Naulizia nyenzo alizotumia nabii Ada (A.S) kusimamisha ukhalifa

Baada ya Nuhu(a.s) Mtume aliyemfuatia ni Nabii Hud(a.s). Hud(a.s) alitumwa na Mola wake kuwalingania kabila (taifa) la ‘Ad. Kabila la ‘Ad lilikuwa likijulikana kama ‘Ad-al-ram au ‘Ad-Ula. ‘Ad walikuwa wakiishi kusini ya Bara

Swali: 

Naulizia nyenzo alizotumia nabii Ada (A.S) kusimamisha ukhalifa

 

Jibu

Mbinu za Hud(a.s) Katika Kufikisha Ujumbe

 

Katika kulingania Uislamu kwa watu wake, Hud(a.s) alitumia mbinu zifuatazo:


 

Kwanza alijieleza kwa uwazi na kuwanasihi watu wake:

“Akasema: Enyi kaumu yangu! Mimi sio mpumbavu. Lakini mimi ni Mtume niliyetoka kwa Mola wa walimwengu. Nakufikishieni ujumbe wa Mola wangu. Na mimi kwenu ni (mtu) nasihi muaminifu.(7:67-68)


 


Mnaona ajabu kukufikieni mawaidha yanayotoka kwa Mola wenu kwa (ulimi wa) mtu aliye mmoja katika nyinyi ili akuonyeni? (Muabuduni Mwenyezi Mungu) na mkumbuke alivyokufanyeni Khalifa baada ya watu wa Nuhu.Na akakuzidisheni sana katika umbo. Basi zikumbukeni neema za Mwenyezi Mungu ili mpate kufaulu.” (7:69)


 

Pili aliwapa hoja kwanini wanalazimika kumuamini Allah na kumuabudu ipasavyo.


 


Mcheni yule ambaye amekupeni haya mnayoyajua.” “Amekupeni (chungu ya) wanyama na watoto wanaume.” “Na mabustani na chemchem, (mito).” (26:132-134)


 

Tatu, aliwabashiria kupata malipo mema hapa hapa ulimwe nguni endapo watamcha Allah(s.w) ipasavyo:


 

“Enyi watu wangu! Ombeni msamaha kwa Mola wenu (kwa mabaya yenu yaliyopita) kisha mtubie kwake, atakuleteeni mawingu yateremshayo mvua tele, na atakuzidishieni nguvu juu ya nguvu zenu (mlizonazo). Wala msikengeuke kuwa waovu.” (11:52)


 

Nne, aliwahofisha watu wake na adhabu kali ya Allah(s.w)
iwapo watamuasi.


 

“Na kama mtarudi nyuma (hainidhurishi kitu); nimekwisha kukufikishieni niliyotumwa nayo kwenu; na Mola wangu atawafanya makhalifa (wakazi wa mahali hapa) watu wengine wasiokuwa nyinyi; wala nyinyi hamtaweza kumdhuru hata kidogo. Hakika Mola wangu ni Mwenye kuhifadhi kila kitu.” (11:57)


 

“(Wakumbushe) alipowaambia ndugu yao Hud.‘Je, hamtamu ogopa (Mwenyezi Mungu hata nikikutajieni adhabu yot itakayokufikieni kwa mabaya yenu mnayoyafanya)? Bila shaka mimi kwenu ni Mtume muaminifu.” (26:124-125).


 

Tano,aliwafahamisha kwa uwazi watu wake kuwa hakutarajia kupata malipo ya Utume wake kutoa kwao.


 

“Enyi watu wangu! Sikuombeni ujira juu ya haya. Haukuwa ujira wangu ila kwa yule aliyeniumba. Basi hamyatii akilini (haya ninayokuambieni)?” (11:51).


 

“Wala sikutakieni juu yake ujira, ujira wangu haupo ila kwa
Mola wa walimwengu wote.” (26:127)

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Main: Afya File: Download PDF Views 880

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰5 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Get well understood on ACNE skin condition.

DEFINITIONAcne is a skin condition that occurs when your hair follicles become plugged with oil and dead skin cells. Acne usually appears on your face, neck, chest, back and shoulders. Effective treatments are available, but acne can be persistent. The pi

Soma Zaidi...
Sababu zinazosababishwa na bacteria aina ya Salmonella.

 Bakteria aina ya Salmonella huishi ndani ya matumbo ya watu, wanyama na ndege.  Watu wengi wameambukizwa salmonella kwa kula vyakula vilivyochafuliwa na kinyesi. 

Soma Zaidi...
Faida za kula Kitunguu

Kitunguuu thaumu ni muhimu sana katika afya yako, je unazijuwa faida hizo? njoo pamoja nami

Soma Zaidi...
NINI VIDONDA VYA TUMBO?

Ni vidonda vinavyotokea katika ukuta wa tumbo. Vidonda hivi tumezoea kuviita vidonda vya tumbo ila hapa nitataja kitaalamu kuwa vidonda hivi hufahamika kama peptic ulcers.

Soma Zaidi...
Maumivu ya tumbo la chango wakati wa hedhi

Sababu za maumivu ya tumbo la chango wakati wa hedhi, nini ufanye na dalili za maumivu ya tumbo la chango

Soma Zaidi...
Tabia na vyakula vya watu wa kundi AB

Posti hii inahusu zaidi tabia na vyakula wanavyopaswa kutumia watu wenye damu ya kundi AB

Soma Zaidi...
Dawa za utbu Fangasi wa wenye ucha

Maala h nawenda kukufundisha matbabu ya utbu fangas wa wenye ucha.

Soma Zaidi...