Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 57: Mkataba wa udhalimu

Baada ya Baini Abd Manaf kukubaliana kumlinda Mtume Muhammad basi Maquraish wakaweka mkataba wa udhalimu utakaozuia kutoshirikiana na banu abd Manaf kwa lolote lile.

Mkataba wa udhalimu

Matukio manne muhimu yalitokea ndani ya kipindi cha chini ya mwezi mmoja — kuongoka kwa Hamzah, kuongoka kwa ‘Umar, kukataa kwa Muhammad (Rehema na Amani ziwe juu yake) kufanya mazungumzo ya maelewano, na agano lililowekwa kati ya Banu Muttalib na Banu Hashim la kumkinga Muhammad (Rehema na Amani ziwe juu yake) dhidi ya jaribio lolote la hila la kumwua. 

 

Makafiri walishangazwa na kutojua hatua waliyopaswa kuchukua ili kujiondoa kwenye kikwazo hiki cha kijasiri na kisichokoma ambacho kilionekana kuvuruga utamaduni wao wote wa maisha. Walikuwa tayari wanajua kwamba kama wangeweza kumwua Muhammad (Rehema na Amani ziwe juu yake), damu ingemwagika sana katika mabonde ya Makkah na bila shaka wangekuwa wamedhulumiwa. Kutokana na hatari hii ya kutisha, walikubaliana kwa unyonge kuchukua njia nyingine ya dhulma ambayo haikuhusisha mauaji.

 

AGANO LA DHULUMA NA UADUI

Washirikina wa Makkah walikutana katika mahali panapoitwa Wadi Al-Muhassab, na wakaweka mkataba wa uhasama dhidi ya Bani Hashim na Bani Al-Muttalib. Walikubaliana kutokuwa na biashara yoyote nao wala ndoa za kindugu. Mahusiano ya kijamii, matembezi na hata mawasiliano ya maneno na Muhammad (Rehema na Amani ziwe juu yake) na wafuasi wake yalikoma hadi Mtume (Rehema na Amani ziwe juu yake) atakapokabidhiwa kwao ili auawe. Vipengele vya tangazo lao vilivyojumuisha hatua kali dhidi ya Bani Hashim vilinakiliwa na mshirikina, Bagheed bin ‘Amir bin Hashim, na kisha kupelekwa kwenye Al-Ka‘bah. Mtume (Rehema na Amani ziwe juu yake) alimuomba Mwenyezi Mungu amlaani Bagheed, na mkono wake ulipooza baadaye.

 

Abu Talib kwa busara na utulivu alichukua hatua na kuamua kujiondoa kwenye bonde lililokuwa mashariki mwa Makkah. Banu Hashim na Banu Al-Muttalib walifuata mfano huo na wakajikusanya ndani ya njia nyembamba (Shi‘b ya Abu Talib), kuanzia mwanzoni mwa Muharram, mwaka wa saba wa utume wa Muhammad hadi mwaka wa kumi, kipindi cha miaka mitatu. Ilikuwa ni kuzingirwa kukali. Ugavi wa chakula ulikoma karibu kabisa na watu waliokuwa wamezingirwa walikabiliwa na mateso makubwa. Washirikina walinunua bidhaa za chakula zilizokuwa zikiingia Makkah ili zisifikie watu waliokuwa Ash-Shi‘b, ambao walipata taabu sana kiasi cha kulazimika kula majani ya miti na ngozi za wanyama. 

 

Vilio vya watoto wadogo walioumia kwa njaa vilisikika waziwazi. Hakuna kitu cha kula kilichowafikia isipokuwa kwa nyakati chache tu, ambapo chakula kidogo kilifichwa na baadhi ya wakaazi wa Makkah walio na huruma. Wakati wa miezi iliyokatazwa kufanya vita — ambapo uhasama ulisitishwa kwa kawaida, walitoka kwenye kifungo na kununua chakula kilichotoka nje ya Makkah. Hata hivyo, bidhaa zilikuwa na bei ya juu isiyo haki ili hali yao ya kifedha isiwaruhusu kuzipata.

