BLOGGER somo la 2: Jinsi ya kuandika post na kuiboresha pamoja na kuidhibiti

Katika post hii utakwend akujifunza jinsi ya kuandika post, kuisimamia na kuoboresha.

Kama unatumia simu upande wa kushoto kuna menu hapo bofya utaletewa list ya menu. Bofya palipoandikwa NEW POST. na kama unatumia kompyuta bofya palipoandikwa NEW POST upande wa kushoto kwa juu.

 

Kama unatumia simu ukurasa utakaofunguka utakuwa tofauti na wanaotumia kompyuta. Hata hivyo nitafafanua kwa manufaa ya wote wanaotumia simu na kompyuta. Hapo chini naleta picha mbili moja kwa wanotumia simu na ingine ni kwa wanaotumia kompyuta.

 

Kwa watumiaji simu

 

Kwa watumiaji kompyuta

 

  1. Hapo kwenye namba 1 ndipo utakwenda kuandika kichwa cha habari cha hiyo post yako.
  2. Kwenye namba 2 ni kwa ajili ya ku preview yaa ni kuangalia jinsi ambavyo post yako itaonekana na wasomaji wako kabla hujaipost
  3. Kwenye namba 3 hapo ndipo utakapobofya pindi unapomaliza. Ukibofya hapo post yako inakuwa live. Hivyo watu wote wataweza kuiona.
  4. Hiyo ni menu ambapo kila unachokiona hapo kitakusaidia katika kuboresha muonekano wa post. Kwa wanaotumia siku buruza huo mstari utakuonyesha menu zaidi.
  5. Kwenye nmaba 4 hapo hutumika ku edit html code za hiyo post yako. Kama unataka kuongeza maboresho kwa kuweka code za html, css na javascript kwenye post yako, basi hapo ndio sehemu inayotumika.

 

Menu ya vifaa vya uandishi

Sasa ngoja tuone baadhi ya sehemu muhimu katika uandishi wa post yako kwenye blog.

  1. Ni kwa ajii ya kufanya herufi kuwa bold
  2. Ni kwa ajili ya kufanya maandishi kuwa italics
  3. Ni kwa ajili ya kupigia mstari maandishi
  4. Kwa ajili ya kukata maadhishi
  5. Kwa ajili ya kuweka rangi kwenye maandishi
  6. Kwa ajili ya kuweka rangi ya background
  7. Kwa ajili ya kuweka link
  8. Kwa jili ya kuweka picha
  9. Kwa ajili ya kuweka video na audio
  10. Kwa ajili ya kuweka emoj
  11. Kwa ajili ya kupangilia muonekano wa paragraph
  12. Kwa ajili ya kupangilia mtiririko wa namba
  13. Kwa ajili ya kunukuu

 

...

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: blogger Main: ICT File: Download PDF Views 1380

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

BLOGGER somo la 3: Jinsi ya kuifanya Blog yako iweze kuonekana Google kwa urahisi

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuifanya blog yako iweze kuoneka Google kwa urahisi

Soma Zaidi...
Blogger somo la 1: Jinsi ya kutengeneza Blog

Somo hili litakwenda kukufundisha hatuwa kwa hatuwa jinsi ya kufunguwa blog kwenye mtandao wa blogger.

Soma Zaidi...