picha

Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 27: Kushuka tena kwa Wahyi

Baada ya kukatika kwa Wahyi kwa muda wa masiku kadhaa hatimaye Jibril akaleta tena wahyi kwa mara nyingine.

GABRIELI ALETEA UFUNUO WA ALLAH TENA:

Ibn Hajar alisema: "Kusimama kwa ufunuo (wahyi) wa Allah kwa siku chache kulikuwa ni ili kumtuliza Mtume wa Allah (Rehema na amani zimshukie) kutokana na hofu aliyokuwa nayo na pia kumfanya atamani sana kuupokea ufunuo. Wakati hali ya mkanganyiko ilipoondoka, alama za ukweli zilionekana, na Mtume wa Allah (Rehema na amani zimshukie) alijua kwa hakika kwamba alikuwa amekuwa Mtume wa Mola Mkuu. Alikuwa na uhakika pia kwamba kile kilichomjia kilikuwa si kingine bali ni mjumbe n wahyi kutka kwa ALLh. Kutamani kwake kuupokea ufunuo huo kulikuwa sababu nzuri ya uimara wake na utulivu wake wakati wa kupokea ufunuo wa Allah."

 

Al-Bukhari ameripoti kutoka kwa Jabir bin ‘Abdullah kuwa alimsikia Mtume wa Allah (Rehema na amani zimshukie) akizungumza kuhusu kipindi cha kusimama kwa ufunuo kama ifuatavyo:

“Wakati nilipokuwa natembea, nilisikia sauti kutoka angani. Nilipoinua macho yangu, kwa hakika alikuwa ni yule malaika yuleyule aliyenitembelea katika pango la Hira’. Alikuwa ameketi kwenye kiti kati ya ardhi na mbingu. Niliogopa sana na nikapiga magoti chini. Nilirudi nyumbani nikisema: ‘Nifunikeni…, nifunikeni…’. Allah aliniteremshia aya:

 

‘Ewe uliyejifunika (kwa nguo)! Inuka ukahadharishe! Na Mola wako Mtukuze! Na nguo zako zitakase! Na uepukane na uchafu (sanamu)!’” [74:1-5]

Baada ya hapo, ufunuo ukaanza kuja kwa nguvu, mara kwa mara na kwa mpangilio.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-08-17 14:06:48 Topic: Historia ya Mtume Muhammad (s.a.w) Main: Masomo File: Download PDF Views 1436

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 web hosting     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 33: Mquraishi wanagunduwa kuhusu dini Mpya

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu namna ambavyo wito wa ulingano ulipoenea na kuwafikia maquraish na washirikina

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 4: Historia ya kuangamizwa kwa jeshi la Tembo

Katika soo hili utakwenda kujifunza historia ya jeshi la tembo na jinsi lilivyoangamizwa. Pia utajifunza namna ambavyo watu wa Makkah waliweza kujilinda.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 57: Mkataba wa udhalimu

Baada ya Baini Abd Manaf kukubaliana kumlinda Mtume Muhammad basi Maquraish wakaweka mkataba wa udhalimu utakaozuia kutoshirikiana na banu abd Manaf kwa lolote lile.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 54: Kusilimu kwa Umar bin Al- Khattab

Hii ni historia fupi ya kuslimu kwa Umar na kuanza kwa taswira mpya ya waislamu na uislamu katika mji wa makkah

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 26: Kusimama kwa Wahy

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu kusimama kwa Wahyi kuja kwa Mtume Muhammad ﷺ

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 69: Kikao cha kumuuwa Mtume Muhammad s.a.w kinakaliwa

Katika somo hili utajifunza mambo yaliojiri katika kikao kilicho andaliwa kwa ajili ya kumuuwa Mtue Muhammad s.a.w. Katika kikao hiki mpaka Iblis alihudhuria

Soma Zaidi...