picha

Je AI itauwa ubunifu, ama kudhoofisha taaluma?

Tupo katika kipindi ambacho, tafiti nyingi zinahitajika kuhusu athari za AI kwenye ubunifu na taaluma.

Wakati kalkuleta za kidijitali zilipoanza kutumika, baadhi ya watu walihofia kuwa hazitahitajika tena akili za wanahisabati. Wengine walihisi kuwa wataalamu wa hesabu watapoteza nafasi zao. Lakini leo tunajua kuwa calculator haikumaliza taaluma ya hesabu – badala yake, ilirahisisha kazi na kuongeza ubora wa uchambuzi wa kihisabati.

 

Mfano mmoja ni sekta ya uhandisi: licha ya uwepo wa kalkuleta na kompyuta, bado wahandisi hujifunza hisabati kwa kina – kwa sababu vifaa hivyo ni vya kusaidia, si vya kuchukua nafasi ya maarifa.

 

Sasa tupo kwenye zama za AI. Programu kama Copilot, ChatGPT, na zana nyingine zinaweza kusaidia kuandika msimbo (code). Kwa mujibu wa Microsoft, zaidi ya 30% ya msimbo wa programu unaandikwa na AI kwa sasa. Hii imesababisha baadhi ya wanafunzi na watengenezaji kuamini kuwa hawahitaji tena kujifunza lugha za programu – kwamba AI itawafanyia kila kitu.

 

Lakini ukweli ni kwamba, kama ilivyokuwa kwa calculator, AI ni nyenzo ya kusaidia, si mbadala wa maarifa ya msingi. Mtu asiyefahamu programming hawezi kutumia AI kwa ufanisi mkubwa. AI itakupa misingi, lakini ubunifu, mantiki ya kutatua tatizo, na maadili ya programu bado vinahitaji akili ya binadamu.

 

Kwa hiyo, badala ya kuogopa AI, tujifunze kuitumia vizuri. Na zaidi ya hapo, tuendelee kujifunza misingi ya taaluma zetu – kwa sababu teknolojia ni msaidizi, si mbadala wa ujuzi halisi.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:45 Topic: more Main: ICT File: Download PDF Views 520

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Dua za Mitume na Manabii   

Post zinazofanana:

Namna ya kujilinda dhidi ya kudukuliwa kwa simu yako

Leo tutajifunza sababu zinazoifanya simu kuwa rahisi kudukuliwa na hatua madhubuti za kuzuia udukuzi. Tutazungumza kuhusu matumizi salama ya intaneti, usimamizi wa apps, usalama wa akaunti, pamoja na tabia muhimu za kujikinga.

Soma Zaidi...
Nini kinaweza kusababisha simu yako kudukuliwa

Hapa tunajadili sababu kuu zinazoifanya simu iwe rahisi kudukuliwa, mbinu zinazotumiwa na wadukuzi, na mambo ya kawaida ambayo watumiaji hufanya bila kujua na kujipeleka kwenye hatari.

Soma Zaidi...
Tofauti ya Developer na Programmer

Katika post hii utakwenda kujifunza kuhusu tofauti ya programmer na developer

Soma Zaidi...
Tofauti kati ya Blogger na WordPress

Blogger na WordPress ni majukwaa maarufu ya kuunda blogu na tovuti. Blogger ni huduma ya bure inayomilikiwa na Google, rahisi kutumia lakini ina mipaka katika uhariri na udhibiti. WordPress ni jukwaa lenye uhuru mkubwa wa kubinafsisha tovuti, lenye toleo la bure (WordPress.com) na la kujitegemea (WordPress.org).

Soma Zaidi...
Tofauti ya RAM na ROM

RAM (Random Access Memory) na ROM (Read-Only Memory) ni aina za kumbukumbu kwenye kompyuta au vifaa vya kielektroniki, lakini zina malengo na tabia tofauti.

Soma Zaidi...
Ukurasa wa AMP kwenye SEO

Katika somo hili tutaeleza maana ya AMP (Accelerated Mobile Pages), jinsi inavyofanya kazi, faida zake katika SEO, changamoto zake, na njia bora za kuitumia ili kuboresha utendaji wa tovuti yako kwenye injini za utafutaji kama Google.

Soma Zaidi...
Server ni nini?

Server ni kompyuta au mfumo unaotoa huduma au rasilimali kwa kompyuta na vifaa vingine kupitia mtandao. Zinaweza kutoa huduma kama kuhifadhi data, kuendesha tovuti, kusambaza faili, au kushughulikia barua pepe.

Soma Zaidi...
Utowauti wa HDD (Hard Disk Drive) na SSD (Solid State Drive)

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu HDD (Hard Disk Drive) na SSD (Solid State Drive)

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuzuia kudukuliwa kwa akaunti yako ya Facebook

Thibitisha akaunti yako kwa hatua za usalama kama kutumia nenosiri imara, kuweka uthibitisho wa hatua mbili (2FA) kwa kutumia authenticator, kukagua matumizi ya vifaa vilivyoingia (logged in devices), kuondoa apps zisizo za lazima, na kuzuia ulaghai (phishing). Hatua hizi zinaongeza sana ulinzi na kupunguza hatari ya kudukuliwa.

Soma Zaidi...
Rafiki wa kweli kwa programmer

Ninutani lakini Kuna mafunzo, programmer wote hawatamsahau rafiki huyu

Soma Zaidi...