KUTOKA KWENYE KISIMA MPAKA KUWA MFALME

KUTOKA KWENYE KISIMA MPAKA KUWA MFALME

Download kitabu Hiki Bofya hapa KUTOKA KWENYE KISIMA MPAKA KUWA MFALME.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

KUTOKA KWENYE KISIMA MPAKA KUWA MFALME

pic
Download kitabu Hiki Bofya hapa

KUTOKA KWENYE KISIMA MPAKA KUWA MFALME.

Pale kisimani khalidi aliokolewa na majini waliokuwa wakiishi pale kwa muda wa miaka mingi iliyopita. Hata kabla ya kufika chini walimzi,isha na kumbebe na kumtua kidogokidogo na hakupatwa na madhara. Majini hawa walimpenda Khalidi kwa tabia zake njema na ukarimu uliopambwa na uchamungu wake. Hivyo hawakupenda damu ya mtu mkarimu iumwagike mule kisimani walipokuwa wakiishi.

Basi alipokuwa kati ya kupoteza fahamu na kurudi fahamu yaani akiwa kwenye mang’amung’amu akawasikia majini wakizungumza. “unajuwa mtoto wa mfalme wa nchi hii anaumwa sana na inapata miezi sita sasa bila ya kupona” wengine wakawa wanajibu “mimi sijapata kusikia hilo kabisa” kukatokea mmoja akasema “mimi nafahamu dawa ya ugonjwa wake” basi pale yule aliye anzisha mada akamuuliza “ni ipi dawa yake?” akamjibu “nyumbani kwa Khalidi kuna paka mwenye rangi nne na adimu sana paka hawa. Magoya saba ya mkia wa paka huyu ukiyachoma na ubani na harufu ikimpata vilivyo huyo mtoto wa mfalme kwa hakika atapona.

Wale majini hawakujuwa kama Khalidi amewasikia. Basi baa da ya muda wakamtoa pale ndani ya kisima. Khalidi alipitiwa na usingizi na aliposhituka akajikuta kitandani kwake. Alipoamka asubuhi akachukuwa magoya saba ya mkia wa ule paka akisubii kuona kama aliuwa anaota au ilikuwani kweli. Siku ile ilienda salama sana na hakukuwa na tatizo lolote, na huku Jalidi akaamini amemuuwa Khalidi,

Siku ilofata akaona ugeni unaingia kwake ni mfalme na msafra wake wakija kwakwe ili amuombee dua binti yake aliyekuwa anaumwa kwa miezi sita hata bila ya kupoona. Hapo khalidi akajuwa kumbe haikuwa ndoto ila ni ukweli. Pale akamchukuwa mgonjwa yule na akachukuwa udi na kachanganya na mgoya yale na akaomba dua. Hata kabla ya kumaliza alisikia kishindo. Mgonjwa alianguka chini na kupoteza fahamu.

Watu wakaanza kumpepea na mflme alijuwa lamda binti yake amepatwa na jambo. Baada ya masaa kadha akazinduka na hakuhisi maumivu yeyote. Hii inamaanisha alipona kabisa ugonjwa wake. Basi mfalme kwa furaha akamwambia “kijana kwa furaha nilizo nazo sina kikubwa cha kukulipa lakini naomba umuoe binti yangu” Khalidi alikubaliana na mawazo hayo na akamuowa binti mfalme. Kwakuwa mfalme hakuwa na mtoto wa kiume basi alopofariki Khalidi akapewa ufalme na akawa anaongoza nchi.

Miaka 15 sasa imepita toka aonane na Jalidi. Siku moja aliiona tena sura ya Jalidi ikiwa getini kuja kuomba msaada kwani maisha yamemuwia magumu. Jalidi alishangazwa kumuona Khalidi kuwa ndiye mfalme wao. Bila ya kinyongo Khalidi akamaidia Halidi n kumpati a vyakula na nguo kwa wingi sana na kumpatia na usafiri wa kubebea mizigo kwenda na yayo kijiji ni.

Kijana alipomaliza kusimulia hadithi hii akmwambia jini “nii ndio ilivyokuwa kati ya wagomvi wawili hawa, hivyo nakuomba unifanyie huruma kama Khalidi alivyomuhurumia Jalidi pindi alipomtumbukiza shimoni. Lile jini likasema “kwa hakika khabari hii inasikitisha lakini haiewzi kulinganisha hasira nilizo nazo . kwa hakika binti niliyemuuwa nilitoka nae mabli sana. Basi pale pale jini likapiga mguu chini na upepo mkali ukanibeba. Niliachwa kuleleni cha mlima uliopo pembenu ya ufukwe. Jini lile likanambia “nitakuonea huruma, sitakuuwa lakini nitakigeuza nyani” basi akanimwagia maji yamoto na palepale nikaanza kutowa magoya na kuota mkia. Kucha na hatimaye nikawa nyani kamili.


                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Aliflela1 Main: Burudani File: Download PDF Views 721

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

HADITHI YA MWEN YEKUTABIRIWA MTOTO WA TAJIRI
HADITHI YA MWEN YEKUTABIRIWA MTOTO WA TAJIRI

Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITI YA MWENYE KUTABIRIWA MTOTO WA TAJIRI Kwanza tambua ewe ndugu yangu kuwa mimi ni mtoto wa tajiri mkubwa sana katika nchi yetu hii.

Soma Zaidi...
Safari saba za sinbad
Safari saba za sinbad

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za safari saba za Sinbad

Soma Zaidi...
KUTOKA NYANI MPAKA KUWA CHONGO
KUTOKA NYANI MPAKA KUWA CHONGO

Download kitabu Hiki Bofya hapa KUTOKA NYANI MPAKA KUWA CHONGO.

Soma Zaidi...
KIAPO CHA SULTANI
KIAPO CHA SULTANI

Download kitabu Hiki Bofya hapa KIAPO CHA SULTANI.

Soma Zaidi...
HADITHI YA SAMAKI WA RANGI NNE
HADITHI YA SAMAKI WA RANGI NNE

Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA SAMAKI WA RANGI NNE.

Soma Zaidi...
Hadithi ya mke na kasuku
Hadithi ya mke na kasuku

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...
Hadithi ya kinyozi msiri wa mfalme
Hadithi ya kinyozi msiri wa mfalme

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...
Hadithi ya Khalid mwenye kuneemeshwa na Jalid
Hadithi ya Khalid mwenye kuneemeshwa na Jalid

Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...
HADITHI YA CHONGO WA TATU MTOTO WA MFALME
HADITHI YA CHONGO WA TATU MTOTO WA MFALME

Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA CHONGO WA TATU MTOTO WA MFALME Mimi ni mtoto wa mfalme kama nilivyotangulia kusema na ni mtoto wa kipekee kwa baba na mama.

Soma Zaidi...