Sababu za mkojo kushindwa kutoka kwenye kibofu.
Post hii inahusu zaidi mkojo kushindwa kutoka kwenye kibofu na kwa kitaalamu huitwa retention of urine.
Sababu za mkojo kushindwa kutoka kwenye kibofu.
1.kuharibika kwa tezi za kibofu Cha mkojo, wakati mwingine kama Kuna uhary wowote kwenye tezi za kibofu mkojo ushindwa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo ingawa mtu anasikia hamu ya kutoa mkojo lakini hawezi, kltezi za kibofu Cha mkojo kwa kitaamu huitwa prostate gland. Kwa hiyo kama tatizo hilo limetokea mgonjwa anapaswa kumpelekea hospitalini kwa sababu mkojo kubaki ndani ni hatari.
2. Pengine mkojo hushindwa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo kwa sababu ya kufanyiwa upasuaji kwa sababu wakati mwingine Kuna sehemu inaweza kuzibua kwa bahati mbaya au pengine kwa sababu ya kuzoea kutumia milija wa kupitisha mkojo, mtu akitaka kutumia njia ya kawaida mkojo unaweza kushindwa kutoka kwanza lakini kwa sababu ya kuzoea mkojo unaweza kuanza kupita tena baadae kwa mtu Mwenye tatizo hili Inabidi kufuata masharti ya waganga na wauguzi.na ataweza kuelekea kwenye hali ya kawaida.
3. Kushindwa kufanya kazi kwa Neva mbalimbali ambazo uhusika na mkojo.
Nevu mbalimbali zikishindwa kufanya kazi yake kuu ya kuamuru mkojo utokea kwa wakati wake mkojo unaweza kubaki kwa Sababu tunajua kuwa mwilini kwa binadamu Kuna nevu na nevu hizo ndo zinahakikisha kila kitu mwilini linaenda sawa kwa hiyo kama nevu hazifanyi kazi na mkojo utashindwa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo mpaka kazi ya nevu ikamilike.
4. Kuharibika kwa kibofu Cha mkojo.
Wakati mwingine mkojo ukosa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo kwa sababu ya kuharibika kwa sehemu mbalimbali za kibofu Cha mkojo hali hii utokea kwa sababu ya maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo au labda pengine ni kwa sababu ya ajali kwenye kibofu Cha mkojo hali hii usababisha mkojo kushindwa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo, kwa hiyo tunapaswa kuhakikisha kuwa mkojo unatoka kwenye kibofu maana ukibaki ni hatari sana.
5. Pengine mkojo hushindwa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo kwa sababu ya baadhi ya madawa yanayotumiwa na mhusika kama vile atropine na antidepressants, hizi dawa zikileta matokeo kama haya ni lazima mgonjwa apelekwe hospitali mapema Ili kusaidia mkojo uweza kutoka kwenye kibofu Cha mkojo.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 ai web app 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Yajuwe maradhi mbalmbali ya ini na chanzo chake
Ini ni moja ya ogani za mwili ambazo husumbuliwa na maradhi hatari sana. Katika post hii utakwend akuyajuwa maradh hatari ambayo hushambulia ini. Pia utajifunza jinsi a kujikinga na maradhi hayo.
Soma Zaidi...Njia za jumla za kujikinga na magonjwa mbalimbali
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kujikinga na magonjwa, kwa kawaida tunajua wazi kuwa magonjwa yapo na yanasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na mengine hayasambai yanaweza kumpata mtu mmoja akapona au magonjwa mengine si ya kupona
Soma Zaidi...Daliliza shinikizo la Chini la damu.
Shinikizo la chini la damu (hypotension) litaonekana kuwa jambo la kujitahidi. Hata hivyo, kwa watu wengi, shinikizo la chini la damu linaweza kusababisha dalili za Kizunguzungu na kuzirai. Katika hali mbaya, shinikizo la chini la damu linawez
Soma Zaidi...Walio katika hatari ya kupata magonjwa ya ngono
Posti hii inahusu zaidi watu walio kwenye liski ya kupata magonjwa ya ngono, ni watu wanaofanya mambo yanayosababisha kupata magonjwa ya ngono.
Soma Zaidi...Dalili za UKIMWI huonekana baada ya muda gani
Hapa utajifunza muda mabao dalili za VVU na UKIMWI huonekana, na kwa muda gani mgonjwa ataishi na UKIMWI bila ya kutumia ARV
Soma Zaidi...