Ni zipi sifa za imamu wa swala?

Ni zipi sifa za imamu wa swala?

Sifa za Imamu Imamu ni kiongo kuongoza swala:



1. Mwenye zi. Mtu yeyote mwenye sifa zifuatazo anaweza
kuweza kuisoma Qur-an vizuri na mwenye
kuielewa vizuri.
2. Anayefahamu na kuelewa vizuri hadithi na Sunnah.
3. Mwenye tabia njema na siha nzuri.
4. Mwenye umri mkubwa (sifa hizi zizingatiwe kwa mfuatano wake).



Kama itatokea kwenye msikiti mmoja kuna watu wengi wenye sifa hizi, itabidi ipigwe kura. Pia kiongozi au mtu mwenye mamlaka katika jamii atakuwa ndiye mwenye haki ya kuwa Imamu. Hali kadhalika mtu akiwa nyumbani kwake, atakuwa ndiye mwenye haki ya kuwa Imamu. Sifa hizi zinabainishwa katika Hadithi ifuatayo:



Abu Mas 'ud amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: Yule aliye na uwezo mkubwa zaidi wa kusoma Kitabu cha Allah (Qur-an) atakuwa Imamu wao. Kama watakuwa sawa kwa kusoma Qur-an basi atakuwa Imamu yule aliye na ujuzi mkubwa wa Hadithi, na kama wako sawa basi yule aliyetangulia kuhajiri (kuham a kutoka Makka kw enda Madina) na kama wako sawa katika kuhajiri, basi yule aliye na umri mkubwa kuliko wote ndiye atakayekuwa Imamu. Hakuna mtu atakaye kuwa Imamu wa yule aliyemzidi madaraka (au yule aliye na mamlaka juu yake) na wala hatakaa katika nyumba yake kwa kumpa heshima mpaka apate ridhaa yake. Na hakuna mtu atakayekuwa Imamu katika nyumba au familia ya mwingine. (Muslim).



Imamu wa msikiti atakapochaguliwa hapatakuwa na mwingine kuswalisha bila ruhu sa yake. Ni vibaya mno kujipachika Uimamu mahali bila ya ridhaa ya watu unaowaongoza. Aliyejipachika Uimamu swala yake haitasihi.



Ibn Umar amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema kuwa watu w atatu ambao sw ala zao hazitakubaliwa ni: 'Yule anayeswalisha w atu na huku hawamtaki, anayekuja kwenye swala nyuma (kuja kwenye swala baada ya wakati kupita, pia kuswali mwenyewe nyuma ya mstari), na yule anayemfanya mwanamke huru kuwa mtumwa'.(Abu Daud, Ibn Majah).



Kumfuata Imamu baada ya kuwekwa ni jambo la lazima. Hata kama Imamu huyo atafanya makosa au dhambi kubwa kiasi gani kabla Waislamu hawajamtoa na kumweka mwingine itabidi lazima wamfuate kutokana na Hadithi ifuatayo:-



Abu Hurairah (r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah (s.a.w) amesema, 'Jihadi ni wajibu chini ya Amir yeyote akiwa mcha-Mungu, au si mcha-Mungu na hata kama atakuwa amefanya madhambi makubwa, na swala ni wajibu nyuma ya kila Imamu akiwa mcha-Mungu au si mcha-Mungu na hata akiwa amefanya madhambi makubwa '. (Abu Daudi)
Inavyotakiwa, kama Imamu ataonekana kuwa anakiuka miiko ya Kiislamu kwa kutenda yale yaliyokatazwa katika Uislamu, kama vile zinaa, ulevi, wizi, n.k. itabidi Waislamu wamtoe kwenye Uimamu na kuweka Imamu mwingine mwenye sifa zilizotajwa. Kabla ya kuchagua mwingine watawajibika kumfuata Imamu huyo huyo muovu.Hekima yake ni kuepusha ugomvi, mifarakano baina ya waislamu.




                   




Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 427


Download our Apps
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Nini maana ya riba, na yapi madhara yake?
8. Soma Zaidi...

Kwa nini imefaradhishwa kufunga katika Mwezi wa ramadhani?
Soma Zaidi...

SHARTI ZA KUWAJIBIKA KWA ZAKA
Soma Zaidi...

JIFUNZE DINI YA KIISLAMU, quran, hadithi, tawhid, tajwid, sira na fiqh
Jifunze mengi kuhusu dini hapa Soma Zaidi...

Kukaa itiqaf na sheria zake hasa katika mwezi wa ramadhani
Soma Zaidi...

Uislamu ni Nasaha (kunasihiana) kwa Mwenyezi Mungu, Kitabu chake Mtume wake , Viongozi na waislamu wote
' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ' ': "' '?... Soma Zaidi...

TAKBIRA YA KWANZA, DUA BAADA YA TAKBIRA YA KUHIRIMIA SWALA NA KUSOMA ALHAMDU (SURAT AL-FATIHA KWENYE SWALA
2. Soma Zaidi...

Bara la Arabu Zama za Jahiliyyah
Wakati Mtume(s. Soma Zaidi...

NGUZO ZA IMAN
Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala Soma Zaidi...

Lengo la kuletwa mitume
Mitume wameletwa kuwa Waalimu na viongozi wa kuwafundisha watu Uislamu na kuwaelekeza kuusimamisha Uislamu katika jamii kinadharia na kimatendo kama tunavyojifunza katika Qur-an:'Kwa hakika Tuliwapeleka Mitume wetu kwa dalili wazi wazi na Tukavitere.. Soma Zaidi...

Kujiepusha na kukaribia zinaa
Si zinaa tu iliyoharamishwa bali hata yale yote yanayotengeneza mazingira na kuchochea kufanyika kwa zinaa nayo pia yameharamishwa. Soma Zaidi...

Siku ya idi al-fitir na namna ya kusherekea idi
Soma Zaidi...