Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ambavyo Maswahaa wa Mtume walivyokuwa na ushujaa katika kuipambania dini.
Maswahaba wa Mtume (s.a.w.) walikuwa watu waliotoa maisha yao kwa ajili ya dini ya Uislamu. Wengine waliteswa, wengine walikufa shahidi, na wengine waliongoza majeshi kwa ujasiri mkubwa. Ushujaa wao haukuwa tu katika vita, bali pia katika kusimamia haki, kuonyesha subira, na kujitoa kwa ajili ya Uislamu.
Bilal bin Rabah alikuwa mtumwa wa Makkah aliyesilimu katika siku za mwanzo za Uislamu. Alipogundulika kuwa Muislamu, aliteswa vibaya na bwana wake, Umayyah bin Khalaf. Alilazwa juani jangwani huku mwili wake ukiwekewa mawe mazito, akilazimishwa kuuacha Uislamu.
Lakini Bilal hakukata tamaa. Kila alipoteswa, alitamka kwa nguvu: "Ahad! Ahad!" (Mwenyezi Mungu ni Mmoja! Mwenyezi Mungu ni Mmoja!).
Hatimaye, Abu Bakr As-Siddiq (r.a.) alimnunua na kumweka huru. Baada ya Uislamu kushinda, Bilal akawa muadhini wa kwanza wa Uislamu, na sauti yake ilisikika ikilingania watu kwa sala katika mji wa Madinah.
📖 Dalili ya Hadithi:
Mtume (s.a.w.) alimwambia Bilal:
"Ee Bilaal Nielezee juu ya ‘amali njema kabisa unayoitenda, kwani nimesikia sauti ya viatu vyako vikiwa mbele yangu Peponi"
🔹 Funzo: Ushujaa hauko tu kwenye vita; kusimama imara katika imani hata katikati ya mateso ni aina ya ushujaa mkubwa.
Hamza alikuwa ami wa Mtume (s.a.w.) na mmoja wa wapiganaji hodari zaidi wa Kiislamu. Alisilimu baada ya kusikia kuwa Mtume (s.a.w.) ametukanwa na Abu Jahl, na tangu siku hiyo akawa mtetezi mkuu wa Uislamu.
Katika vita vya Uhud, Hamza alisimama kidete dhidi ya maadui wa Uislamu. Alikuwa mpiganaji jasiri, lakini hatimaye aliuawa kwa hila na Wahs">... Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu Umeionaje Makala hii.. ? Katika somo hili utakwenda kujifunza namna ambavyo Mswahaba walikuwa wakimpenda Mtume s.a.w zaidi ya nafsi zao Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu mmwanamke shujaa anayejulikana kwa jina la Naseebah bint Ka'ab (Nusaybah bint Ka'ab) mwanamke aliyemlinda Mtume s.a.w wakati wanaume wanakimbia vitani Huyu ni Sahaba ambaye Allah alituma jeshi la Nyuki kulinda Maiti yake, wakati makafiri walitaka kukata kichwa chake Karibu kwneye Katika historia ya Maswahaba wa Mtume Muhammad s.a.w. Katika mfululizo wa masomo haya tutakwend akunagalia mengi katika mambo yanayohusu uislamu kupitia maisha ya Maswahaba. Katika somo hili utakwend akujifunz abaadhi ya wanawake ambao wameshiriki vita vya uhudi na kutoa mchango mkubwa. Wanawake hawa wapo wengi ila hapa nitakuletea wanne tu. Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu historia ya swahaba anayeitwa Khabbab bin Al-Aratt (r.a.) Katika makala hii utakwend akujifunz anamna gani maswahaba walishiriki katika michezo mbali mbali na jinsi ilivyoweza kuwasaidia katika harakati za dini. Katika somo hili utajifunza sifa nyingine ya unyenyekevu ambayo walikuwa nayo Maswahaba wa Mtume (s.a.w) Katika somo hili utakwend akujifunza ujasiri wa maswahaba mbalimbali katika kulinda jamii ya kiislamu katika vita vya Ahzab Katika somo hili utakwend akujifunza namna illivyokuwa Imani Isiyoyumba ya Maswahaba
help_outlineZoezi la Maswali
Tarehe: 1970-01-01 03:33:45
Topic: Historia ya Maswahaba
Main: Dini
File: Download PDF
Views 436
👉1
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉2
Madrasa kiganjani
👉3
kitabu cha Simulizi
👉4
Bongolite - Game zone - Play free game
👉5
Kitabu cha Afya
👉6
Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Historia ya Maswahaba somo la 5: Mapenzi ya Maswahaba kwa Mtume
Historia ya Maswahaba somo la 8: Mjuwe Naseebah bint Ka'ab (Nusaybah bint Ka'ab) mwanamke shujaa
Historia ya Masahaba Ep 11: Asim bin Thabit – Mmoja wa Mashujaa wa Kiislamu
Historia ya Maswahaba somo la 01: Nani ni Maswahaba
Historia ya Maswahaba somo la 9: Baadhi ya Wanawake 4 walioshiriki vita vya Uhdi
Historia ya Maswahaba somo la 6: Historia ya Khabbab bin Al-Aratt (r.a.)
Historia ya Masahaba Ep 10: Michezo waliokuwa wakicheza Masahaba
Historia ya Maswahaba somo la 4: Unyenyekevu wa Maswahaba
Historia ya maswahaba somo la 7: Maswahaba katika Historia ya vita vya handani - vita vya ahzab
Historia ya Maswahaba somo la 3: Imani Isiyoyumba ya Maswahaba