image

Kutokana nyani mpaka kuwa chongo

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

KUTOKA NYANI MPAKA KUWA CHONGO.

Katika hali ya unyani nikajiambia “kama nikiishi msituni kwa hakika italiwa na chui bora niende kwa binadamu huenda nikapata muokoaji”. mwazo yangu yakawahivyo nikashuka pale na kuelekea ufukweni. Nikakuta kunajahazi linakaribia kuondoka. Basi niktafuta mti na kuutumia kama mtumbwi na kielekea kwenye jahazi.

 

Watu walishangaa sana kuona nyani anaweza kutumia nyenzo kuweza kuvuka. Wakaanza kukusanyika ili kuona akina ya nyani walioendelea kiasi hiki. Walikuwepo wengine wananipigia makofi na wengine wakawa wananicheka na wengine wananozonea. Mimi sikujali mpaka nikakamata jahazi na kukaa pembeni. Walikuwepo watu walotaka kunirudisha majini na wengune hata wakadiriki kunipiga mawae. Kwa bahati njewa nahodha wa jahazi akawakataza ni kuahidi kunilinda kwa maajabu niloonesha.

 

Haukupita muda ghafla jahazi letu likavamiwa na kundi kubwa la watu walooneka na ni waheshimiwa wenye madaraka ya juu serikalini. Mkubwa wao akajitambulisha “sisi ni watu wa baraza la mtukufu muheshimiwa mfalme. Karani muandishi wa mfalme amefariki mwezi ulopita hivyo tunatafuta mtu mwenye muandiko mzuri ili achukuwe nafasi” basi wakagawa makaratasi kwa kila mtu aandike chochote kwenye karatsi.

 

Basi walipomaliza na mimi nikaashiria nipewe karatasi ya kuandika. Basi nahodha akanipatia karatasi na kaamu na nikakaa mkao wa 4 na kushika kalamu vizuri kisomi. Watu wote walishangaa sana kuona nyani mwenye ujuzi wa hali yajuu hii. Basi niliandika mashairi machache ya kumsifu mfalme na kumjazia sifa kemkem. Kisha nikawapatia karatasi. Kwa hakika walishangaa sana kuona nyani ana ujusi wa namna hii.

 

Basi walichukuwa makaratasi yao na kuondoka, huko mfalme aliziangalia karatasi na kuupenda mwandiko wangu. Palepale aliamuru uletwe usafiri uje kunibeba. Nilibebwa kiheshimiwa zaidi na kuekwa mbele ya mfalme. Nilitowa heshima kinyaninyani na mfalme akaelewa. Alimipa karatasi niandike nikaandika tena mashairi ya kumpamba zaidi ya yale ya mwanzo. Kwakweli alistaajabu na kufurahi pia. Mfalme alikuwa anapenda sana kucheza bao. Hivyo aliashiria liletwe bao.

 

Basi nikacheza mechi na mfalme. Kwa mara ya kwanza nilimfunga nikaona amekasirika. Hivyo nikamwachia kanifunga goli tatu na kulipisha zote. Mwisho mfalme akaamrisha kiletwe chakula asi kikaletwa na sikula kinyaninyani nilinawa mikono na kula kwa kutumia mikono yangu. Yote nilokuwa nikiyafanya yalikuwa yakimstaajabisha mfalme na watu wa baraza lake.

 

Ilipofika jioni mfalme akaagiza aletwe binti yake wa kipekee ili astaajabu uwepo wa nyani mbele ya macho ya mfalme. Kama zilivyo tamaduni za waislamu mtoto wa kike hujifunika mwili wake ila kwa ndugu zake wa karibu na wazazi wake. Kwakuwa aliitwa na baba yake alukuja kawaida hat bila ya kujifunika. Ila maratu alipoingia kwa baba yake alihaza na kurudi nyuma na kwenye kujifunika kisha akarudi. Mfalme alishangaa kilichomsibu hata mwamnae akarudi.

 

Binti akaeleza “baba unaniita mbele ya mwanaume mwingine nikiwa sijajifunika” pale mfalme alishangaa na kumwambia “nipo mimi tu hapa na huyu nyani, ametoka wapi huyo mwanaume mwingie?”. akajibu “baba huyo sionyani ni mtu na amegeuzwa kuwa nyani kiuchawi. Ni aina za uchawi wanaotumia majini” basi mimi kusikia maneno yale nilitingisha kichwa kuashiria kukubaliana na maneno ya binti. Mafalme akamwambia “umeyajuwa vipi haya mwanangu?” binti akajibu “yule bib I aliyekuwa akinilea alinifundisha aina nyingi za uchawi na kuopoa”.

 

Basi mfalme akamtaka binti yake aniopoe na binti akakubali. Siku ilofata asubuhi sisi watatu tulielekea kwenye jumba bovu lililohamwa zamani am,bapo binti amelelewa na huyo bibi. Binti akatuambua mimi na mfalme kukaa pale na tusiondoke kwa loote lile litalotokea. Hivyo binti akaanza kuzungumza maneno yasiyojulukana. Ghafla akatokea nge na binti akageuka kenge akawa anamkimbiza nge amle. Yule nge akageuka tandu na binti akageuka nyoka.

 

Basi ikawa hivyo kila mmoja akigeuka flani mwinzie anageuka kitu kingine. Hali ilikuwa hivyo mpaka yule nge akageuka kunguru basi binti akageuka kipanga wakapaa wakikimbizaa na tusiwaone walipokwenda. Tulikaa pale kwa muda mrefu na tusiwaone. Ghafla tukaona punda aliyefundia kitu anakuja na akatema punje za komamanga. Kisha akageuka kuwa kuku mtembe na uanza kula punje za komamanga. Alizila zote alizoziona akawa anaashiria kama kuna ingine.

