Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 27: Kushuka tena kwa Wahyi

Baada ya kukatika kwa Wahyi kwa muda wa masiku kadhaa hatimaye Jibril akaleta tena wahyi kwa mara nyingine.

GABRIELI ALETEA UFUNUO WA ALLAH TENA:

Ibn Hajar alisema: "Kusimama kwa ufunuo (wahyi) wa Allah kwa siku chache kulikuwa ni ili kumtuliza Mtume wa Allah (Rehema na amani zimshukie) kutokana na hofu aliyokuwa nayo na pia kumfanya atamani sana kuupokea ufunuo. Wakati hali ya mkanganyiko ilipoondoka, alama za ukweli zilionekana, na Mtume wa Allah (Rehema na amani zimshukie) alijua kwa hakika kwamba alikuwa amekuwa Mtume wa Mola Mkuu. Alikuwa na uhakika pia kwamba kile kilichomjia kilikuwa si kingine bali ni mjumbe n wahyi kutka kwa ALLh. Kutamani kwake kuupokea ufunuo huo kulikuwa sababu nzuri ya uimara wake na utulivu wake wakati wa kupokea ufunuo wa Allah."

 

Al-Bukhari ameripoti kutoka kwa Jabir bin ‘Abdullah kuwa alimsikia Mtume wa Allah (Rehema na amani zimshukie) akizungumza kuhusu kipindi cha kusimama kwa ufunuo kama ifuatavyo:

“Wakati nilipokuwa natembea, nilisikia sauti kutoka angani. Nilipoinua macho yangu, kwa hakika alikuwa ni yule malaika yuleyule aliyenitembelea katika pango la Hira’. Alikuwa ameketi kwenye kiti kati ya ardhi na mbingu. Niliogopa sana na nikapiga magoti chini. Nilirudi nyumbani nikisema: ‘Nifunikeni…, nifunikeni…’. Allah aliniteremshia aya:

 

‘Ewe uliyejifunika (kwa nguo)! Inuka ukahadharishe! Na Mola wako Mtukuze! Na nguo zako zitakase! Na uepukane na uchafu (sanamu)!’” [74:1-5]

Baada ya hapo, ufunuo ukaanza kuja kwa nguvu, mara kwa mara na kwa mpangilio.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Historia ya Mtume Muhammad (s.a.w) Main: Dini File: Download PDF Views 634

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 53: Kuslimu kwa Hamza bin Abdul-Muttalib

Hapa utajifunza historia ya kuslimu kwa Hamzah bin Abdul-Muttalib.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 70: Kuhama kwa Mtume Muhammad s.a.w kuelekea Madina

Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu safari ya Mtume Muhammad s.a.w kuelekea Madina. Utajifunza changamoto za safari alizokutana nazo.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 9: Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu tukio la Kupasuliwa kwa Kifua Mtume Wakati Akiwa Mtoto

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 52: Maamuzi ya kumuuwa Mtume Muhammad

Baada ya mbinu nyingi za Maquraish kufeli sasa wanaamuwa bora tu wamuuwe Muhammad ili kukomesha kuendelea mafundishio bya dini mpya.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 29: Amri za kwanza alizopewa Mtume Muhammad ﷺ

Katika somo hili utajifunza amri ambazo alipewa Mtume Muhammad ﷺ mwanzoni kabisa mwa kazi yake ya Kulingania dini

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 15: Historia ya Abdallah baba wa Mtuume Muhammad

Katika somo hili utakwenda kujifunza historia fupi ya Abadallah baba wa Mtume Muhammad ﷺ

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 10: Kufa kwa mama yake Mtume ﷺ

Katika somo hili utakwenda kujifunz akuhusu habari ya kifo cha Bi Amina ambaye ni mama yake Mtume MUhammad ﷺ

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 42: Historia fupi ya Al-Naḍr ibn al-Ḥārith ibn ʿAlqama Adui wa Mtume Muhammad ﷺ

Katika somo hili utakwenda kujifunza historia ya Adui wa Mtume Muhammad ﷺ mwanzoni mwa kuenea kwa Uislamu Makkah.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 33: Mquraishi wanagunduwa kuhusu dini Mpya

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu namna ambavyo wito wa ulingano ulipoenea na kuwafikia maquraish na washirikina

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 26: Kusimama kwa Wahy

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu kusimama kwa Wahyi kuja kwa Mtume Muhammad ﷺ

Soma Zaidi...