picha

Naulizia nyenzo alizotumia nabii Ada (A.S) kusimamisha ukhalifa

Baada ya Nuhu(a.s) Mtume aliyemfuatia ni Nabii Hud(a.s). Hud(a.s) alitumwa na Mola wake kuwalingania kabila (taifa) la ‘Ad. Kabila la ‘Ad lilikuwa likijulikana kama ‘Ad-al-ram au ‘Ad-Ula. ‘Ad walikuwa wakiishi kusini ya Bara

Swali: 

Naulizia nyenzo alizotumia nabii Ada (A.S) kusimamisha ukhalifa

 

Jibu

Mbinu za Hud(a.s) Katika Kufikisha Ujumbe

 

Katika kulingania Uislamu kwa watu wake, Hud(a.s) alitumia mbinu zifuatazo:


 

Kwanza alijieleza kwa uwazi na kuwanasihi watu wake:

“Akasema: Enyi kaumu yangu! Mimi sio mpumbavu. Lakini mimi ni Mtume niliyetoka kwa Mola wa walimwengu. Nakufikishieni ujumbe wa Mola wangu. Na mimi kwenu ni (mtu) nasihi muaminifu.(7:67-68)


 


Mnaona ajabu kukufikieni mawaidha yanayotoka kwa Mola wenu kwa (ulimi wa) mtu aliye mmoja katika nyinyi ili akuonyeni? (Muabuduni Mwenyezi Mungu) na mkumbuke alivyokufanyeni Khalifa baada ya watu wa Nuhu.Na akakuzidisheni sana katika umbo. Basi zikumbukeni neema za Mwenyezi Mungu ili mpate kufaulu.” (7:69)


 

Pili aliwapa hoja kwanini wanalazimika kumuamini Allah na kumuabudu ipasavyo.


 


Mcheni yule ambaye amekupeni haya mnayoyajua.” “Amekupeni (chungu ya) wanyama na watoto wanaume.” “Na mabustani na chemchem, (mito).” (26:132-134)


 

Tatu, aliwabashiria kupata malipo mema hapa hapa ulimwe nguni endapo watamcha Allah(s.w) ipasavyo:


 

“Enyi watu wangu! Ombeni msamaha kwa Mola wenu (kwa mabaya yenu yaliyopita) kisha mtubie kwake, atakuleteeni mawingu yateremshayo mvua tele, na atakuzidishieni nguvu juu ya nguvu zenu (mlizonazo). Wala msikengeuke kuwa waovu.” (11:52)


 

Nne, aliwahofisha watu wake na adhabu kali ya Allah(s.w)
iwapo watamuasi.


 

“Na kama mtarudi nyuma (hainidhurishi kitu); nimekwisha kukufikishieni niliyotumwa nayo kwenu; na Mola wangu atawafanya makhalifa (wakazi wa mahali hapa) watu wengine wasiokuwa nyinyi; wala nyinyi hamtaweza kumdhuru hata kidogo. Hakika Mola wangu ni Mwenye kuhifadhi kila kitu.” (11:57)


 

“(Wakumbushe) alipowaambia ndugu yao Hud.‘Je, hamtamu ogopa (Mwenyezi Mungu hata nikikutajieni adhabu yot itakayokufikieni kwa mabaya yenu mnayoyafanya)? Bila shaka mimi kwenu ni Mtume muaminifu.” (26:124-125).


 

Tano,aliwafahamisha kwa uwazi watu wake kuwa hakutarajia kupata malipo ya Utume wake kutoa kwao.


 

“Enyi watu wangu! Sikuombeni ujira juu ya haya. Haukuwa ujira wangu ila kwa yule aliyeniumba. Basi hamyatii akilini (haya ninayokuambieni)?” (11:51).


 

“Wala sikutakieni juu yake ujira, ujira wangu haupo ila kwa
Mola wa walimwengu wote.” (26:127)

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2021-10-21 Topic: General Main: Afya File: Download PDF Views 937

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 web hosting    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Ugonjwa wa chunusi

Posti hii inaonyesha dalili,sababu na matatizo ya chunusi

Soma Zaidi...
Tabia za watu wenye damu ya group A au kundi A.

Posti hii inahusu zaidi tabia za watu wenye damu la kundi A na vyakula ambavyo wanapaswa kuvitumia, na pengine tutaona baadhi ya vyakula ambavyo havipaswi kutumiwa na watu wenye damu ya kundi A au group A

Soma Zaidi...
JE ?WAJUA WANADAMU WA KWANZA JINSI WALIVYOWEZA KUISHI NA MUNGU ?

Posti hii inajihusisha jinsi gani wanadamu wa kwanza walivyoishi na mwenyezi Mungu apo zamani.tunaona kuwa vitabu vinatuambia vya dini vinatuambia Mungu amemuumba mwanadamu kwa mikono yake mwenyewe.lakini kisayansi tunaona kwamba mwanadamu ametokana na wa

Soma Zaidi...
MADHARA YA KIAFYA YANAYOHUSIANA NA MINYOO: kuliwa kwa tishu, damu, ini na nyama, kuisha damu, kutapika,

MADHARA YA KIAFYA YANAYOHUSIANA NA MINYOO Tofauti na madhara ambayo tumeyaona huko juu kwenye dalili kama maumivu ya kicha, tumbo na miwasho, kichefuchefu na kutapika.

Soma Zaidi...
Madhara ya kutotibu Maambukizi kwenye mifupa

Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu ugonjwa wa Maambukizi kwenye mifupa, kwa hiyo tusipotibu tunaweza kupata madhara yafuatayo.

Soma Zaidi...
Faida za mbegu za papai

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za mbegu za papai na umuhimu wake kiafya

Soma Zaidi...
Sababu zinazopelekea kujamiina kwa uchungu (maumivu)

kijamiana kwa uchungu kitaalamu hujulikana Kama dysarthria ambayo inafafanuliwa kuwa maumivu ya mara kwa mara au ya mara kwa mara katika sehemu ya siri ambayo hutokea kabla tu, wakati au baada ya kujamiiana

Soma Zaidi...
Namna ya kuandaa mbegu za parachichi kwa matumizi ya dawa.

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuandaa mbegu za maparachichi ili kutumika kama dawa,kwa sababu ya kuwepo kwa tiba kutokana na mbegu hii ni vizuri kujua maandalizi.

Soma Zaidi...