image

Hadithi ya kinyozi yeye mwenyew

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani

HADITHI YA KINYOZI YEYE MWENYEWE

Mimi si mtu wa maneno mengi kama kijana anavyonidhania. Hata hivyo nipo tofauti sana na kaka zangu kwani mimi ndiye mtoto wa mwisho.. nitakusimulieni kisa kimoja hapa ndipo mtagundua kuwa mimi si mtu wa maneno mengi. Siku moja nilipokuwa sina kitu cha kukila na kwa kuwa mimi si mtu wa maneno mengi sikuweza kwenda kukopa. Niliweza kusikia wepesi wa tumbo langu kwa njaa, hata nikathubutu kufunga kipande cha kanga tumboni. Sikujuwa ni kwa nini siku ile nilikuwa na njaa sana. Niliamini huenda ikawa ni majaribu yamenifikia. Mingurumo ya tumbo ilizidi kusumbua.

 

Basi katika pirika zangu nikakutana na vijana 10 wapo kwenye dau. Kwa mawazo yangu nikadhani wanakwenda kusherehekea. Na hii ilikuwa ni kawaida kwa vijana wakikusanyika eneo hili wanakwenda upande wa pili wa mto kufurahia na kula na kunywa. Mawazo ya njaa yalikuja karibu zaidi hata ikawa chakula kama kipo mbele yangu. Nikaanza kupata harufu ya paja la kuku lililokaangwa na kukaushwa vyema. Chapati za mayai zilizofunika samaki vyema. Harufu ya juisi nikaanza kuipata kwa mbaali wakati nakodolea macho paja la kuku.

 

Kwa njaa zangu na pupa ndipo nikakimbilia bilauri ya juisi na kuanguka. Loo! Nimevunja bilauri ya watu. Ghafla nikashituka kutoka kwenye dimbwi la mawazo. Nikawahi kwenye dau na mimi kuingia. Bila hata ya kuuliza zaidi kilichowakuta na wapi wanakwenda. Kwa kuwa mimi si mtu wa maneno mengi sikuweza kuuliza sana. Nahodha akang’oa dau na kuanza kutokomea mtoni. Nilianza kushangaa kumbe vijana wote 10 waliomo mule wamefungwa minyororo, na walikuwa chini ya uangalizi wa askari. Kwa kuwa mimi si mtu wa maneno mengi niliendelea kuwa kimya.

 

Tulipofika ng’ambu ya pili ya mto tulipokelewa na kundi kubwa la askari na kupelekwa kwa kadhi. Sikuzungumza kitu na wala sikujitetea kwa lolote. Ni kwa sababu mimi si mtu wa maneno mengi. Tulipofika kwa kadhi wale mabwana kumbe walikuwa na kosa na mauwaji na hivyo kadhi akaamuriu vijana wote 10 wakatwe vichwa vyao mara moja. Kwa kuwa mimi si mtu wa maneno mengi niliendelea kukaa kimya none hatma ya uwepo wangu pale. Basi askari akawachukuwa wote vijana 10 na kwenda kukata vichwa vyao.

 

Baada ya muda kidogo askari akaja mbele ya kadhi na kutamka kuwa kazi imekwisha, yaani ameshakata vichwa vyao. Kadhi akamuuliza mbona umechukuwa 9 na huyu wa 10 umemuacha hapa. Askari akajibu hapana mkuu nimechukuwa wote 10. kadhi hakuamini hata akaenda kuhesabu vichwa. Loo! Ni kweli vichwa vilikamilika 10. hapa kadhi akawa na furushi la maswali kichwani mwake. Furushi lote akataka kunitundika mimi. Kwa kuwa mimi si mtu wa maneno mengi niliendelea kunyamaza. Kadhi akaja akiwa amefura kw ahasira na mawazo.

 

Alipokaa vyema akaagiza aletewe maji kwenye chombo. Kadha alipoletewa maji alikuywa na kutawadha. Alifanya hivi ili kupunguza hasira, ili asijefanya maamuzi yasiyo ya haki. Kisha kadhi akaniuliza haya wewe ni nanai na imekuwaje akuajumlishwa kwenye kundi hili la watu wabaya? Basi sasa sina budi nikaanza kumueleza Kadhi namna nilivyofika pale. Kadhi alishangaa sana kuona vile hivyo akanieleza kuwa ni kwa nini hukuzungumza toka mwanzo. Nikamueleza kuwa mimi si mtu wa maneno mengi. Nikaendelea “usidhani kuwa mimi ni mtu wa maneno mengi, mimi ni tofauti sana na kaka zangu.

 

Kwani kaka yangu wa kwanza ni kichaa na ameupata ukichaa kutokana na yaliyomkuta na maneno mengi yake. Ili uamini kuwa mimi si mtu wa maneno mengi, nitakuhadithia yaliyowapata kaka zangu wote kutokana na maneno yao mengi. Baada ya kuzungumza hivi kinyozi akaanza kuhadithia yaliyotokea kwa kaka wake wa kwanza: 





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1229


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Siku ya sita ya wageni
SIKU YA SITA YA WAGENI Siku ya sita walianza mapema kama siku ya nne kisha wakamueleza baba awapeleke msituni. Soma Zaidi...

ALADINI KATIKA PANGO LA UTAJIRI
Soma Zaidi...

Hadithi ya kinyozi kaka wa pili
Soma Zaidi...

Hadithi iliyosimuliwa na tabibu
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

NDANI YA JUMBA LA ALADINI
Soma Zaidi...

Hatma ya kijana mchonganishi
Soma Zaidi...

Hadithi iliyosimuliwa na mshona nguo
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Harusi ya aladini na binti sultani
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...

Hadithi ya Kaka wa tatu wa kinyozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Jaribio la tatu la aladini
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...

Jaribio la kwanza la aladini
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...

NJE YA JUMBA LA KIFAHARI JUMBA LA ALADINI
Soma Zaidi...