Baada ya Nuhu(a.s) Mtume aliyemfuatia ni Nabii Hud(a.s). Hud(a.s) alitumwa na Mola wake kuwalingania kabila (taifa) la ‘Ad. Kabila la ‘Ad lilikuwa likijulikana kama ‘Ad-al-ram au ‘Ad-Ula. ‘Ad walikuwa wakiishi kusini ya Bara
Swali:
Naulizia nyenzo alizotumia nabii Ada (A.S) kusimamisha ukhalifa
Jibu
Katika kulingania Uislamu kwa watu wake, Hud(a.s) alitumia mbinu zifuatazo:
Kwanza alijieleza kwa uwazi na kuwanasihi watu wake:
“Akasema: Enyi kaumu yangu! Mimi sio mpumbavu. Lakini mimi ni Mtume niliyetoka kwa Mola wa walimwengu. Nakufikishieni ujumbe wa Mola wangu. Na mimi kwenu ni (mtu) nasihi muaminifu.(7:67-68)
Mnaona ajabu kukufikieni mawaidha yanayotoka kwa Mola wenu kwa (ulimi wa) mtu aliye mmoja katika nyinyi ili akuonyeni? (Muabuduni Mwenyezi Mungu) na mkumbuke alivyokufanyeni Khalifa baada ya watu wa Nuhu.Na akakuzidisheni sana katika umbo. Basi zikumbukeni neema za Mwenyezi Mungu ili mpate kufaulu.” (7:69)
Pili aliwapa hoja kwanini wanalazimika kumuamini Allah na kumuabudu ipasavyo.
Mcheni yule ambaye amekupeni haya mnayoyajua.” “Amekupeni (chungu ya) wanyama na watoto wanaume.” “Na mabustani na chemchem, (mito).” (26:132-134)
Tatu, aliwabashiria kupata malipo mema hapa hapa ulimwe nguni endapo watamcha Allah(s.w) ipasavyo:
“Enyi watu wangu! Ombeni msamaha kwa Mola wenu (kwa mabaya yenu yaliyopita) kisha mtubie kwake, atakuleteeni mawingu yateremshayo mvua tele, na atakuzidishieni nguvu juu ya nguvu zenu (mlizonazo). Wala msikengeuke kuwa waovu.” (11:52)
Nne, aliwahofisha watu wake na adhabu kali ya Allah(s.w)
iwapo watamuasi.
“Na kama mtarudi nyuma (hainidhurishi kitu); nimekwisha kukufikishieni niliyotumwa nayo kwenu; na Mola wangu atawafanya makhalifa (wakazi wa mahali hapa) watu wengine wasiokuwa nyinyi; wala nyinyi hamtaweza kumdhuru hata kidogo. Hakika Mola wangu ni Mwenye kuhifadhi kila kitu.” (11:57)
“(Wakumbushe) alipowaambia ndugu yao Hud.‘Je, hamtamu ogopa (Mwenyezi Mungu hata nikikutajieni adhabu yot itakayokufikieni kwa mabaya yenu mnayoyafanya)? Bila shaka mimi kwenu ni Mtume muaminifu.” (26:124-125).
Tano,aliwafahamisha kwa uwazi watu wake kuwa hakutarajia kupata malipo ya Utume wake kutoa kwao.
“Enyi watu wangu! Sikuombeni ujira juu ya haya. Haukuwa ujira wangu ila kwa yule aliyeniumba. Basi hamyatii akilini (haya ninayokuambieni)?” (11:51).
“Wala sikutakieni juu yake ujira, ujira wangu haupo ila kwa
Mola wa walimwengu wote.” (26:127)
Umeionaje Makala hii.. ?
Sty ni uvimbe mwekundu, chungu karibu na ukingo wa kope ambalo linaweza kuonekana kama jipu au chunusi. Sties mara nyingi hujazwa na usaha. Mtindo kawaida huunda nje ya kope lako. Lakini wakati mwingine inaweza kuunda kwenye sehemu ya ndani ya kope lak
Soma Zaidi...Post hii inahusu Vijana walivyoingiliana kwenye mahusiano na kusababisha kitoelewana kwa hiyo tutaona jinsi walivyoendeleana na kusababisha maumivu zaidi.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za mbegu za maboga
Soma Zaidi...Nahitimisha kwa kusema ili ufanikiwe katika kuwa mahili wa kutafuta taarifa mtandaoni au kujifunza chochote mtandaoni ni lazima uelewe kuwa borwser au kivinjali kwa kiswahili ndio kama njia ya wewe kuingilia tovuti yoyote ile duniani.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi tabia za watu wenye damu la kundi A na vyakula ambavyo wanapaswa kuvitumia, na pengine tutaona baadhi ya vyakula ambavyo havipaswi kutumiwa na watu wenye damu ya kundi A au group A
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu ugonjwa wa Maambukizi kwenye mifupa, kwa hiyo tusipotibu tunaweza kupata madhara yafuatayo.
Soma Zaidi...Maambukizi ya bakterial aina ya shigela ni maambukizi ya utumbo unaosababishwa na familia ya bakteria wanaojulikana kama shigella. Ishara kuu ya maambukizi ya shigella ni kuhara, ambayo mara nyingi huwa na damu.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi madhara ya kupiga punyeto, ni madhara yanayotokea kwa watu wanapenda kupiga punyeto.
Soma Zaidi...