 

Kumbe kulikuwa na punje moja imebaki iliyokuwa ikibingiria kulekea kwenye mfereji wa maji. Aliiwahi aikamate lakini akachelewa na ikaangukia kwenye maji, na palepale ikageuka kuwa samaki. Binti akageuka kuwa samaki mkubwa zaidi na wakakimbizana mpaka yule samamki akageuka kuwa dragon na kuanza kumwaga moto. Binti akageuka kuwa dragoni na kutukinga sisi na motoule. Kwa bahati mbaya moto uke ulumchoma binti kwenye miyo na chehe ikajanipata kwenye jicho na kulipasua na hiyo ikawa ndio sababu ya chongo yangu ya jicho la kulia.

 

Baada ya mapamabno makali binti alifanikiwa kulichoma jini lile na kuliuwa. Alianguka chini na kuanza kuhe,a kwa uchovu. Alipopata nguvu akachukuwa majivu ya lieldragoni la kijini na kuchanganya na maji. Akatamka maneno na kunumwagia na palepale nikageuka kuwa mtu kamili. Furaha ilitanda kwa mfalme ila ghafla binti aliikata furaha hii kwa kumwambia “baba nimefanikiwa kumuuwa jini na kumtibu kijana, ila na mimi umri wangu umebakia siku tatau tu. Ule moto uliniunguza kweye moyo”.

 

Siku tatu binti alifariki dunia na majonzi yalienea kwa mfalme kwani alikuwa na mtoto mmoja tu. Baa da ya situ saba mfalme aliniita na kunambia “upo huru kwa sasa maana sio nyani tena. Nimefanikiwa kukuokoa lakini nimepoteza maisha ya binti yangu. Hivyo siwezi kukuangalia. Ninakuomba uondoke nchini hapa na usirudi tena, kwani uwepo wako utaendelea kunikumbusha binti yangu.

 

Basi nikaamua kuondoka nchini pale na nisijuwe pa kwenda. Nikaeekea baghdadi na nikanyoa kichwa cahngu na nyusi zangu. Nilipofika hapa nikakutana na wenzangu hawa na hatukupata kujuwa hadithi ya kila mmoja kati yetu. Hivyo hii ndio hadithi yangu. Zubeidah akamfuata waziri na kumwambia ataje stori yake yeye na wenzie basi akaeleza kuwa wao ni wafanya biashara wameomba hifadha pale baada ya kuingiliwa na usiku.

 

Basi mpaka wanamaliza kusimulia hadithi zao ilikuwa ni majogoo hivyo Zubeydah akwaaruhusu watu wote watoke mule ndani. Bila hata kuomba waruhusiwe kukaa mule mpaka asubuhi walitoka mbiombio. Mfalme aliyejifanya mfanya biashara akamwambia waziri “wachukuwe chongo hawa watatu na ukalale nao nyubani kwako na ifikapo asubuhi niitie wale wanawake watatu wote waje kwenye baraza letu nao wataje hadithi zao. Inaonekana kuna makubwa yamewafika.

 

 

Basi mambo yakawa kama alivyotaka mfalme, kesho asubuhi wale wadada wakaletwa mbele ya mfalme na mfale akawaambia “hatukuwaita kwa kuwaadhibu kwa mlichotufanyia jana ila tunataka mtueleze na nyinyi haithi zenu hata mkayafanya yale mlikuwa mkiyafanya. Zubeydah aliposikia sauti ile akajua niwale watu wa jana kumbe ni mfalme na watu wake. Basi akapiga magoti na wenzake wakafata na akaanza kuomba msamaha “tusamehe ewe mtukufu mfalme, kwa hakika hatukujuwa kuwa ni wewe mfalme, tumekukosea sana hata tukaweza panga kwenye shingo yako” mfalme akamjibu “nimekwisha samehe tafadhali aeni bila wasi na mueleze hadithi zenu.

 

Mfalme akawa anawashawishi kwa maneno mazuri na kuwaambia “nioneni kama mpo na rafiki zenu hapa na kuwa huru kusema chochote kile”. basi mabinti wakaanza kuangaliana wakitafakari ni nani aanze kusimulia hadithi yake. Kabla hawajaanza na wale machongo watatu wakaletwa ili wapate kusikiliza hadithi za wadada hawa. Basi wakaanza kusimulia hadithi zao kama ifuatavyo;-





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1297


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Hadithi ya mji uliogeuzwa mawe
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

HADITHI ZA ALIF LELA U LELA: HADITHI YA WANAWAKE WATATU NA CHONGO WATATU
Soma Zaidi...

Ndoto ya mgonjwa, binti mfalme
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Hadithi ya binti wa pili mwimba mashairi mwenye makovu
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Kuelekea bonde la uokozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

Hadithi ya mke na kasuku
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Alif lela u lela: utangulizi
Katika nchi za China, Hindi, Uarabuni na Uajemi alikuwepo mfalme aliyefahamika na kuheshimika sana kwa uhodari wake na utawala wake mzuru. Soma Zaidi...

HADITHI YA BINTI MWENYE KUFICHWA MTOTO WA MFALME
Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA BINTI MWENYEKUFICHWA, MTOTO WA MFALME. Soma Zaidi...

Kisiwa cha uokozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

Alif lela u lela 1
Alif lela u lela ni hadithi zilizosheheni utamu na machungu pamoja na visa vya wachawi na majinim soma sasa. Soma Zaidi...

Hadithi ya tabibu wa mfalme
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

Hadithi ya mzee wa pili na mbwa wawili weusi
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...