Json somo la 2: Sheria za uandishi wa Json
Katika somo hili utakwenda kujifunza sheria za uandishi wa json
Sheria za Kuandika JSON
Kabla ya kuanza kuandika JSON, ni muhimu kuelewa sheria zake. Sheria hizi zitakusaidia kuandika data sahihi na kuepuka makosa.
1. JSON Huandikwa kwa Jozi za Key na Value
-
Kila jozi ya data ina key na value.
-
Key ni jina la data na value ni thamani ya data hiyo.
-
Kati ya key na value, tumia alama ya nukta mbili (:).
Mfano:
"jina": "John Doe"
2. Key Lazima Ziwe Ndani ya Alama za Semi Mbili ("")
-
Key zote lazima ziwe ndani ya alama za funga semi mbili.
-
Thamani (value) ya aina ya maandishi (string) pia huwekwa ndani ya alama za semi mbili.
Mfano:
"jina": "John Doe",
"mji": "Mpanda"
3. JSON Huandikwa Ndani ya Mabano Makubwa ({})
-
Data yote ya JSON lazima ianze na kifungua bano kubwa { na kumalizika na kifunga bano kubwa }.
Mfano:
{
"jina": "John",
"umri": 30
}
4. Value Zinaweza Kuwa Aina Mbalimbali za Data
-
Aina za data zinazokubalika kwenye JSON ni:
-
String: Maandishi, huwekwa kwenye alama za semi mbili ("example").
-
Number: Namba kamili au zenye desimali (30, 12.5).
-
Boolean: Thamani za true au false.
-
Null: Thamani isiyo na kitu (null).
-
Array: Orodha ya thamani nyingi, huwekwa kwenye mabano ya mraba ([]).
-
Object: JSON ndani ya JSON, huwekwa kwenye mabano makubwa ({}).
Mfano:
{
"jina": "John D...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 ai web app 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Json somo la 6: Jinsi json inavyohifadhiwa kwenye database
Katika somo hili utakwend akujifunza namna ambavyo json inaweza kuhifadiwa kwenye database
Soma Zaidi...Json somo la 5: Aina za data zinazotumika kwenye json
atika somo hili utakwenda kujifunza ainza za data zinazotumika kwenye Json
Soma Zaidi...Json somo la 4: Jinsi ya ku encode na ku decode data za json
Katika somo hili utakwend akujifunz aku encode na ku decode data za json katika baadhi ya language
Soma Zaidi...Json somo la 3: Matumizi ya Json
Katika somo hili utakwend akujifunza baadhi ya matumizi ya Json
Soma Zaidi...JSON somo la 1: Maana ya json
Katika somo hili utakwend akujifunz amaana ya json, umuhimu wake na kazi zake.
Soma Zaidi...Json somo la 7: Aina za database ambazo zinafuata mtindo wa json
Kuelewa aina mbalimbali za database zinazotumia au kufuata mtindo wa JSON kwa uhifadhi wa data, faida zake, na mifano ya matumizi.
Soma Zaidi...