Hadithi ya kinyozi mwenyewe

Hadithi ya kinyozi mwenyewe

HADITHI YA KINYOZI YEYE MWENYEWE



Mimi si mtu wa maneno mengi kama kijana anavyonidhania. Hata hivyo nipo tofauti sana na kaka zangu kwani mimi ndiye mtoto wa mwisho.. nitakusimulieni kisa kimoja hapa ndipo mtagundua kuwa mimi si mtu wa maneno mengi. Siku moja nilipokuwa sina kitu cha kukila na kwa kuwa mimi si mtu wa maneno mengi sikuweza kwenda kukopa. Niliweza kusikia wepesi wa tumbo langu kwa njaa, hata nikathubutu kufunga kipande cha kanga tumboni. Sikujuwa ni kwa nini siku ile nilikuwa na njaa sana. Niliamini huenda ikawa ni majaribu yamenifikia. Mingurumo ya tumbo ilizidi kusumbua.


Basi katika pirika zangu nikakutana na vijana 10 wapo kwenye dau. Kwa mawazo yangu nikadhani wanakwenda kusherehekea. Na hii ilikuwa ni kawaida kwa vijana wakikusanyika eneo hili wanakwenda upande wa pili wa mto kufurahia na kula na kunywa. Mawazo ya njaa yalikuja karibu zaidi hata ikawa chakula kama kipo mbele yangu. Nikaanza kupata harufu ya paja la kuku lililokaangwa na kukaushwa vyema. Chapati za mayai zilizofunika samaki vyema. Harufu ya juisi nikaanza kuipata kwa mbaali wakati nakodolea macho paja la kuku.


Kwa njaa zangu na pupa ndipo nikakimbilia bilauri ya juisi na kuanguka. Loo! Nimevunja bilauri ya watu. Ghafla nikashituka kutoka kwenye dimbwi la mawazo. Nikawahi kwenye dau na mimi kuingia. Bila hata ya kuuliza zaidi kilichowakuta na wapi wanakwenda. Kwa kuwa mimi si mtu wa maneno mengi sikuweza kuuliza sana. Nahodha akang'oa dau na kuanza kutokomea mtoni. Nilianza kushangaa kumbe vijana wote 10 waliomo mule wamefungwa minyororo, na walikuwa chini ya uangalizi wa askari. Kwa kuwa mimi si mtu wa maneno mengi niliendelea kuwa kimya.


Tulipofika ng'ambu ya pili ya mto tulipokelewa na kundi kubwa la askari na kupelekwa kwa kadhi. Sikuzungumza kitu na wala sikujitetea kwa lolote. Ni kwa sababu mimi si mtu wa maneno mengi. Tulipofika kwa kadhi wale mabwana kumbe walikuwa na kosa na mauwaji na hivyo kadhi akaamuriu vijana wote 10 wakatwe vichwa vyao mara moja. Kwa kuwa mimi si mtu wa maneno mengi niliendelea kukaa kimya none hatma ya uwepo wangu pale. Basi askari akawachukuwa wote vijana 10 na kwenda kukata vichwa vyao.


Baada ya muda kidogo askari akaja mbele ya kadhi na kutamka kuwa kazi imekwisha, yaani ameshakata vichwa vyao. Kadhi akamuuliza mbona umechukuwa 9 na huyu wa 10 umemuacha hapa. Askari akajibu hapana mkuu nimechukuwa wote 10. kadhi hakuamini hata akaenda kuhesabu vichwa. Loo! Ni kweli vichwa vilikamilika 10. hapa kadhi akawa na furushi la maswali kichwani mwake. Furushi lote akataka kunitundika mimi. Kwa kuwa mimi si mtu wa maneno mengi niliendelea kunyamaza. Kadhi akaja akiwa amefura kw ahasira na mawazo.


Alipokaa vyema akaagiza aletewe maji kwenye chombo. Kadha alipoletewa maji alikuywa na kutawadha. Alifanya hivi ili kupunguza hasira, ili asijefanya maamuzi yasiyo ya haki. Kisha kadhi akaniuliza haya wewe ni nanai na imekuwaje akuajumlishwa kwenye kundi hili la watu wabaya? Basi sasa sina budi nikaanza kumueleza Kadhi namna nilivyofika pale. Kadhi alishangaa sana kuona vile hivyo akanieleza kuwa ni kwa nini hukuzungumza toka mwanzo. Nikamueleza kuwa mimi si mtu wa maneno mengi. Nikaendelea 'usidhani kuwa mimi ni mtu wa maneno mengi, mimi ni tofauti sana na kaka zangu.


Kwani kaka yangu wa kwanza ni kichaa na ameupata ukichaa kutokana na yaliyomkuta na maneno mengi yake. Ili uamini kuwa mimi si mtu wa maneno mengi, nitakuhadithia yaliyowapata kaka zangu wote kutokana na maneno yao mengi. Baada ya kuzungumza hivi kinyozi akaanza kuhadithia yaliyotokea kwa kaka wake wa kwanza:


Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 95

Post zifazofanana:-

tarekh 01
NASABA YA MTUME (S. Soma Zaidi...

Historia ya Luqman mtu aliyesifika kuwa na Hikma
Luqman ni katika watu wema kabisa waliopita zama za nyuma. Soma Zaidi...

Hadithi Ya 38: Anayeonyesha Uadui Kwa Rafiki Yangu Mtiifu Ninatangaza Vita Dhidi Yake
Soma Zaidi...

uran na sayansi
3; Mchujo wa maji dhaliliKatika aya nyingine tunakuja kupata funzo kuwa maji aliyoumbiwa mwanadamu licha yakuwa na sifa zilizotajwa katika kurasa zilizopita ila pia maji haya yanasifa kuwa ni madhalilina pia na yamechujwa kama tunavyoelezwa katika quran?? Soma Zaidi...

FAIDA ZA VITAMINI C NA UMUHIMU WA VITAMINI C MWILINI
Utafahamu faida za vitamini C mwilini pamoja na kujuwa umuhimu wa vitamini C Soma Zaidi...

Kwa nini hakuna haja ya Mtume mwingine baada ya Muhammad
Na tukiutafiti Uislamu kwa makini kama mfumo kamili wa maisha tunaona unadhihiri ukweli wa aya hii ya Qur-an. Soma Zaidi...

Watu wa Mji Waliomuua Muislamu kwa Kuwa Amewasadikisha Wajumbe wa Allah(s.w)
Katika Suratul Yassin Allah(s. Soma Zaidi...

Sababu na Chanzo cha vidonda vya tumbo
Zijuwe sababu za kutokea kwa vidonda vya tumbo. Sababu kuu za vidonda vya tumbo hizi hapa Soma Zaidi...

Chemsha bongo namba 15
24. Soma Zaidi...

Nimemaliza heddhi mwezi huu lkni najihisi tena dalili zakublidi wiki nzima hii kwann?
Soma Zaidi...

mafunzo ya TAJWID na imani ya dini ya kiislamu
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII SALEHE
Soma Zaidi...