Simulizi za Hadithi EP 4 Part 12: Hadithi ya mfalme alikuwa kwenye kisima

Wapendwa tuendelee kuoata stori nzuri na za kusisimua kutoka katika kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA.....

KUTOKA KWENYE KISIMA MPAKA KUWA MFALME.

 

Pale kisimani khalidi aliokolewa na majini waliokuwa wakiishi pale kwa muda wa miaka mingi iliyopita. Hata kabla ya kufika chini walimzi,isha na kumbebe na kumtua kidogokidogo na hakupatwa na madhara. Majini hawa walimpenda Khalidi kwa tabia zake njema na ukarimu uliopambwa na uchamungu wake. Hivyo hawakupenda damu ya mtu mkarimu iumwagike mule kisimani walipokuwa wakiishi.

 

Basi alipokuwa kati ya kupoteza fahamu na kurudi fahamu yaani akiwa kwenye mang’amung’amu akawasikia majini wakizungumza. “unajuwa mtoto wa mfalme wa nchi hii anaumwa sana na inapata miezi sita sasa bila ya kupona” wengine wakawa wanajibu “mimi sijapata kusikia hilo kabisa” kukatokea mmoja akasema “mimi nafahamu dawa ya ugonjwa wake” basi pale yule aliye anzisha mada akamuuliza “ni ipi dawa yake?” akamjibu “nyumbani kwa Khalidi kuna paka mwenye rangi nne na adimu sana paka hawa. Magoya saba ya mkia wa paka huyu ukiyachoma na ubani na harufu ikimpata vilivyo huyo mtoto wa mfalme kwa hakika atapona.

 

Wale majini hawakujuwa kama Khalidi amewasikia. Basi baa da ya muda wakamtoa pale ndani ya kisima. Khalidi alipitiwa na usingizi na aliposhituka akajikuta kitandani kwake. Alipoamka asubuhi akachukuwa magoya saba ya mkia wa ule paka akisubii kuona kama aliuwa anaota au ilikuwani kweli. Siku ile ilienda salama sana na hakukuwa na tatizo lolote, na huku Jalidi akaamini amemuuwa Khalidi,

 

Siku ilofata akaona ugeni unaingia kwake ni mfalme na msafra wake wakija kwakwe ili amuombee dua binti yake aliyekuwa anaumwa kwa miezi sita hata bila ya kupoona. Hapo khalidi akajuwa kumbe haikuwa ndoto ila ni ukweli. Pale akamchukuwa mgonjwa yule na akachukuwa udi na kachanganya na mgoya yale na akaomba dua. Hata kabla ya kumaliza alisikia kishindo. Mgonjwa alianguka chini na kupoteza fahamu.

 

Watu wakaanza kumpepea na mflme alijuwa lamda binti yake amepatwa na jambo. Baada ya masaa kadha akazinduka na hakuhisi maumivu yeyote. Hii inamaanisha alipona kabisa ugonjwa wake. Basi mfalme kwa furaha akamwambia “kijana kwa furaha nilizo nazo sina kikubwa cha kukulipa lakini naomba umuoe binti yangu” Khalidi alikubaliana na mawazo hayo na akamuowa binti mfalme. Kwakuwa mfalme hakuwa na mtoto wa kiume basi alopofariki Khalidi akapewa ufalme na akawa anaongoza nchi.

 

Miaka 15 sasa imepita toka aonane na Jalidi. Siku moja aliiona tena sura ya Jalidi ikiwa getini kuja kuomba msaada kwani maisha yamemuwia magumu. Jalidi alishangazwa kumuona Khalidi kuwa ndiye mfalme wao. Bila ya kinyongo Khalidi akamaidia Halidi n kumpati a vyakula na nguo kwa wingi sana na kumpatia na usafiri wa kubebea mizigo kwenda na yayo kijiji ni.

 

Kijana alipomaliza kusimulia hadithi hii akmwambia jini “nii ndio ilivyokuwa kati ya wagomvi wawili hawa, hivyo nakuomba unifanyie huruma kama Khalidi alivyomuhurumia Jalidi pindi alipomtumbukiza shimoni. Lile jini likasema “kwa hakika khabari hii inasikitisha lakini haiewzi kulinganisha hasira nilizo nazo . kwa hakika binti niliyemuuwa nilitoka nae mabli sana. Basi pale pale jini likapiga mguu chini na upepo mkali ukanibeba. Niliachwa kuleleni cha mlima uliopo pembenu ya ufukwe. Jini lile likanambia “nitakuonea huruma, sitakuuwa lakini nitakigeuza nyani” basi akanimwagia maji yamoto na palepale nikaanza kutowa magoya na kuota mkia. Kucha na hatimaye nikawa nyani kamili.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Mankaa image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Simulizi za Hadithi Main: Burudani File: Download PDF Views 251

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Simulizi za Hadithi EP 6 Part 3: Mlevi asimuliwa hadithi

Muendelezo wa simulizi za HALIF LELA U LELA kitabu cha pili....

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 3 Part 6: Simulizi ya samaki wa rangi nne

Simulizi za HALIF LELA U LELA zipo nyingi na zinasisimua.. kisa hiki cha samaku wa rangi nne kipo katika kitabu cha kwanza

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 10: Ndoa ya binti mfalme na Sinbad

Hadithi za HALIF LELA U LELA kitabu cha kwanza muendelezo......

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 7 Part 1: Aladini na taa ya mshumaa wa ajabu

Hii ni simulizi iliyopo ndani ya kitabu cha pili cha hadithi za HALIF LELA U LELA......

Soma Zaidi...
Simulizi za Hadithi EP 5 Part 13: Sehemu ya sita ya safari ya Sinbad

Muendelezo wa safari ya Sinbad iliyopo ndani ya kitabu cha kwanza cha hadithi za HALIF LELA U LELA...

Soma Zaidi...