Historia ya Mtume Muhammad (s.a.w) somo la 1: Asili ya Waarabu

Katika somo hili utakwenda kujifunza Asili ya waarabu na kusambaa kwao katika bara arab

HISTORIA YA WATU WA MAKA KUTOKA KWA NABII IBRAHIM (A.S) 

Nabii Ibrahim (AS), pia anajulikana kama Khalilu-Llah" (خليل الله)  yaani rafiki wa Allah, anachukuliwa kuwa babu mkubwa wa Nabii Muhammad ï·º, ambaye alifuata ari ya babu yake katika kuamini na kuhubiri aina safi zaidi ya upwekeshaji wa Mwenyezi Mungu. Tarehe ya kuzaliwa kwake haijulikani ingawa kuna maoni mengi yanayotofautiana kwa kiasi kikubwa.

 

Nabii Ibrahim aliamrishwa na Allah kumleta Mke wake Hajar na mtoto wake Ismail na kumucha jangwani. Alimuacia kisi kidogo cha chakula na maji. Kiasi kile hakikudumu kwa muda mrefu kikaisa. Jangwani hapo hakukuwa na mti, wala maji. Baada ya maji kuisha Ismail akapata kiu kikali na akaanza kulia kwa kiu, ili aweze kupata maji. Mama yake akawa anakimbia kati ya vilima wiviwli  akipanda juu kuangalia kama ataona bonde lenye maji karibu. Vilima hivyo vilijulikana kama Swafa na Marwa ambapo Mpka leo vinaonekana na mahujaji wanatekeleza Ibada ya hija kwa kutembea kwenye vilima hivi.

 

Wakati huo yeye alizunguruka kati ya vilima hivyo viwili huku Ismail alinendelea kuhangaika na kiu. Basi akawa anapiga chini miguu yake. Ndipo Allah akaamrisha patoke maji chini ya miguu. Inasemekana ni Malaika Jibril alipiga pale chini kwa mbawa zake. Basi mama Ismail akarejea na kukuta kuna maji. Ndipo akaanza kuzungusia kisima hiko. Kwa kuwa kisima hiko kilikuwa na sehemu pekee inayotoa maji jangwani hapo basi kuna baadhi ya wasafiri waliokuwa wakipita hapo kibiashara wakitokea Yemen walipita na kuomba maji. Kisima hiki kimejulikana kama zamzam na sababu ya jina hili ni kuwa pale alipokuwa anajuia maji yasisambae akama anasema zam zam kwa lugha yake alimaanisha tulia tulia. Lugha hii ina asili na Africa ambapo Hajra alitokea.

 

Mama Ismail akawa anatoa huduma ya maji kwa wasafiri. Wasafiri wale wakaanza kuweka makazi na hatimaye mji mdogo ukajengeka.  Sehemu hiyo ndio Mkkah ya leo, na kisima hiko ndio kisima cha Zamzam ambacho mpaka leo kipo. Basi Ismail na Mama yake waliishi hapo, huku Nabii Ibrahim akama anakuja kuwatembelea mara kwa mara. 

 

Kisima cha Zamzam kiliendelea kuwepo kwa mamia ya miaka. Ila baadaye kilitoweka. Kutoweka kwa kisima hili kunazungumziwa nikwa sababu ya Mdhambi waliokuwa wakiyafanya watu wa kabila la Jurhum.  Pia historia inaelezwa kuwa watu hawa walifukuzwa Maka hivyo wakakifukia kisima hiki pamoja na mali zao na baadhi ya vitu vingine. Hvyo kwa miaka mingi Makkah ilikuwa haina kisima hiko. Ilifikia wakati hata watu wakasahau kabisa sehemu ambapo kisima hiko kilikuwepo. Pia kulikuwa na habari za kuzusha kuhusu yeyeto ambaye atakifukuwa kuwa anaweza kupatwa na jambo baya.

 

Mwanawe, Ismail na mama yake Haajar, walikaa katika bonde la Makkah pamoja na kabila la Yemeni, Jurhum. Ilikuwa Makkah ambapo baba na mwana walijenga Ka'bah, wakinyanyua nguzo zake kwa mujibu wa amri ya Allah na kisha wakiita watu kufanya hija. Ismail mwenyewe alikuwa na wana kumi na wawili kutoka kwa binti wa Mudad (mkuu wa kabila la Jurhum), ambao majina yao ni Nabet, Qidar, Edbael, Mebsham, Mishma', Duma, Micha, Hudud, Yetma, Yetour, Nafis na Qidman, ambao mwishowe waliunda makabila kumi na mawili yaliyokaa Makkah na kufanya biashara kati ya Yemen, Shaam, na Misri.

