Baada ya Nuhu(a.s) Mtume aliyemfuatia ni Nabii Hud(a.s). Hud(a.s) alitumwa na Mola wake kuwalingania kabila (taifa) la ‘Ad. Kabila la ‘Ad lilikuwa likijulikana kama ‘Ad-al-ram au ‘Ad-Ula. ‘Ad walikuwa wakiishi kusini ya Bara
Swali:
Naulizia nyenzo alizotumia nabii Ada (A.S) kusimamisha ukhalifa
Jibu
Katika kulingania Uislamu kwa watu wake, Hud(a.s) alitumia mbinu zifuatazo:
Kwanza alijieleza kwa uwazi na kuwanasihi watu wake:
“Akasema: Enyi kaumu yangu! Mimi sio mpumbavu. Lakini mimi ni Mtume niliyetoka kwa Mola wa walimwengu. Nakufikishieni ujumbe wa Mola wangu. Na mimi kwenu ni (mtu) nasihi muaminifu.(7:67-68)
Mnaona ajabu kukufikieni mawaidha yanayotoka kwa Mola wenu kwa (ulimi wa) mtu aliye mmoja katika nyinyi ili akuonyeni? (Muabuduni Mwenyezi Mungu) na mkumbuke alivyokufanyeni Khalifa baada ya watu wa Nuhu.Na akakuzidisheni sana katika umbo. Basi zikumbukeni neema za Mwenyezi Mungu ili mpate kufaulu.” (7:69)
Pili aliwapa hoja kwanini wanalazimika kumuamini Allah na kumuabudu ipasavyo.
Mcheni yule ambaye amekupeni haya mnayoyajua.” “Amekupeni (chungu ya) wanyama na watoto wanaume.” “Na mabustani na chemchem, (mito).” (26:132-134)
Tatu, aliwabashiria kupata malipo mema hapa hapa ulimwe nguni endapo watamcha Allah(s.w) ipasavyo:
“Enyi watu wangu! Ombeni msamaha kwa Mola wenu (kwa mabaya yenu yaliyopita) kisha mtubie kwake, atakuleteeni mawingu yateremshayo mvua tele, na atakuzidishieni nguvu juu ya nguvu zenu (mlizonazo). Wala msikengeuke kuwa waovu.” (11:52)
Nne, aliwahofisha watu wake na adhabu kali ya Allah(s.w)
iwapo watamuasi.
“Na kama mtarudi nyuma (hainidhurishi kitu); nimekwisha kukufikishieni niliyotumwa nayo kwenu; na Mola wangu atawafanya makhalifa (wakazi wa mahali hapa) watu wengine wasiokuwa nyinyi; wala nyinyi hamtaweza kumdhuru hata kidogo. Hakika Mola wangu ni Mwenye kuhifadhi kila kitu.” (11:57)
“(Wakumbushe) alipowaambia ndugu yao Hud.‘Je, hamtamu ogopa (Mwenyezi Mungu hata nikikutajieni adhabu yot itakayokufikieni kwa mabaya yenu mnayoyafanya)? Bila shaka mimi kwenu ni Mtume muaminifu.” (26:124-125).
Tano,aliwafahamisha kwa uwazi watu wake kuwa hakutarajia kupata malipo ya Utume wake kutoa kwao.
“Enyi watu wangu! Sikuombeni ujira juu ya haya. Haukuwa ujira wangu ila kwa yule aliyeniumba. Basi hamyatii akilini (haya ninayokuambieni)?” (11:51).
“Wala sikutakieni juu yake ujira, ujira wangu haupo ila kwa
Mola wa walimwengu wote.” (26:127)
Umeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi jeraha kwenye ubongo hasahasa jeraha la kawaida yaani lisilokuwa kali, ni jeraha ambalo utokana na ajali au kupigwa na kitu chochote kwenye kichwa, zifuatazo ni dalili za jeraha lisilokuwa la kawaida kwenye ubongo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi tabia na vyakula wanavyopaswa kutumia watu wenye damu ya kundi AB
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za mbegu za papai na umuhimu wake kiafya
Soma Zaidi...Posti hii inaonyesha Faida za vitunguu swaumu.vitunguu swaumu sio kiungo Cha chakula tu kama desturi ya watu wengi wanavyojua Bali kitunguu swaumu kimesimama Kama dawa pia ya kutibu maradhi na Magonjwa mengi mwilini.
Soma Zaidi...In fact there is a lot of signs and symptoms of pregnancy a mother experiences throughout pregnant. These signs may start to be revealed immediately after conception or in the first week after conception. A term pregnancy is traditionally calculated by mi
Soma Zaidi...Kutengeneza tovuti ni jambo moja na kuilinda ni jambo la pili. Kutokana na kukua kwa sayansi na teknolojia, kumepelekea kukua na kushamiri kwa uhalifu kwa njia ya mtandao.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalili zilizopo katika matatizo ya ngono.
Soma Zaidi...