HADITHI YA NURDINI 05: Rafiki wa Kweli

Mungu ashukuriwe sana, hatimaye miezi kadhaa ikapita bila ya waziri Masoud kugundua siri nzito.

HADITHI YA NURDINI 05: Rafiki wa Kweli

RAFIKI WA KWELI




Mungu ashukuriwe sana, hatimaye miezi kadhaa ikapita bila ya waziri Masoud kugundua siri nzito. Mfalme aliendelea kumkumbusha waziri Faridi hatimaye akasahau kabisa lile swala. Miezi saba ikapita. Maradhi ya ajabu yakampata waziri faridi na akafariki dunia. Baada ya taratibu za mazishi kukamilika haikupita hata miezi mitatu mama Nurdini akafariki dunia. Loo !!!!! yalikuwa ni maonzi juu ya majonzi kwa Nurdini ambaye siku zote alitegemea baba na mama. Kwa kweli kizuri hata hakidumu kwa muda mrefu. Ukweli ni kuwa mzee Faridi aliishi mika mingi na kula chumvi nyingi. Alifariki akiwa na miaka 81. je kizuri hakidumu kweli?



Nurdini sasa akiwa yaima, akawa ndiye mrithi wa pekee wa mali za baba. Hakuweza kuwafahamu ndugu za baba yake hatammoja. Maisha yaliendelea, aliendelea kula mali za baba bila kuzalisha. Aliendelea kufurahi na mkewe kipenzi. Marafiki zake waliendelea kula na kusaza. Waliendelea kutanua na mengineyo kibao. Kama ilivyo mali bila daftari huisha bila habari, hatimaye mali ya Nurdini ikaendelea kupungua kwa kasi sana. Kweli bandubandu hualiza gogo. Baada ya miezi kadhaa pesa zilimuishia. Nurdini akaanza kuuza Watumwa wote apate pesa ya kutumi,.



Mambo hayakumnyookea, marafiki wakakata mguu kabisa kuonana naye. Akaanza kuuza vitu vya ndani hata vikamwishia na kubakiwa na kitanda na vitu vichavche kwa ajili ya kupikia. Mwishowe akaamuwa kwenda kumuuza mewe ambaye alikuwaga ni mtumwa hapo mwanzo. Hii ni kutokana na ushauri wa mkewe kumuonea huruma mumewe hivyo akamwambia amuuze apate pesa, huwenda akazalisha pesa ya kumkomboa na wakakutana mbele ya safari. Nurdini alimpenda sana mkewe lakin aliamini kuwa ushauri huu ni mzuri.



Alimchukuwa mkewe na kwenda kumuuza kwa pesa ile ambayo baba yake alimnunulia. Waziri Masoud alimuona Nurdini akimuuza mtumwa ambaye anafanana sifa na yule aliyekuwa akitafutwa na baba ake. Hapo aliamini kuwa baba yake alimpatia mwanaye mtumwa wa mfalme. Masoud aliweka oda ya kumnunua yule mtumwa, lakini Nurdini alipotambuwa hili akagoma kumuuza maana aliamini kwa ukorofi wa Masoud asingeweza kumpatia pesa. Ikabakia ugomvi kati ya Masoud na Nurdini. Nurdini wakati huo akamchukuwa mkewe na kumtia kwenye farasi tayari kuondoka mbio.



Masoud alitaka kutumia uwaziri wake lakini alishindwa, kwani Nurdini alikuwa ni mjeuri. Masoud akamvuta shati Nurdini na akaanguka chini yeye na mkewe, tena kwenye matope. Nurdini alimpiga ngumi waziri, ngumi iliyomtoa damu. Kisha akatimua mbio. Waziri bila ya kujifuta damu akaenda kwa mfalme kushitaki. Hiko akaeleza wazi kila ambacho kilitokea kwa yule mtumwa aliyemtaka kuwa bwana faridi alimuozesha mwanaye na sasa mtoto anataka kumuuza.



Mfalme alikasirika sana, na akatangaza aletewe Nurdini popote alipo. Jeshi kubwa liliamuriwa likamchukuwe Nurdini. Katika jeshi lile alikuwepo kijana mmoja aliyekuwa na ukaribu sana na baba Nurdini, hivyo akaenda mbio kwa Nurdini na kumtaarifu akimbie haraka sana. Nurdini hakuamini anachoambiwa ila akakubali kuamini, hivyo akajiandaa kuondoka yeye na mkewe. Yule askari akampatia nurdini kiasi cha pesa alicho nacho na kuwafanyia mipango ya kupata jahazi dogo la kuondokea kwasiri. Mambo haya yalifanyika kwa siri sana na haikuchukuwa muda Nurdini akaondoka, na mkewe kuelekea Baghadad.



Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 141

Post zifazofanana:-

Nahtaji kujua dalili za Mama mjamzto kujifungua
Soma Zaidi...

Vita vya Uhud na sababu ya kutokea kwake, Mafunzo ya Vita Vya Uhud
Vita vya Uhudi. Soma Zaidi...

Mafungu ya mirathi katika uislamu
Mafungu ya urithi yaliyotajwa katika haya sita yafutayo:1. Soma Zaidi...

Zijuwe Suna zinazofungamana na swaumu na funga ya ramadhani
Soma Zaidi...

NJIA ZA KUKABILIANA NA MRESHA YA KUSHUKA
1. Soma Zaidi...

ijuwe namna ya kufanya ihram na Vazi la ihram
Soma Zaidi...

Kwa nini vidole vimekatwa
HADITHI YA ALIYEKATWA VIDOLE GUMBA Mimi nilikuwa mfanyabiashara mdogo sana, katika mji wa Baghdad. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Shu'ayb(a.s).
Kutokana na kisa cha Nabii Shu'ayb(a. Soma Zaidi...

BONGOCLASS STAFF MEMBERS
RAJABU ATHUMAN BA. Soma Zaidi...

Mama mjamzito anapo hisi uchungu je mtoto huendelea kucheza tumboni?
Swali langi ni hiliMama mjamzito anapo hisi uchungu je mtoto huendelea kucheza tumboni? Soma Zaidi...

RAJABU ATHUMAN MAHEDE,(MAARUFU KAMA MWALIMU RAJABU ATHUMANI MAHEDE, AU OSTADHI RAJABU ATHUMANI MAHEDE)
Soma Zaidi...

Kuangamizwa kwa Watu wa Lut(a.s) watu wa Sodoma na Gomora
Watu wa Lut(a. Soma Zaidi...