Katika somo hili, utajifunza vipimo vinavyotumika kwenye CSS kama vile px, em, rem, %, vw, na vh. Vipimo hivi hutumika kuweka ukubwa wa maandishi, padding, margin, urefu, na upana wa vipengele kwenye tovuti.
Katika CSS, vipimo hutumika kuelezea ukubwa wa vitu kama maandishi, nafasi, au vipengele vyenyewe. Ili tovuti ionekane vizuri kwenye vifaa vya ukubwa tofauti, ni muhimu kuelewa aina tofauti za vipimo na matumizi yake sahihi.
px – PixelPixel ni kipimo cha kudumu (fixed unit).
Haina uhusiano na ukubwa wa skrini.
p {
font-size: 16px;
}
💡 Inafaa kwa vipengele vinavyohitaji ukubwa thabiti.
% – AsilimiaAsilimia hujitegemea kulingana na mzazi wake (parent element).
Inatumika sana kwenye upana (width), urefu (height), na margin.
div {
width: 80%;
}
💡 Ukisema 80%, maana yake element itachukua 80% ya mzazi wake.
em – Relative to Parent Font Size1em ni sawa na ukubwa wa font ya mzazi wake.
Ukisema 2em, maana yake ni mara mbili ya font-size ya mzazi.
body {
font-size: 16px;
}
p {
font-size: 2em; /* 32px */
}
rem – Relative to Root (html) Font Size1rem ni sawa na font-size ya mzizi (html).
Inasaidia kuweka vipimo vinavyolingana kwenye ukurasa mzima.
html {
font-size: 16px;
}
h1 {
font-size: 3rem; /* 48px */
}
vw – Viewport Width1vw ni 1% ya upana wa skrini (viewport).
.box {
width: 50vw; /* 50% ya upana wa skrini */
}
vh – Viewport Height1vh ni 1% ya urefu wa skrini.
.hero {
height: 100vh; /* 100% ya urefu wa skrini */
}
| Unit | Inategemea nini? | Mfano wa Matumizi |
|---|---|---|
| px | Ukubwa wa kudumu (fixed) | font-size, width |
| % | Ukubwa wa mzazi | width, height |
| em | Font-size ya mzazi | padding, font-size |
| rem | Font-size ya html |
font-size ya mwili |
| vw | Upana wa dirisha la browser | layout ya ukurasa mzima |
| vh | Urefu wa dirisha la browser | sehemu za "full screen" |
Kuelewa units za CSS ni msingi wa kutengeneza tovuti zinazobadilika vizuri. Tumia rem kwa consistency, % kwa layouts zinazobadilika, na vw/vh kwa vipengele vinavyojaza skrini.
Tutajifunza jinsi ya kufanya harakati (motion) na mabadiliko ya mwonekano kwa kutumia transition, transform, na @keyframes.
1rem inategemea nini?
a) Ukubwa wa mzazi wa element
b) Ukubwa wa mzizi (html)
c) Ukubwa wa skrini
d) Ukubwa wa picha
50% ya width ina maana gani?
a) Element ni nusu ya upana wa mzazi wake
b) Nusu ya ukurasa
c) Nusu ya font-size
d) Haina maana
1vw inamaanisha nini?
a) 1% ya urefu wa skrini
b) 1 pixel tu
c) 1% ya upana wa skrini
d) Kiwango cha padding
Tofauti kuu kati ya em na rem ni ipi?
a) em ni fixed, rem ni relative
b) em hutegemea mzazi, rem hutegemea mzizi
c) rem hutegemea picha
d) Hakuna tofauti
Unit gani inayofaa zaidi kwa full-screen background?
a) px
b) %
c) em
d) vh
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili utajifunza tofauti kati ya margin na padding, kazi ya kila moja, jinsi ya kuzipima, na jinsi zinavyotumika kudhibiti nafasi ndani na nje ya elementi kwenye ukurasa wa HTML.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza kuhusu property muhimu ya CSS inayoitwa display, ambayo huamua jinsi element inavyoonyeshwa kwenye ukurasa. Tutachambua aina kuu za display: block, inline, inline-block, na none.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutajifunza kuhusu CSS Filters — mitindo inayotumika kuhariri mwonekano wa picha, video, au elementi nyingine kwa kuongeza athari kama blur, brightness, contrast, grayscale, na nyinginezo. Hii huifanya tovuti kuwa ya kisasa, ya kuvutia, na yenye mwingiliano mzuri.
Soma Zaidi...Katika somo hili, utajifunza jinsi ya kudhibiti muonekano wa sehemu ya nyuma (background) ya HTML element kwa kutumia CSS. Utaweza kuongeza rangi, picha, kuweka picha zisirudiwarudiwe, na hata kusogeza picha kwenye maeneo tofauti ya ukurasa.
Soma Zaidi...Katika somo hili, tutajifunza kuhusu CSS functions muhimu zinazotumika kufanya mahesabu, kuweka vipimo vya kisasa vinavyobadilika kulingana na hali ya kifaa, na kutumia variables. Tutazingatia functions kama: calc(), clamp(), var(), min(), max(), na mwishoni tutajifunza jinsi ya kutengeneza custom function kwa kutumia variables.
Soma Zaidi...Katika somo hili, utajifunza mbinu mbalimbali za kubadilisha muonekano wa maandishi kwa kutumia CSS, kama vile kupamba maandishi kwa mistari, kivuli, nafasi kati ya herufi, na mpangilio wa maneno.
Soma Zaidi...Katika somo hili, tutajifunza kuhusu CSS Specificity — yaani mfumo wa kipaumbele unaotumiwa na kivinjari kuchagua ni mtindo (style) upi utumike iwapo kuna migongano kati ya selectors mbalimbali. Utaelewa jinsi ya kupanga selectors zako vizuri ili kuzuia matatizo ya mitindo kutofanya kazi kama ulivyotarajia.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutumia float ili kupanga elementi upande wa kushoto (left) au kulia (right). Pia utajifunza jinsi ya kutumia clear kuondoa athari za float na kuhakikisha layout yako inabaki thabiti.
Soma Zaidi...Mfano wa kitu kinachoweza kumaba mtoto kooni ni kama chagula kigumu, pesa ya sarafu, kijiwe na mengineyo. Endapo hili litataokea msaada wa haraka unahitajika kwa ulazima.
Soma Zaidi...Katika somo hili, tutajifunza jinsi ya kuleta miondoko na harakati kwenye tovuti kwa kutumia CSS Transitions na Animations. Hii itasaidia kuboresha muonekano na matumizi ya tovuti.
Soma Zaidi...