Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 27: Kushuka tena kwa Wahyi
Baada ya kukatika kwa Wahyi kwa muda wa masiku kadhaa hatimaye Jibril akaleta tena wahyi kwa mara nyingine.
GABRIELI ALETEA UFUNUO WA ALLAH TENA:
Ibn Hajar alisema: "Kusimama kwa ufunuo (wahyi) wa Allah kwa siku chache kulikuwa ni ili kumtuliza Mtume wa Allah (Rehema na amani zimshukie) kutokana na hofu aliyokuwa nayo na pia kumfanya atamani sana kuupokea ufunuo. Wakati hali ya mkanganyiko ilipoondoka, alama za ukweli zilionekana, na Mtume wa Allah (Rehema na amani zimshukie) alijua kwa hakika kwamba alikuwa amekuwa Mtume wa Mola Mkuu. Alikuwa na uhakika pia kwamba kile kilichomjia kilikuwa si kingine bali ni mjumbe n wahyi kutka kwa ALLh. Kutamani kwake kuupokea ufunuo huo kulikuwa sababu nzuri ya uimara wake na utulivu wake wakati wa kupokea ufunuo wa Allah."
Al-Bukhari ameripoti kutoka kwa Jabir bin ‘Abdullah kuwa alimsikia Mtume wa Allah (Rehema na amani zimshukie) akizungumza kuhusu kipindi cha kusimama kwa ufunuo kama ifuatavyo:
“Wakati nilipokuwa natembea, nilisikia sauti kutoka angani. Nilipoinua macho yangu, kwa hakika alikuwa ni yule malaika yuleyule aliyenitembelea katika pango la Hira’. Alikuwa ameketi kwenye kiti kati ya ardhi na mbingu. Niliogopa sana na nikapiga magoti chini. Nilirudi nyumbani nikisema: ‘Nifunikeni…, nifunikeni…’. Allah aliniteremshia aya:
‘Ewe uliyejifunika (kwa nguo)! Inuka ukahadharishe! Na Mola wako Mtukuze! Na nguo zako zitakase! Na uepukane na uchafu (sanamu)!’” [74:1-5]
Baada ya hapo, ufunuo ukaanza kuja kwa nguvu, mara kwa mara na kwa mpangilio.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 web hosting 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 55: Mazungumzo ya Utbah bin Rabi'a na Mtume Muhammad (SAW)
Baada ya Quraish kufeli mbinu zao za mateso, sasa wanaanza mbinu za diplomasi, wanajaribu kumshawishi Mtume kwa kumpa mali nauongozi
Soma Zaidi...Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 61: Matukie mengineyo kwneye safari ya Taif
Baadhi ya matukio mengine yaliyoteokea kweye safari hii ya Tfai
Soma Zaidi...Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 25 Jibril analeta Wahyi kwa Mtume Muhammad ﷺ
Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu historia ya Mwanzoni mwa Wahyi aliouleta Jibril kwa Mtume Muhammad ﷺ
Soma Zaidi...Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 14: Historia ya Amina mama wa Mtume Muhammad
Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu historia ya Amina mama wa Mtume Muhammad ﷺ
Soma Zaidi...Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 39: Baraza la ushauri kuwazuia mahujaji kumfuata Muhammad ﷺ
Katika somo hili utakwenda ujifunza kuhusu uwamuzi wa Baraza la ushauri kuwazuia mahujaji kumfuata Muhammad ﷺ wakati wa msimu wa hija.
Soma Zaidi...Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 60: Kulingania Uislamu nje ya Makkah
Mwaka wa 10 toka kupata utume, Mtume Muhammad (S.A.W) anaanza kulingania dini nje ya Mji wa Makkah
Soma Zaidi...