Je AI itauwa ubunifu, ama kudhoofisha taaluma?

Je AI itauwa ubunifu, ama kudhoofisha taaluma?

Tupo katika kipindi ambacho, tafiti nyingi zinahitajika kuhusu athari za AI kwenye ubunifu na taaluma.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Wakati kalkuleta za kidijitali zilipoanza kutumika, baadhi ya watu walihofia kuwa hazitahitajika tena akili za wanahisabati. Wengine walihisi kuwa wataalamu wa hesabu watapoteza nafasi zao. Lakini leo tunajua kuwa calculator haikumaliza taaluma ya hesabu – badala yake, ilirahisisha kazi na kuongeza ubora wa uchambuzi wa kihisabati.

 

Mfano mmoja ni sekta ya uhandisi: licha ya uwepo wa kalkuleta na kompyuta, bado wahandisi hujifunza hisabati kwa kina – kwa sababu vifaa hivyo ni vya kusaidia, si vya kuchukua nafasi ya maarifa.

 

Sasa tupo kwenye zama za AI. Programu kama Copilot, ChatGPT, na zana nyingine zinaweza kusaidia kuandika msimbo (code). Kwa mujibu wa Microsoft, zaidi ya 30% ya msimbo wa programu unaandikwa na AI kwa sasa. Hii imesababisha baadhi ya wanafunzi na watengenezaji kuamini kuwa hawahitaji tena kujifunza lugha za programu – kwamba AI itawafanyia kila kitu.

 

Lakini ukweli ni kwamba, kama ilivyokuwa kwa calculator, AI ni nyenzo ya kusaidia, si mbadala wa maarifa ya msingi. Mtu asiyefahamu programming hawezi kutumia AI kwa ufanisi mkubwa. AI itakupa misingi, lakini ubunifu, mantiki ya kutatua tatizo, na maadili ya programu bado vinahitaji akili ya binadamu.

 

Kwa hiyo, badala ya kuogopa AI, tujifunze kuitumia vizuri. Na zaidi ya hapo, tuendelee kujifunza misingi ya taaluma zetu – kwa sababu teknolojia ni msaidizi, si mbadala wa ujuzi halisi.

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:45 Topic: more Main: ICT File: Download PDF Views 133

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Tofauti ya Developer na Programmer
Tofauti ya Developer na Programmer

Katika post hii utakwenda kujifunza kuhusu tofauti ya programmer na developer

Soma Zaidi...
Nini maan ya Trojan kwenye tehama
Nini maan ya Trojan kwenye tehama

Trojan ni Moja ya maneno tunayoyasikia sana kwneye tehama. Leo nitakupa maana yake

Soma Zaidi...
Vipi matoleo ya softawe (version) yanaandikwa
Vipi matoleo ya softawe (version) yanaandikwa

Katika somo hili utajifunza utaratibu unaotumiwa kuweka matoleo kwnye software.

Soma Zaidi...
Kwa Nini blog nyingi hazina sehemu ya comment
Kwa Nini blog nyingi hazina sehemu ya comment

Zani ilikuwa sehemu ya ku comment ni muhimu sana kwenye blog, ila Sasa sehemu hii imeondolewa kwenye blog nyingi. Ni Kwa nini hasa imeondolewa. Post hii itakujibu swali hilo

Soma Zaidi...
Rafiki wa kweli kwa programmer
Rafiki wa kweli kwa programmer

Ninutani lakini Kuna mafunzo, programmer wote hawatamsahau rafiki huyu

Soma Zaidi...
Firewall ni nini kwenye tehama
Firewall ni nini kwenye tehama

Katika post hii utakwenda kujifunza maana ya neno firewall

Soma Zaidi...
Kwa Nini lugha nyingi za kompyuta zimeanzia Marekani
Kwa Nini lugha nyingi za kompyuta zimeanzia Marekani

Post hii utakwenda kujikitabzaidi kujibu swali, hata hivyo itambulike kuwa wengi wa wanasayansi waliohusika kwenye lugha hizi sio wamarekani.

Soma Zaidi...