Je AI itauwa ubunifu, ama kudhoofisha taaluma?

Tupo katika kipindi ambacho, tafiti nyingi zinahitajika kuhusu athari za AI kwenye ubunifu na taaluma.

Wakati kalkuleta za kidijitali zilipoanza kutumika, baadhi ya watu walihofia kuwa hazitahitajika tena akili za wanahisabati. Wengine walihisi kuwa wataalamu wa hesabu watapoteza nafasi zao. Lakini leo tunajua kuwa calculator haikumaliza taaluma ya hesabu – badala yake, ilirahisisha kazi na kuongeza ubora wa uchambuzi wa kihisabati.

 

Mfano mmoja ni sekta ya uhandisi: licha ya uwepo wa kalkuleta na kompyuta, bado wahandisi hujifunza hisabati kwa kina – kwa sababu vifaa hivyo ni vya kusaidia, si vya kuchukua nafasi ya maarifa.

 

Sasa tupo kwenye zama za AI. Programu kama Copilot, ChatGPT, na zana nyingine zinaweza kusaidia kuandika msimbo (code). Kwa mujibu wa Microsoft, zaidi ya 30% ya msimbo wa programu unaandikwa na AI kwa sasa. Hii imesababisha baadhi ya wanafunzi na watengenezaji kuamini kuwa hawahitaji tena kujifunza lugha za programu – kwamba AI itawafanyia kila kitu.

 

Lakini ukweli ni kwamba, kama ilivyokuwa kwa calculator, AI ni nyenzo ya kusaidia, si mbadala wa maarifa ya msingi. Mtu asiyefahamu programming hawezi kutumia AI kwa ufanisi mkubwa. AI itakupa misingi, lakini ubunifu, mantiki ya kutatua tatizo, na maadili ya programu bado vinahitaji akili ya binadamu.

 

Kwa hiyo, badala ya kuogopa AI, tujifunze kuitumia vizuri. Na zaidi ya hapo, tuendelee kujifunza misingi ya taaluma zetu – kwa sababu teknolojia ni msaidizi, si mbadala wa ujuzi halisi.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:45 Topic: more Main: ICT File: Download PDF Views 248

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Utowauti wa HDD (Hard Disk Drive) na SSD (Solid State Drive)

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu HDD (Hard Disk Drive) na SSD (Solid State Drive)

Soma Zaidi...
Worm katika kompyuta ni nini?

Katika kompyuta, worm ni aina ya programu hasidi (malware) inayojinakili yenyewe na kusambaa kupitia mitandao bila kuhitaji kushikamana na faili au programu nyingine. Tofauti na virusi, worm husambaa haraka zaidi na mara nyingi hutumia mtandao kuenea.

Soma Zaidi...
Virusi ni nini kwenye kompyuta?

Virusi vya kompyuta ni programu hasidi (malware) inayojishikiza kwenye faili au programu halali na kujiendesha pale faili hiyo inapofunguliwa. Virusi vinaweza kuharibu data, kupunguza kasi ya kompyuta, au kusababisha upotevu wa taarifa.

Soma Zaidi...
Rafiki wa kweli kwa programmer

Ninutani lakini Kuna mafunzo, programmer wote hawatamsahau rafiki huyu

Soma Zaidi...
Server ni nini?

Server ni kompyuta au mfumo unaotoa huduma au rasilimali kwa kompyuta na vifaa vingine kupitia mtandao. Zinaweza kutoa huduma kama kuhifadhi data, kuendesha tovuti, kusambaza faili, au kushughulikia barua pepe.

Soma Zaidi...
Tofauti ya RAM na ROM

RAM (Random Access Memory) na ROM (Read-Only Memory) ni aina za kumbukumbu kwenye kompyuta au vifaa vya kielektroniki, lakini zina malengo na tabia tofauti.

Soma Zaidi...
Firewall ni nini kwenye tehama

Katika post hii utakwenda kujifunza maana ya neno firewall

Soma Zaidi...
Tofauti ya Developer na Programmer

Katika post hii utakwenda kujifunza kuhusu tofauti ya programmer na developer

Soma Zaidi...
Nini maan ya Trojan kwenye tehama

Trojan ni Moja ya maneno tunayoyasikia sana kwneye tehama. Leo nitakupa maana yake

Soma Zaidi...
Kwa Nini lugha nyingi za kompyuta zimeanzia Marekani

Post hii utakwenda kujikitabzaidi kujibu swali, hata hivyo itambulike kuwa wengi wa wanasayansi waliohusika kwenye lugha hizi sio wamarekani.

Soma Zaidi...