Deni la Penzi

DENI LA MAPENZI Badisiku ambayo niliamua niuze vitu vya ndani kwangu ili nilipe madeni ya watu, ndipo yule binti akatokea tena.

Deni la Penzi

DENI LA MAPENZI
Badisiku ambayo niliamua niuze vitu vya ndani kwangu ili nilipe madeni ya watu, ndipo yule binti akatokea tena. Ilikuwa kama bahati vile akanikabidhi pesa ndefu nikalipa madeni na haikubakia hata kidogo. Siku hiyo alikaa karibu nami na kuanza kuzungumza hapa na pale. Nilimuomba niione sura yake kwa ukaribu zaidi, alimuita mjakazi wake mmoja na kumwambia akae karibu naye, kisha akafunua kitambaa kilichoziba uso wake.



Nilipata kujiridhisha baada ya kukutana na nyusi ndefu zilizolala vyema, zilizo nyeusi sana, silizonyooka kama mwezi mwandamo. Macho ya duara yaliyo meupe. Nywele nyembamba, zilizoshuka kukaribia masikio. Hakuwa mweupe sana kama mwarabu wa Sham. Sikupata kujuwa nini amepaka kwenye midomo yake, maana alikuwa anameremeta. Sikutaka zaidi kumuangalia, niliamini itakuwa ni makosa. Kwakuwa nilikuwa naangalia uso, iliniridhisha kukubali uwepo wake.



Hatimaye nikatamk maneno kumweleza, kama kuna dawa umenipa. Mwenzio zilali kutwa kucha kukuwaza. Siwachi kufukiri sura yako machoni mwangu. Nakiri kwa ulimi wangu, penzi lako nahitaji. Nilijikuta nabwabwanya maneno yasiyo mpangilio, yasiyo na vina vya mashairi, wala weledi wa mazungumzo. Niliamini kubwabwanya kwangu kutakuwa kumeelewaka japo kidogo. Hakuweza kunijibu kitu chochote, ila alinieleza kuwa atanijibu kwa barua. Lakini aliniomba kuwa nimkopee tena bidhaa kama za siku ile.



Hata sikuwahi kufikiri, nikaingia kwenye maduka ya wenzangu na kumchukulia bidhaa zake. Kwa haraka akawaagiza vijakazi wake, wakafunga mzigo na kupotelea mtaani. Baada tu ya kuondoka nikaanza kujiuliza, hivi inamaana utajiri wote alionao yule binti ndo anashindwa kuwa na pesa ya kununulia bidhaa hizi?, ama hii ni mbinu ya matajiri kunyonya wanyonge. Sikuweza kuwaza sana maana kila nikikumbuka sura yake, na kimna ambavyo moyo wangu kwake, hata deni pia nalisahau.



Sasa nikawa na mambo mawili ya kusubiria, kwanza barua na pili ni pesa ya watu. Sikumoja mapema asubuhi nikapokea barua kutoka kwa mtu asiyejulikana. Barua iliandikwa kwa maandishi meusi, kutokana na wino wa ngisi uliochanganywa na manukato. Imeandikwa kwenye karatasi nzuri. Kwa shauku nilikata kamba na kufungua barua ile. Maneno machache yaliandikwa:



Salam, kipenzi, natumai upo salama. Nashukuru kwa nguo ulionichagulia siku ile imenitosha sawa. Ujumbe wa barua hii utaletewa ifikapo jioni, na pesa yako pia. Basi ilipofika jioni akaja moja kati ya wale wajakazi wake. Akanipatia pesa yangu kisha akaanza kusimulia:-



“.….. toka alipoondoka hapa siku ile hakuweza kulala kwa kukuwaza wewe. Anakupenda na amenituma nije nikwambie hivyo. Kama upo tayari anakutaka wende ukaonekane kwao.” kwani anaitwa nani na kwao ni wapi? Huu ni mzigo wa maswali nilio mjibu. Anaitwa Shaniat bint ‘Aziz mkwe wa sultani Harun Rashid. Mmh sasa nitafikaje kwao?” nilimuulliza. “…. kuna mtihani umepewa na mke wa mfalme, uende kwa siri, ukifanikiwa atafanya taratibu zote za harusi yetu badala ya kuridhishwa nawe atakapo kuona, na kama ukifeli ukakamatwa, basi utapoteza maisha” haya ndiyo maneno aliyonijibu.



Sikujuwa ni kwa nini ameamuwa kunipa mtihani huu. Lakini nilijuwa kuwa kama nisipoweza kumuona ka masiku mengi zaidi huwenda nikawa kichaa ama punguani. Niliamini ni bora nijaribu kwenda kwa siri nikifa nife kiume, kuliko kubakia hapa na kujiwazia naishia kukumbatia ukuta. Nikamjibu kuwa nimekubali. Basi akanielekeza kuwa kesho mida ya jioni niende kwenye bostani lililopo karibu na ikulu na hapo nitakutana nae.



Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Aliflela2 Main: Burudani File: Download PDF Views 774

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Viatu vya ajabu

VIATU VYA AJABU VYAONDOKA NA MKONO WANGU Aliponieleza sifa za viatu anavyotaka nikamsogelea kwa ukaribu na kumkazia macho kama nataka kumpiga vile kisha nikamuuliza “wewe ni nani, na ni nani amekutuma, vina nini hasa viatu hivi” alibakia kimya ...

Soma Zaidi...
Hadithi ya Kaka wa pili wa kinyozi

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani

Soma Zaidi...
Ndoa ya Siri yafanyika

Posti hii inakwenda kukuendelezea hadithi kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultan

Soma Zaidi...
Ujumbe wa Siri kwenye kitabu cha ajabu

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu

Soma Zaidi...
Hadithi ya kinyozi yeye mwenyew

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani

Soma Zaidi...
KIFO CHA MTOA BURUDANI WA MFALME

Hapo zamani katika mi wa Baghadani wakati wa utawala wa Sultani Harun Rashid alikuwepo kijana mmoja aliyekuwa karibu sana na Sultani kwa kuwa alikuwa akimpa burudani.

Soma Zaidi...
Jaribio la pili la aladini

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu

Soma Zaidi...