 

Baadaye, makabila haya yalienea kote kwenye peninsula, wakati mwingine hata nje ya mipaka yake. Kati ya makabila kumi na mawili, yote yalitoweka isipokuwa uzao wa wawili: Nabet na Qidar. Wanabatei (au wana wa Nabet) walijenga ustaarabu uliofanikiwa kaskazini mwa Hijaz, wakifanya Petra (katika siku hizi Jordan) kuwa mji mkuu wao hadi Warumi walipokuja na kushinda ufalme wao. Uzao wa Qidar, waliishi kwa muda mrefu Makkah wakiongezeka kwa idadi, hasa kupitia 'Adnan na mwanawe Ma'ad ambao Waarabu wa 'Adnani walijinasibisha kwao. 'Adnan alikuwa babu wa ishirini na moja katika mfululizo wa ukoo wa Nabii. Nizar, mwana pekee wa Ma'ad, alikuwa na wana wanne ambao walijitenga katika makabila manne makubwa; Eyad, Anmar, Rabi'a na Mudar. Makabila ya Mudar yalijitenga katika matawi mawili makubwa: Qais 'Ailan bin Mudar na tawi la Elias bin Mudar. Kati ya Elias bin Mudar walikuwa Tamim bin Murra, Hudhail bin Mudrika, Banu Asad bin Khuzaimah na tawi la Kinana bin Khuzaimah, ambao kutoka kwao walikuja Quraysh, uzao wa Fahr bin Malik bin An-Nadr bin Kinana.

 

Quraysh walijitenga katika makabila mbalimbali, maarufu zaidi walikuwa Jumah, Sahm, 'Adi, Makhzum, Tayim, Zahra na matawi matatu ya Qusai ibn Kilab: 'Abd Al Dar bin Qusai, Asad bin 'Abdul 'Uzza bin Qusai na 'Abd Manaf bin Qusai. 'Abd Manaf alijitenga katika makabila manne: 'Abd Shams, Nawfal, Muttalib na Hashim. Ni kutoka familia ya Hashim ambapo Allah alimchagua Nabii wa mwisho na Mtume, Muhammad ï·º mwana wa 'Abdullah mwana wa 'Abdul Muttalib mwana wa Hashim, rehema na amani za Allah ziwe juu yake.

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

help_outlineZoezi la Maswali

info Jaza maswali yote au baadhi kisha bofya kitufe cha kutuma majibu hapo chini.
1 Ni watu wa kabila gani la kutokea Yemen waliweka makazi yao Jngwani pale ambapo Hajra na Mwanaye walikuwepo _____?
2 Nabii Ismail alibahatika kuwa na watoto wangapi ______?
3 Quraish wanatokana na uzao wa _______?
4 Nabii Ibrahim pia anajulikana kwa jina la ______________
5 Sehemu ya Jagwani ambapo Nabii Ibrahi alimuacha mke wake na mtoto wake inajulikana hivi leo kama mji wa _____?
6 Kisima kilichotokana na maji yaliyobubujika wakati Nabii Ismail akibiga miguu yake alipohitaji maji wakati akiwa mchanga kilijulikana kama ________
7 Mke wa Nabii Ibrahim aliyemzaa Ismail aliitwa nani ___________
8 Nabii Ibrahimu na Mwanaye Ismail walijenga ________ kwa kunyanyuwa kuta zake

Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Historia ya Mtume Muhammad (s.a.w) Main: Dini File: Download PDF Views 1120

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Historia ya Mtume Muhammad ï·º somo la 26: Kusimama kwa Wahy

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu kusimama kwa Wahyi kuja kwa Mtume Muhammad ï·º

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ï·º somo la 64: Ndoa ya Mtume Muhammad baada ya Khadija

Katika somo hili utakwend akujifunz akuhusu Ndoa Mtume Muhammad baada ya Bi Khadija alimuoa Sauda kisha Aisha

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ï·º somo la 46: Historia fupi ya Al-Arqam ibn Abi al-Arqam

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuusu historia ya mmoja katika maswahaba wa mwanzoni na mwenye mchango mkubwa sana katika uislamu ambaye ni Al-Arqam ibn Abi al-Arqam

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ï·º somo la 29: Amri za kwanza alizopewa Mtume Muhammad ï·º

Katika somo hili utajifunza amri ambazo alipewa Mtume Muhammad ï·º mwanzoni kabisa mwa kazi yake ya Kulingania dini

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ï·º somo la 50: Historia ya safari ya Hijra ya kwanza kuelekea Ethiopia

Hapa tutakwend akujifunz akwa urefu zaidi kuhusu safari hii ya kwanz aya kuelekea Ethiopia inayojulkana kama Hijra ya kwanza.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ï·º somo la 43: Mateso walyoyapata waslamu

Katka somo hili utakwenda kujifunza kuhusu mateso ambayo wamepewa Waislamu ili kuachana na uislamu wao

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ï·º somo la 71: Maisha ya Mtume Madina

Hapa tunakwenda kuianza upya safari ya Maisha ya Mtume akiwa Madina

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ï·º somo la 48: Hijra ya kwanza kuelekea Ethiopia

Katika somo hiliutajifunza kuhusu Hijra ya Kwanz ana ya Pili kuelekea Ethiopia na mambo yaliyojitokeza.

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ï·º somo la 66: Mkataba wa Aqaba wa kwanza

Katika somo hili utajifunza kuhusu historia ya Mkataba wa Aqaba wa kwanza

Soma Zaidi...
Historia ya Mtume Muhammad ï·º somo la 19: Hilf al-Fudul - makataba wa haki

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu historia ya mkataba wa al-Fudhul na matokeo yake katika kusimamaia haki za wafanyabiashara.

Soma Zaidi...