Menu



Viatu vya ajabu

VIATU VYA AJABU VYAONDOKA NA MKONO WANGU Aliponieleza sifa za viatu anavyotaka nikamsogelea kwa ukaribu na kumkazia macho kama nataka kumpiga vile kisha nikamuuliza “wewe ni nani, na ni nani amekutuma, vina nini hasa viatu hivi” alibakia kimya ...

Viatu vya ajabu

VIATU VYA AJABU VYAONDOKA NA MKONO WANGU
Aliponieleza sifa za viatu anavyotaka nikamsogelea kwa ukaribu na kumkazia macho kama nataka kumpiga vile kisha nikamuuliza “wewe ni nani, na ni nani amekutuma, vina nini hasa viatu hivi” alibakia kimya kwa muda kidogo kisha aksema “baba anakutafuta, anakuhitaji uende nyumbani”. nikamuahidi kuwa nitakwenda siku ya ijumaa. Basi akaniahidi kuwa atakuja na ndugu yake kesho kuja kunielekeza nyumbani kwao.



Kesho yake nikaandaa pale ndani chumba kingine kitupu. Nikaweka vyakula na vinywaji. Alipokuj tukaendelea kuburudika na wageni wangu watatu wenzie wamefunika sura zao. Mmoja kati yao alitoka nje, kisha baada ya muda akarudi. Basi kumbe alikwenda chukuwa dawa bila ya sisi kujuwa akiweka kwenye kinywaji na tukalewa, na kuja kuamka ni usiku na nilipowasha taa nikakuta pembeni yangu kuna kichwa cha yule binti wa siku zote aliyetaka viatu. Sikuweza kuwaona wenzie wawili.



Nilishituka sana kuona binti amekufia kwangu, nikafunga duka na kuchimba shimo uwani nikamfanyia maiti yake maandalizi yote na kumzika kwa siri. Usiku huohuo niliondoka na kurudi misri. Nikawa kila baada ya miezi 6 nalipa pesa ya ada ya kile chumba. Nilikaa misri kwa muda wa miaka mitatu hata nikajiridhisha kuwa huwenda mpaka sasa wakawa wamesahau kilichotokea. Nikaamuwa kurudi tena Yemeni ili nikamalize kazi yangu ya kuwatafuta wale watu. Pia kukutana na yule mzee aliyenitafutaga.



Nilifika Yemeniwakati wa usiku, nikaingia dukani kwangu na kuanza kusafisha, alama za michirizi ya damu zilikuwa zikionekana. Nilisafisha, sasa nilipokuwa naamsha viti ndipo nikaokota pete. Pete ilikuwa na picha ya kichwa cha mamba kwa juu. Picha ya kichwa cha kunguru na kambale kwa upande wa pembeni kulia na ushoto. Nikaamuwa kuiuza pete ile nipate pesa za kuanzia maisha. Nikaenda kwa sonara wa kwanza akasema hanunui pete ila maana ni ya thamani sana.



Nikaenda kwa sonara mwengine akaniambia nisubiri. Akaondoka kidogo na kwenda alikokwenda kisha akarudi. Akanieleza kuwa hawezi kununua. Kume aipotoka alikwenda kutoa taarifa kuwa pete iliyoibiwa imeonekana. Usiku askari wakanifamia na kunibambikia kesi ya wizi vinginevyo nitaje jinsi nilivyoipata pete ile. Mbele ya kadhi nilishindwa kueleza ukweli nikiamini kuwa nikieleza ukweli ndio nitauliwa. Nikamueleza niliiba kwa binti mmoja.



Baada ya hapo kadhi akanipa hukumu ya kukatwa mkono wangu. Nilishukuru kukatwa mkono ili kunusuru kichwa changu. Walinikata mkono, nilipata maumivu makali sana, damu ilitoka na nikapoteza fahamu. Nilipokuja kushituka nikajikuta nipo kwenye kitanda. Nilijiuguza pale kwa muda wa siku tatu. Siku ya nne akaja mzee mmoja mrefu mwenye sura ya heshima. Kwa kumuangalia utajuwa kuwa ni mchamungu, pia ni tajiri. Akaniambia “mwanangu, najua hii pete hukuiiba, naelewa fika hii pete haiwezi kuibiwa, hivyo basi nieleze historia yako na hadi likatokea hili la kutokea”. nikaanza kumueleza mpaka mwisho, kuanzia wageni wa baba, hata nikafika Yemeni na haliyotokea.



Nilipomaliza kusimulia yule mzee alikuwa akitokwa na machozi kisha akaema kwa hakika umesema vyema kwa hakika hukudanganya. Nilitambua historia yako hata kabla hujaitaja. Nilitaka kuthibitisha ukweli wa maneno yale, yaliyonenwa na wageni wale, yapata miaka 10 iliyopita. Mwananfu kuwa na amani hapa ulipofika ni kwenu, na jihisi upo kwa baba yako. Natambua yaliyomkuta baba yako, mwanangu na wewe. Nitakueleza kuanzia tafsiri ya waliyoyatenda wageni wale kwenu, na maswali mlioyashindwa kuyajuwa kuhusu wageni wale.


Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Aliflela2 Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 797


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani     👉5 kitabu cha Simulizi     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zifazofanana:-

BINTI MZURI ASIYETAMBULIKA
BINTI HUYU NI NANI? Soma Zaidi...

HADITHI YA MLEVI
Soma Zaidi...

Kwanini dirisha moja?
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...

Hadithi ya Kaka wa kwanza wa kinyozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Hadithi ya Kinyozi kaka wa kwanza
Soma Zaidi...

Muendelezo wa hadithi ya mshona nguo
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Wagen wa Ajabu
UJIO WA WAGENI WA BARAKA. Soma Zaidi...

Hadithi ya Kaka wa sita wa kinyozi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Hadithi ya kinyozi
Soma Zaidi...

Harusi ya aladini na binti sultani
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...