 

UTATA NA KUSAMBARATIKA KWA MKATABA

Hali hii hatimaye ilisababisha mfarakano kati ya makundi mbalimbali ya Makkah, ambao walikuwa na uhusiano wa damu na watu waliowekwa kwenye kifungo. Baada ya miaka mitatu ya kizuizi, na katika Muharram, mwaka wa kumi wa utume wa Muhammad, mkataba ulivunjika. Hisham bin ‘Amr, ambaye kwa siri alikuwa akiingiza chakula kwa Bani Hashim wakati wa usiku, alienda kumuona Zuhair bin Abi Omaiyah Al-Makhzoumy na kumkosoa kwa kukubali kimya hali hiyo isiyovumilika iliyokuwa ikiwakumba wajomba zake walioko uhamishoni. 

 

Alikubaliana kufanya kazi pamoja na Hisham kuunda kundi la shinikizo la kukomesha kifungo hicho. Kundi la watu watano waliungana kwa msingi wa uhusiano wa damu ili kubatilisha mkataba na kutangaza kwamba vipengele vyote vya mkataba huo ni batili. Walikuwa Hisham bin ‘Amr, Zuhair bin Abi Omaiyah, Al-Mut‘im bin ‘Adi, Abu Al-Bukhtari na Zam‘a bin Al-Aswad. Walikubaliana kukutana kwenye eneo lao la mkutano na kuanza kazi yao kwenye eneo la Al-Ka‘bah.

 

Katika wakati huo, Abu Talib alikuwa amekaa pembezoni mwa Msikiti. Alipowajulisha kuwa Wahyi ulikuwa umeteremshwa kwa Mtume (Rehema na Amani ziwe juu yake) kwamba mchwa walikuwa wamekula mkataba wote isipokuwa sehemu iliyokuwa na jina la Mwenyezi Mungu, alipendekeza kuwa kama maneno yake hayangekuwa kweli, wangekuwa tayari kumtoa Muhammad (Rehema na Amani ziwe juu yake) kwao, vinginevyo wangekubaliana kuvunja mkataba huo. Wakamakubali. Al-Mut‘im alienda kukagua mkataba na akakuta kuwa ulikuwa umeharibiwa na mchwa isipokuwa sehemu iliyoandikwa jina la Allah.

 

Tangazo hilo lilivunjwa hivyo, na Muhammad (Rehema na Amani ziwe juu yake) na watu waliobaki waliruhusiwa kutoka Ash-Sh‘ib na kurejea nyumbani.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Historia ya Mtume Muhammad (s.a.w) Main: Dini File: Download PDF Views 155

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 24: Katika pango la Hira

Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu yaliyojiri katka pango la Hira kabla ya kupokea utume

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 50: Historia ya safari ya Hijra ya kwanza kuelekea Ethiopia

Hapa tutakwend akujifunz akwa urefu zaidi kuhusu safari hii ya kwanz aya kuelekea Ethiopia inayojulkana kama Hijra ya kwanza.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 63: Kuingia uislamu Madina

Katika somo hili utakwend akujifunz ahistoria ya kuingia Uislamu katika mji wa Makkah

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 14: Historia ya Amina mama wa Mtume Muhammad

Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu historia ya Amina mama wa Mtume Muhammad ﷺ

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 39: Baraza la ushauri kuwazuia mahujaji kumfuata Muhammad ﷺ

Katika somo hili utakwenda ujifunza kuhusu uwamuzi wa Baraza la ushauri kuwazuia mahujaji kumfuata Muhammad ﷺ wakati wa msimu wa hija.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 52: Maamuzi ya kumuuwa Mtume Muhammad

Baada ya mbinu nyingi za Maquraish kufeli sasa wanaamuwa bora tu wamuuwe Muhammad ili kukomesha kuendelea mafundishio bya dini mpya.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 61: Matukie mengineyo kwneye safari ya Taif

Baadhi ya matukio mengine yaliyoteokea kweye safari hii ya Tfai

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 26: Kusimama kwa Wahy

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu kusimama kwa Wahyi kuja kwa Mtume Muhammad ﷺ

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 33: Mquraishi wanagunduwa kuhusu dini Mpya

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu namna ambavyo wito wa ulingano ulipoenea na kuwafikia maquraish na washirikina

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ﷺ somo la 11: Kufarki kwa babu yake na kulelewa na baba yake mkubwa

Katika somo hili utajifunza kuhusu Mtume MUhammad ﷺ kulelewa na Kufarki kwa babu yake na kulelewa na baba yake mkubwa:

Soma Zaidi...