picha

nina maambukizi ya zinaha maumivu wakati wa kukojoa na usaha

Mimi nilifanya ngono isiyo salama Tar 14/07 mwaka huu, nilikutana tu na mwanamke ambae sikuwa hata na background yake yoyote hivyo baada ya siku tatu nilijikuta nina maambukizi ya zinaha (maumivu wakati wa kukojoa na usaha), hivyo nilienda hospital na kup

nina maambukizi ya zinaha maumivu wakati wa kukojoa na usaha

Mimi nilifanya ngono isiyo salama Tar 14/07 mwaka huu, nilikutana tu na mwanamke ambae sikuwa hata na background yake yoyote hivyo baada ya siku tatu nilijikuta nina maambukizi ya zinaha (maumivu wakati wa kukojoa na usaha), hivyo nilienda hospital na kupatiwa matibabu...



Namba ya swali 050

Baada ya kuanza dawa kwa muda kama wa wiki moja nilianza kupata maumivu ya kifua na kurudi hoapitali siku ya 12 baada ya tendo, nilipimwa vipimo vyote ikiwepo HIV na sikukutwa na chochote mpaka kufika siku ya 18 nikapata mafua ambayo yameambatana na homa kali na sijakutwa pia na malaria baada ya kwenda hospital, pia nina mamivu ya tumbo hasa sehemu ya chini na kitovu na kifua sehemu za manyonyo



Namba ya swali 050

Kwa muda huo wote toka pale nimekuwa natumia dawa tofauti za kifua, gesi tumboni, na mafua lakini mwili kwa sasa una maumivu makali mgongo, mikono na tumbo.



Namba ya swali 050

HIV haiwezi kuonekana kabla ya miezi mitatu



Namba ya swali 050

Dalili zake huanza kuja baada ya muda gani? Mheshimiwa pia kuhusu hizi changamoto zinaweza kuwa dalili za HIV? Leo ni siku ya 22 baada ya kitendo



Namba ya swali 050

Dalili zake zinanzia wiki ya kwanza mpaka miezi mitatu kisha zinapotea kabisa.



Namba ya swali 050

Dalili zake ni pamoja na mfua na homa Dokta?



Namba ya swali 050

Yes hizo ni dalili, ila zinawwza kuanbatana na mashambukizi mengi. Hivyo uhakika ni kupima baada ya miezi 3. Vipi ulipatabkuvimba mitoki, kwebye mapaja, shingo ama kwapa?



Namba ya swali 050

Hapana hiyo sijapata
mitoki ndio matezi?



Namba ya swali 050

Yes mitoki ni tezi



Namba ya swali 050

Zenyewe zinakuwaje, au ni uvimbe unatokea?



Namba ya swali 050

Hizi huwa ni katika viashiria vya mwanzoni sana, hata na huwapata watu wengi, sana



Namba ya swali 050

Hiyo sijawahi kupata kabisa, na mbaya zaidi nina hofu ambayo naona mpaka kufikia miezi mitatu itakuwa i,enipeleka pabaya zaidi, kwahiyo kwa kipindi cha miezi mitatu hii homa hazitakwisha?



Namba ya swali 050

HIV haipo hivyo kaka, yenyewe ipo siri sana. Inavijidaliki vichache sana, ambavyo sio rahisi kuviona kabisa. Homa kali, iloambatana na maumivu ya kifua, na mafua, huenda ni sababu nyingine kabisa. Ok, ulisema ulitokwa na usaha, bipo ulipopima walikueleza unanshida gani?



Namba ya swali 050

Walisema tu kwamba ni shida ya magonjwa ya zinaa ila sikuambiwa ni nini hasa hiyvo nilipatiwa dawa ambazo baada ya kutumia nimekuwa sawa kabisa na nilirudi kwaajili ya vipimo siku tatu baadae baada ya kumaliza dozi na sikukutwa na zile homa tena.



Namba ya swali 050

Yes huwenda ilokuwa ni kisonono.



Namba ya swali 050

Sawa dokta, naomba niwe naendelea kukujulisha hali yangu, lakini pia nipo Dar es Salaam kama naweza kuja kuonana kwa ushauri zaidi?



Namba ya swali 050

Ok



Namba ya swali 050

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1646

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Fahamu Ugonjwa unaosababisha madhara kwenye mapafu

Posti hii inaelezea kuhusiana na Magonjwa yanayosababisha madhara kwenye mapafu na kitaalamu hujulikana Ugonjwa wa Acute Respiratory Distress Syndrome (ARDS) hutokea wakati Majimaji yanapojaa kwenye vifuko vidogo vya hewa nyororo (alveoli) kwenye mapafu

Soma Zaidi...
Jifunze kuhusu ugonjwa wa bawasiri na dalili zake

Katika somo hili utakwenda kujifunz akuhusu ugonjwa wa Bawasiri na dalili zake. Pia utajifunza njia za kujilinda nao.

Soma Zaidi...
Dalili za homa ya ini

Kaika post hii utakwenda kujifunz akuhusu dalili za homa ya ini. Dalili hizi sio lazima zitokee zote. Zinaweza zikatokea baadhi tu na ikatosha kuonjesha kuw auna homa ya ini.

Soma Zaidi...
Je vidonda Mara nyingi vitakuwa maeneo gan ya mwili?

Je vidonda Mara nyingi vitakuwa maeneo gan ya mwili? Hili ni swali lililoulizwa kuhusu vidonda vya tumbo, kuwa vinakaa wapi katika mwili.

Soma Zaidi...
Yajue magonjwa nyemelezi.

Posti hii inahusu zaidi magonjwa nyemelezi ambayo kwa kawaida utokea pale ambapo kinga ya mwili inashuka.

Soma Zaidi...
maumivu makali sana juu ya tumbo yn kama kuna moto hivi na mgongon kama unadungwa sindano hivi je hizo ni dalili za vidonda vya tumbo?

Dr huwa nasikia maumivu makali sana juu ya tumbo yn kama kuna moto hivi na mgongon kama unadungwa sindano hivi je hizo ni dalili za vidonda vya tumbo?

Soma Zaidi...
Magonjwa ya kuambukiza

Magonjwa ya kuambukiza: Ni yale yanayoweza kuambukizwa kutoka kwa mtu mmoja hadi kwa mwingine au kutoka kwa wanyama kwenda kwa mtu Mlipuko tukio lililoenea la ugonjwa katika jamii kwa wakati fulani ambao huonekana kama kesi mpya kwa kiwango ambacho kinazi

Soma Zaidi...
Watu walio hatarini kupata UTI

Somo hili linakwenda kukuletea orodha ya makunfi ya watu walio hatarini kupata UTI

Soma Zaidi...
Naomb niulize ukiingiliana na mwanmke mweny ukimwi unaweza kuambikizwa na kusaambaaa kwa mda gan ndan ya mwil

Muda gani ukimwi huweza kuonekana mwilini ama kugundulika kama umeathirika, ni dalili zipo hujitokeza punde tu utakapoathirika

Soma Zaidi...