Sababu za mkojo kushindwa kutoka kwenye kibofu.
Post hii inahusu zaidi mkojo kushindwa kutoka kwenye kibofu na kwa kitaalamu huitwa retention of urine.
Sababu za mkojo kushindwa kutoka kwenye kibofu.
1.kuharibika kwa tezi za kibofu Cha mkojo, wakati mwingine kama Kuna uhary wowote kwenye tezi za kibofu mkojo ushindwa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo ingawa mtu anasikia hamu ya kutoa mkojo lakini hawezi, kltezi za kibofu Cha mkojo kwa kitaamu huitwa prostate gland. Kwa hiyo kama tatizo hilo limetokea mgonjwa anapaswa kumpelekea hospitalini kwa sababu mkojo kubaki ndani ni hatari.
2. Pengine mkojo hushindwa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo kwa sababu ya kufanyiwa upasuaji kwa sababu wakati mwingine Kuna sehemu inaweza kuzibua kwa bahati mbaya au pengine kwa sababu ya kuzoea kutumia milija wa kupitisha mkojo, mtu akitaka kutumia njia ya kawaida mkojo unaweza kushindwa kutoka kwanza lakini kwa sababu ya kuzoea mkojo unaweza kuanza kupita tena baadae kwa mtu Mwenye tatizo hili Inabidi kufuata masharti ya waganga na wauguzi.na ataweza kuelekea kwenye hali ya kawaida.
3. Kushindwa kufanya kazi kwa Neva mbalimbali ambazo uhusika na mkojo.
Nevu mbalimbali zikishindwa kufanya kazi yake kuu ya kuamuru mkojo utokea kwa wakati wake mkojo unaweza kubaki kwa Sababu tunajua kuwa mwilini kwa binadamu Kuna nevu na nevu hizo ndo zinahakikisha kila kitu mwilini linaenda sawa kwa hiyo kama nevu hazifanyi kazi na mkojo utashindwa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo mpaka kazi ya nevu ikamilike.
4. Kuharibika kwa kibofu Cha mkojo.
Wakati mwingine mkojo ukosa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo kwa sababu ya kuharibika kwa sehemu mbalimbali za kibofu Cha mkojo hali hii utokea kwa sababu ya maambukizi kwenye kibofu Cha mkojo au labda pengine ni kwa sababu ya ajali kwenye kibofu Cha mkojo hali hii usababisha mkojo kushindwa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo, kwa hiyo tunapaswa kuhakikisha kuwa mkojo unatoka kwenye kibofu maana ukibaki ni hatari sana.
5. Pengine mkojo hushindwa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo kwa sababu ya baadhi ya madawa yanayotumiwa na mhusika kama vile atropine na antidepressants, hizi dawa zikileta matokeo kama haya ni lazima mgonjwa apelekwe hospitali mapema Ili kusaidia mkojo uweza kutoka kwenye kibofu Cha mkojo.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 Simulizi za Hadithi Audio ๐2 Kitabu cha Afya ๐3 Bongolite - Game zone - Play free game ๐4 Dua za Mitume na Manabii ๐5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) ๐6 ai web app
Post zinazofanana:
Dalili za kifua kikuu kwa watoto.
Posti hii inahusu zaidi dalili za kifua kikuu kwa watoto,ni Dalili ambazo ujitokeza kwa watoto pindi wanapopata Maambukizi ya kifua kikuu.
Soma Zaidi...Samaani nilikuwa nauriza ninasumburiwa na fanga ya mdomoni naomba ushauri
Fangasi mdomoni wanaweza kuwa tatizo endapo hawatatibiwa mapema. Wanaweza kuongeza majeraha kwenye kinywa.
Soma Zaidi...Sababu za Kichwa Kuuma Mara kwa Mara
โKichwa kuuma mara kwa mara ni changamoto inayomfanya mtu kushindwa kutekeleza majukumu yake ya kila siku kwa ufanisi. Makala hii inaangazia sababu mbalimbali za maumivu ya kichwa ya mara kwa mara, jinsi ya kuyatofautisha, na wakati mwafaka wa kutafuta msaada wa kitaalamu
Soma Zaidi...Dalili za madhara ya figo
Posti hii inahusu dalili za figo.figo husawazisha maji mwilini pamoja na kuchuja mkojo.
Soma Zaidi...Kaswende isiyotibiwa: Athari zake kwenye ubongo na moyo.
โKaswende ni ugonjwa wa zinaa (STI) unaosababishwa na bakteria Treponema pallidum. Ingawa ugonjwa huu hupona kirahisi kwa kutumia dawa za antibayotiki (kama Penicillin) katika hatua za awali, kuupuza dalili au kutokumaliza dozi husababisha bakteria kusambaa mwilini na kuathiri mifumo muhimu ya viungo. Makala hii inachunguza hatua ya tatu ya ugonjwa huu (Tertiary Syphilis) na uharibifu wa kudumu inaoweza kusababisha kwenye mfumo wa neva na moyo.
Soma Zaidi...