SWALI

Mm nimedunga sindano tarehe tano za mwezi wa kwanza n'a mpaka sasa sijaona siku zangu ila nabaki nasikia maumivu chini ya kitovu kwa mbali n'a nimefanya tendo la ndowa siku iliofuata tarehe 6 je naweza kupata mimba? 

Swali No. 324




JIBU

Kwanza utambue kuwa kutopata siku zako sio pekee dalili ya ujauzito. Inaweza kuwa ni side effect ya hiyo sindano. 

 

Pili, mabadiliko tu ya homoni yanaweza kusababisha maumivu na kukosa hedhi. 

 

Tatu dawa za uzazi nasra nyingi husababisha mabadiliko kama hayo. 

 

Jambo la msingi ni kuonana na daktari wako akufanyie uchunguzi juu ya sindano hiyo. Kama inakudhuru akubadilishie. 

 

Hata hivyo yeye inawezekana kupata ujauzito hata kama umetumia sindano endapo kuna shida imetokea lamda dawa imeshindwa kufanya kazi vyema. 



Kumbukumbu
Swali hili limeulizwa na Muulizaji Kutoka WhatsApp Chat yetu tarehe 15-02-2023-12:33:17 . Jina la muulizaji limehifadhiwa.

Nicheki Nicheki WhatsApp






MASWALI YANAYOFANANA