Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 27: Kushuka tena kwa Wahyi
Baada ya kukatika kwa Wahyi kwa muda wa masiku kadhaa hatimaye Jibril akaleta tena wahyi kwa mara nyingine.
GABRIELI ALETEA UFUNUO WA ALLAH TENA:
Ibn Hajar alisema: "Kusimama kwa ufunuo (wahyi) wa Allah kwa siku chache kulikuwa ni ili kumtuliza Mtume wa Allah (Rehema na amani zimshukie) kutokana na hofu aliyokuwa nayo na pia kumfanya atamani sana kuupokea ufunuo. Wakati hali ya mkanganyiko ilipoondoka, alama za ukweli zilionekana, na Mtume wa Allah (Rehema na amani zimshukie) alijua kwa hakika kwamba alikuwa amekuwa Mtume wa Mola Mkuu. Alikuwa na uhakika pia kwamba kile kilichomjia kilikuwa si kingine bali ni mjumbe n wahyi kutka kwa ALLh. Kutamani kwake kuupokea ufunuo huo kulikuwa sababu nzuri ya uimara wake na utulivu wake wakati wa kupokea ufunuo wa Allah."
Al-Bukhari ameripoti kutoka kwa Jabir bin ‘Abdullah kuwa alimsikia Mtume wa Allah (Rehema na amani zimshukie) akizungumza kuhusu kipindi cha kusimama kwa ufunuo kama ifuatavyo:
“Wakati nilipokuwa natembea, nilisikia sauti kutoka angani. Nilipoinua macho yangu, kwa hakika alikuwa ni yule malaika yuleyule aliyenitembelea katika pango la Hira’. Alikuwa ameketi kwenye kiti kati ya ardhi na mbingu. Niliogopa sana na nikapiga magoti chini. Nilirudi nyumbani nikisema: ‘Nifunikeni…, nifunikeni…’. Allah aliniteremshia aya:
‘Ewe uliyejifunika (kwa nguo)! Inuka ukahadharishe! Na Mola wako Mtukuze! Na nguo zako zitakase! Na uepukane na uchafu (sanamu)!’” [74:1-5]
Baada ya hapo, ufunuo ukaanza kuja kwa nguvu, mara kwa mara na kwa mpangilio.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 web hosting 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 56: Abu Talib Awaunganisha Bani Hashim na Bani Al-Muttalib kwa Ulinzi wa Mtume (SAW)
Wana wa Abd Manaf wanaungana kumlinda Mtume Muhammad isipokuwa Abu Lahab yeye amekataa kuungana na ndugu zake.
Soma Zaidi...Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 64: Ndoa ya Mtume Muhammad baada ya Khadija
Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu Ndoa Mtume Muhammad baada ya Bi Khadija alimuoa Sauda kisha Aisha
Soma Zaidi...Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 49: Hila za Maquraish Dhidi ya Wahamiaji
Baada ya Waislamu kuhama Maquraish hawakupendezwa na jambo hilo, hivyo wakaanza kufanya hila ili Warejeshwe kutoka walipohamia
Soma Zaidi...Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 48: Hijra ya kwanza kuelekea Ethiopia
Katika somo hiliutajifunza kuhusu Hijra ya Kwanz ana ya Pili kuelekea Ethiopia na mambo yaliyojitokeza.
Soma Zaidi...Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 66: Mkataba wa Aqaba wa kwanza
Katika somo hili utajifunza kuhusu historia ya Mkataba wa Aqaba wa kwanza
Soma Zaidi...Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 18: Historia ya vita vya Fijar
Hapa utajifunza chanzo vya vita vya al fijar na vipi Mtume Muhammad ﷺ alishiriki katika vita hivyo.
Soma Zaidi...