picha

Naulizia nyenzo alizotumia nabii Ada (A.S) kusimamisha ukhalifa

Baada ya Nuhu(a.s) Mtume aliyemfuatia ni Nabii Hud(a.s). Hud(a.s) alitumwa na Mola wake kuwalingania kabila (taifa) la ‘Ad. Kabila la ‘Ad lilikuwa likijulikana kama ‘Ad-al-ram au ‘Ad-Ula. ‘Ad walikuwa wakiishi kusini ya Bara

Swali: 

Naulizia nyenzo alizotumia nabii Ada (A.S) kusimamisha ukhalifa

 

Jibu

Mbinu za Hud(a.s) Katika Kufikisha Ujumbe

 

Katika kulingania Uislamu kwa watu wake, Hud(a.s) alitumia mbinu zifuatazo:


 

Kwanza alijieleza kwa uwazi na kuwanasihi watu wake:

“Akasema: Enyi kaumu yangu! Mimi sio mpumbavu. Lakini mimi ni Mtume niliyetoka kwa Mola wa walimwengu. Nakufikishieni ujumbe wa Mola wangu. Na mimi kwenu ni (mtu) nasihi muaminifu.(7:67-68)


 


Mnaona ajabu kukufikieni mawaidha yanayotoka kwa Mola wenu kwa (ulimi wa) mtu aliye mmoja katika nyinyi ili akuonyeni? (Muabuduni Mwenyezi Mungu) na mkumbuke alivyokufanyeni Khalifa baada ya watu wa Nuhu.Na akakuzidisheni sana katika umbo. Basi zikumbukeni neema za Mwenyezi Mungu ili mpate kufaulu.” (7:69)


 

Pili aliwapa hoja kwanini wanalazimika kumuamini Allah na kumuabudu ipasavyo.


 


Mcheni yule ambaye amekupeni haya mnayoyajua.” “Amekupeni (chungu ya) wanyama na watoto wanaume.” “Na mabustani na chemchem, (mito).” (26:132-134)


 

Tatu, aliwabashiria kupata malipo mema hapa hapa ulimwe nguni endapo watamcha Allah(s.w) ipasavyo:


 

“Enyi watu wangu! Ombeni msamaha kwa Mola wenu (kwa mabaya yenu yaliyopita) kisha mtubie kwake, atakuleteeni mawingu yateremshayo mvua tele, na atakuzidishieni nguvu juu ya nguvu zenu (mlizonazo). Wala msikengeuke kuwa waovu.” (11:52)


 

Nne, aliwahofisha watu wake na adhabu kali ya Allah(s.w)
iwapo watamuasi.


 

“Na kama mtarudi nyuma (hainidhurishi kitu); nimekwisha kukufikishieni niliyotumwa nayo kwenu; na Mola wangu atawafanya makhalifa (wakazi wa mahali hapa) watu wengine wasiokuwa nyinyi; wala nyinyi hamtaweza kumdhuru hata kidogo. Hakika Mola wangu ni Mwenye kuhifadhi kila kitu.” (11:57)


 

“(Wakumbushe) alipowaambia ndugu yao Hud.‘Je, hamtamu ogopa (Mwenyezi Mungu hata nikikutajieni adhabu yot itakayokufikieni kwa mabaya yenu mnayoyafanya)? Bila shaka mimi kwenu ni Mtume muaminifu.” (26:124-125).


 

Tano,aliwafahamisha kwa uwazi watu wake kuwa hakutarajia kupata malipo ya Utume wake kutoa kwao.


 

“Enyi watu wangu! Sikuombeni ujira juu ya haya. Haukuwa ujira wangu ila kwa yule aliyeniumba. Basi hamyatii akilini (haya ninayokuambieni)?” (11:51).


 

“Wala sikutakieni juu yake ujira, ujira wangu haupo ila kwa
Mola wa walimwengu wote.” (26:127)

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: General Main: Post File: Download PDF Views 1078

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 Dua za Mitume na Manabii     👉4 ai web app     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Elimu juu ya afya ya uzazi

Makala hii itakwenda kukufundisha mambo mbalimbali na muhimu kuhusu afya ya uzazi

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa chunusi

Posti hii inaonyesha dalili,sababu na matatizo ya chunusi

Soma Zaidi...
NINI VIDONDA VYA TUMBO?

Ni vidonda vinavyotokea katika ukuta wa tumbo. Vidonda hivi tumezoea kuviita vidonda vya tumbo ila hapa nitataja kitaalamu kuwa vidonda hivi hufahamika kama peptic ulcers.

Soma Zaidi...
Faida za mbegu za maparachichi.

Posti hii inahusu zaidi faida za mbegu za maparachichi, kwa kawaida tunajua wazi faida za maparachichi pamoja na faida za maparachichi kuna faida kubwa katika mbegu zake kama tutakavyoona

Soma Zaidi...
Sababu zinazopelekea kujamiina kwa uchungu (maumivu)

kijamiana kwa uchungu kitaalamu hujulikana Kama dysarthria ambayo inafafanuliwa kuwa maumivu ya mara kwa mara au ya mara kwa mara katika sehemu ya siri ambayo hutokea kabla tu, wakati au baada ya kujamiiana

Soma Zaidi...
KOSA LANGU LIKO WAPI

Post hii inahusu Vijana walivyoingiliana kwenye mahusiano na kusababisha kitoelewana kwa hiyo tutaona jinsi walivyoendeleana na kusababisha maumivu zaidi.

Soma Zaidi...