picha

nina maambukizi ya zinaha maumivu wakati wa kukojoa na usaha

Mimi nilifanya ngono isiyo salama Tar 14/07 mwaka huu, nilikutana tu na mwanamke ambae sikuwa hata na background yake yoyote hivyo baada ya siku tatu nilijikuta nina maambukizi ya zinaha (maumivu wakati wa kukojoa na usaha), hivyo nilienda hospital na kup

nina maambukizi ya zinaha maumivu wakati wa kukojoa na usaha

Mimi nilifanya ngono isiyo salama Tar 14/07 mwaka huu, nilikutana tu na mwanamke ambae sikuwa hata na background yake yoyote hivyo baada ya siku tatu nilijikuta nina maambukizi ya zinaha (maumivu wakati wa kukojoa na usaha), hivyo nilienda hospital na kupatiwa matibabu...



Namba ya swali 050

Baada ya kuanza dawa kwa muda kama wa wiki moja nilianza kupata maumivu ya kifua na kurudi hoapitali siku ya 12 baada ya tendo, nilipimwa vipimo vyote ikiwepo HIV na sikukutwa na chochote mpaka kufika siku ya 18 nikapata mafua ambayo yameambatana na homa kali na sijakutwa pia na malaria baada ya kwenda hospital, pia nina mamivu ya tumbo hasa sehemu ya chini na kitovu na kifua sehemu za manyonyo



Namba ya swali 050

Kwa muda huo wote toka pale nimekuwa natumia dawa tofauti za kifua, gesi tumboni, na mafua lakini mwili kwa sasa una maumivu makali mgongo, mikono na tumbo.



Namba ya swali 050

HIV haiwezi kuonekana kabla ya miezi mitatu



Namba ya swali 050

Dalili zake huanza kuja baada ya muda gani? Mheshimiwa pia kuhusu hizi changamoto zinaweza kuwa dalili za HIV? Leo ni siku ya 22 baada ya kitendo



Namba ya swali 050

Dalili zake zinanzia wiki ya kwanza mpaka miezi mitatu kisha zinapotea kabisa.



Namba ya swali 050

Dalili zake ni pamoja na mfua na homa Dokta?



Namba ya swali 050

Yes hizo ni dalili, ila zinawwza kuanbatana na mashambukizi mengi. Hivyo uhakika ni kupima baada ya miezi 3. Vipi ulipatabkuvimba mitoki, kwebye mapaja, shingo ama kwapa?



Namba ya swali 050

Hapana hiyo sijapata
mitoki ndio matezi?



Namba ya swali 050

Yes mitoki ni tezi



Namba ya swali 050

Zenyewe zinakuwaje, au ni uvimbe unatokea?



Namba ya swali 050

Hizi huwa ni katika viashiria vya mwanzoni sana, hata na huwapata watu wengi, sana



Namba ya swali 050

Hiyo sijawahi kupata kabisa, na mbaya zaidi nina hofu ambayo naona mpaka kufikia miezi mitatu itakuwa i,enipeleka pabaya zaidi, kwahiyo kwa kipindi cha miezi mitatu hii homa hazitakwisha?



Namba ya swali 050

HIV haipo hivyo kaka, yenyewe ipo siri sana. Inavijidaliki vichache sana, ambavyo sio rahisi kuviona kabisa. Homa kali, iloambatana na maumivu ya kifua, na mafua, huenda ni sababu nyingine kabisa. Ok, ulisema ulitokwa na usaha, bipo ulipopima walikueleza unanshida gani?



Namba ya swali 050

Walisema tu kwamba ni shida ya magonjwa ya zinaa ila sikuambiwa ni nini hasa hiyvo nilipatiwa dawa ambazo baada ya kutumia nimekuwa sawa kabisa na nilirudi kwaajili ya vipimo siku tatu baadae baada ya kumaliza dozi na sikukutwa na zile homa tena.



Namba ya swali 050

Yes huwenda ilokuwa ni kisonono.



Namba ya swali 050

Sawa dokta, naomba niwe naendelea kukujulisha hali yangu, lakini pia nipo Dar es Salaam kama naweza kuja kuonana kwa ushauri zaidi?



Namba ya swali 050

Ok



Namba ya swali 050

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2217

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Dalili na ishara za Ugonjwa wa kuambukiza.

Magonjwa ya kuambukiza ni maradhi yanayosababishwa na vijidudu kama vile bakteria, virusi, fangasi au vimelea. Viumbe vingi vinaishi ndani na kwenye miili yetu. Kwa kawaida hazina madhara au hata kusaidia, lakini chini ya hali fulani, baadhi ya viumbe

Soma Zaidi...
Maambukizi ya ngozi (Cellulitis): Dalili na tiba ya hospitalini.

Ufafanuzi: Ugonjwa wa dharura wa maambukizi ya bakteria kwenye tabaka za ndani za ngozi.Maeneo Yanayoathiriwa Zaidi: Mara nyingi hutokea kwenye miguu, ingawa unaweza kuathiri sehemu yoyote ya mwili ikiwemo uso na mikono.Dalili Kuu: Ngozi kuwa nyekundu, kuvimba, kuhisi joto kali, maumivu makali, na kutoa malengelenge au michirizi myekundu.Tiba ya Hospitalini: Matumizi ya viuavijasumu (antibiotics) vya kumeza au vya kuwekewa kwenye mishipa ya damu (Intravenous) kulingana na ukali wa maambukizi.Matatizo: Isipotibiwa, inaweza kusababisha maambukizi kwenye damu (sepsis), uharibifu wa tishu (necrotizing fasciitis), au maambukizi kwenye mifupa (osteomyelitis).

Soma Zaidi...
Visababishi vya ugonjwa wa Varicose vein

Posti hii inahusu zaidi visababishi mbalimbali vya ugonjwa wa vericose veini, ni visababishi mbalimbali ambavyo utokea kwenye mtindo wa maisha kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Watu walio hatarini kupata UTI

Somo hili linakwenda kukuletea orodha ya makunfi ya watu walio hatarini kupata UTI

Soma Zaidi...
Dalili za Mafua kwa Watoto Wachanga

Mafua kwa watoto wachanga ni hali ya kawaida, lakini inaweza kuwa na changamoto kwa sababu watoto hawa bado hawana kinga imara. Post hii inatoa mwongozo wa kutambua dalili za mapema na hatua za kuchukua ili kumsaidia mtoto wako apate nafuu.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kisukari

Ugonjwa wa kisukari hurejelea kundi la magonjwa yanayoathiri jinsi mwili wako unavyotumia sukari kwenye damu (glucose). Glucose ni muhimu kwa afya yako kwa sababu ni chanzo muhimu cha nishati kwa seli zinazounda misuli na tishu zako. Pia ndio chanzo ki

Soma Zaidi...