MUENDELEZO WA HADITHI YA MSHONA NGUO

MUENDELEZO WA HADITHI YA MSHONA NGUO

MUENDELEZO WA HADITHI YA MSHONA NGUO



Mshona nguo akaendelea kusimulia mbele ya sultani kuwa yule muandaaji wa shughuli alipojiridhisha kuwa kinyozi alimtendea ubaya kijana, basi kinyozi ilibidi afungiwe kwenye chumba maalumu kwa uchunguzi zaidi. Mshona nguo anaendelea kusema kuwa baada ya shughuli kuisha kwa salama mimi niliondoka kuelekea nyumbani. Lakini kwa mkewangu mambo hayajakuwa sawa. Mke wangu alikuwa na wivu sana na alitaka kujuwa hasa kilichonichelewesha. Baada ya kumueleza yote akaniambia nimpeleke na yeye akafurahi, kula na kunywa. Sikuwa na jinsi nilimchukuwa mkewangu na kutafuta hoteli nzuri.


Nikiwa na mkewangu tuliendelea kula na kunywa na kufurahi pamoja hadi ilivyofika jioni. Mkewangu akachukuwa samaki mkubwa sana na ndizi kwa lengo la kwenda kupika chakula cha usiku. Nilijuwa kuwa anantaka kunikomowa maana anajuwa fika kama mimi nimeshiba sana. Niliwaza jambo lamda nitafute mtu wa kwenda naye nyumbani ili tule kwa pamoja. Katika pitapita za mitaa nikiwa na mkewangu, ndipo nikakutana na yule kijana aliyekuwa na ugomvi na kinyozi. Kijana alionekana amelewa na mwenye mawazo. Niliamuwa kumchukuwa ili nimsaidia pia nijisaidie mwenyewe maana mke wangu hatakubali nikishindwa kumaliza chakula.


Kijana alikubali na nilikwenda naye. Bahati nzuri mke wangu alionekana kumkubali kijana kwa ucheshi wake. Roho ya wivu ilianza kunijia ila sikuwa na wasi sana maana nilitambuwa kuwa ijana ataondoka kesho yake asubuhi. Tulipofika nyumbani mke wangu aliwa jikoni mimi na kijana tuliendelea kufurahi na kuzungumza mengi sana. Chakula kilivyoiva ndipo tukaanz akula kwa pamoja na kwa furaha ya hali ya juu. Na hapo ndipo tukio la mauwaji haya ulioshuhudia leo limeanzia. Kijana alikabwa na mwiba wa samaki na kupoteza maisha. Tukampleleka kwa tabibi, tabibu akampeleka kwa muuza nyama, muuza nyama akampeleka mtaani, na mtaani akakutana na mlevi. na tukio likaelezwa kwa ufasaha zaidi kama walivyosimulia wenzake waliotangulia.


Baada ya mshona nguo kumaliza masimulizi haya mfalme akatamka kuwa amewasamehe wote waliohusika na mauwaji haya. Maana tukio hili linashangaza sana. Kisha mfalme akaagiza kinyozi aletwe haraka sana. Askari wawili na mshona nguo walikwenda kwa muandaaji wa ile shughuli ya jana kwenda kumchukuwa kinyozi. Punde kinyozi akaletwa mbele ya sultani. Kinyozi hakujuwa kwa lengo gani ameletwa mbele ya sultani. Kinyozi akaelezwa mlolongo wa tukio zima na namna ambavyo anahusika. Kinyozi alishangazwa sana na tukio zima la mauwaji. Kinyozi akatoa mafuta flani kwenye kichupa akamfunua maitina kumuweka kwenye paja lake.


Loo! Loo! Hakika kijana huyu uhai wake bado upo'! watu wote walishangazwa zaidi na maneno ya kinyozi. Kinyozi akampaka mafuta yale kwenye shingo yake, na kuchukuwa mkasi mrefu, kisha akaingiza kwenye koo la kijana. Looo! Kipande cha samaki na mwiba kikatoka. Kijana akapiga chafya na alirudi kuwa mzima. Kwa hakika tukio hili liishangaza zaidi ya maelezo. Sultani akaagiza tukio zima liandikwe vyema kwenye hazina ya Sultani Harun Ar-Rashid na lijifadhiwe vyema kwa vizazi vijavyo vipate kushuhudia.


Baada ya hapo Sultani akaamuru kusamehewa kila muhusika wa tukio. Pia akamteuwa kinyozi, tabibu na mshona nguo wafanye kazi zao ikulu na kuwafanya wawe watu wa karibu naye. Kuanzia siku hiyo Alikuwa akishauriana nao mmbo kadhaa na kuwafanya ni ndugu zake wa karibu. Kijana alitunukiwa mwanamwari mtoto wa Sultani. Tukio huili lilikuwa ni la kushangaza sana.


Baada ya Sheherazade kusimulia hadithi hii kwa Sultani Shahariar, Mdogo wake Dinarzade alionekana kuipenda sana. Kumbuka miezi mingi ilishhapita toka Shehrazade kuolewa na Sultani na kwa ufundi wa masimulizi Sultani hakufikiri tena kumuuwa. Dinarzade alitaka asimuliwe hadithi nyingine. Na hapo ndipo hadithi ya Aladini ikaanza kusimuliwa usiku ule.


#NB kama utakuwa umesahau jinsi mlolongo wa masimulizi haya ulivyoenda tembelea tovuti yetu. Utakuta mlolongo mzima toka hadithi ya kwanza kitabu cha kwanza hadi hapa tulipo.


Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 107

Post zifazofanana:-

SABABU YA NENO LAKO
Sababu ya neno lako, nasema nimesikia,Sababu ya neno lako, nasema hongera pia,Sababu ya neno lako, nishajua yakonia,Wasema afukuzwae, sihadi pasemwe toka,Sababu ya neno lako, maumivu yanijia,Sababu ya neno lako, nami leo nakwambia,Sababu ya neno lako, sit Soma Zaidi...

Hadithi ya mjakazi wa Mfalme
HADITHI ILIYOSIMULIWA NA MJAKAZI WA SULTANI Mtukufu sultani, nakwenda kukusimulia tukio lililotokea leo hii wakati tulipokuwa tunaburudika. Soma Zaidi...

MUISLAMU ALIYE BORA NI YULE ANAYEWACHA MAMBO YASIYO MUHUSU
' ' ' ' ' ' ': ' ' ' ' ' ' ' ' "' ' ' ' ' '?... Soma Zaidi...

Faida za kula Nazi
Nazi ni katika matunda bora sana kiafya, Soma faida zake kwa afya yako Soma Zaidi...

HADITHI YA CHONGO WATATU WATOTO WA WAFALME
Soma Zaidi...

Kitabu cha Afya 04
Afya inaweza kuathiriwa na vitu vingi sana. Hapa tutaendelea kuona mabo zaidi yanayoathiri afya yako. Soma Zaidi...

Kwanini Uislamu umeipa Elimu nafasi ya kwanza?
Soma Zaidi...

Dawa ya kutibu maumivu ya jino
Utaijuwa Dawa ya maumivu ya jino, sababu za maumivu ya jino na njia za kujikinga na maumivu ya jino Soma Zaidi...

VOCABULARY TEXT 03
learn English Vocabulary Soma Zaidi...

Nabii Ibrahiim(a.s) Kumlingania Uislamu Baba Yake
Baada ya NabiiIbrahiim(a. Soma Zaidi...

maktaba
Soma Zaidi...

SIRI
Hapana mpaka sasa hautambui chochote kuhusu kilichotokea. Soma Zaidi...