ni katika neema za Allah (s.w)



Namba ya swali 000

Shukraa, Allah akuzidishie Elimu



Namba ya swali 000

Aaamin Nawe pia ndugu yangu, Allah akupe Neema nyingi



Namba ya swali 000
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 3137

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Tofauti kat ya sura za Maka na Madina

Sura za Makka na Madina Kutokana na historia ya kushuka kwake sura za Qur-an zimegawanywa katika makundi mawili - sura za Makka na sura za Madina.

Soma Zaidi...
HUKUMU YA NUN SAKINA NA TNWIN

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Makundi ya Id-ghamu katika usomaji wa Quran Tajwid

Kama tulivyoona kuwa id-ghamu ipo katika aina kuu mbili ambazo ni id-ghamu bighunnah na id-ghamu bighair ghumnah. Sasa hapa tutajifunza makundi mengine ya idhgamu.

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA IDGHAM

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
quran na sayansi

YALIYOMONENO LA AWALI1.

Soma Zaidi...
MAANA YA Quran

Maana na majina ya Quran Maana ya Wahyi.

Soma Zaidi...
Sababu za kushushwa kwa surat al-kafirum

SURATUL-KAFIRUN Imeteremshwa maka na inaelezwa katika sababu za kushuka kwake ni kuwa Kundi la makafiri lilimfuata mtume (s.

Soma Zaidi...
Adabu za kusikiliza quran

ADABU ZA KUSIKILIZA QURANI 1.

Soma Zaidi...