Makataba wa hudaibiya: sababu zake, vipengele vyake, na faida za mkataba wa hudaibiya

Makataba wa hudaibiya: sababu zake, vipengele vyake, na faida za mkataba wa hudaibiya

Makataba wa hudaibiya: sababu zake, vipengele vyake, na faida za mkataba wa hudaibiya

Mkataba wa Hudaibiya

- Ni mkataba wa amani baina ya waislamu na Maquraish wa Makkah, mwaka wa 6 A.H, Dhul-Qa’adah (Machi, 628 A.D) katika kitongoji cha Hudaybiyah karibu na
Mji wa Makkah.

- Mkataba ulitiwa saini na Mtume (s.a.w) kwa niaba ya waislamu na Suhail bin Amri
Kwa niaba ya Makafiri wa Kiquraish.



Yaliyopelekea kutokea kwa Mkataba wa Hudaybiyah.
- ilikuwa Mtume (s.a.w) kutimiza ndoto (wahay) aliyoota mwaka 6 A.H. kuwa kuna siku atafanya ‘Umrah’.

- Mtume (s.a.w) akiwa na waislamu 1,400 walikwenda kufanya ibada ya ‘Umrah’ lakini walizuiliwa na Maquraish katika kitongoji cha Hudaibiyah wasiingie Makkah.

- Mtume (s.a.w) alituma wajumbe 2, mmoja baada ya mwingine ili kuwaomba Maquraish wawaruhusu waingie Makkah, lakini walikataliwa.

- Mtume (s.a.w) alituma mjumbe wa 3, ‘Uthman bin Affan’ (r.a) aliyeshikiliwa na Maquraish kwa muda, na kuja tetesi kuwa ameuawa.

- Mtume (s.a.w) aliwakusanya waumini chini ya mti na kuchukua kiapo cha utii (Bai’at) juu ya kulipiza kisasi cha ‘Uthman bin Affan’ (r.a), lakini baadaye alirejea.
Rejea Qur’an (48:18).



- Maquraish kwa kuwaogopa waislamu, walimuomba Mtume (s.a.w) kuweka mkataba wa amani na Mtume (s.a.w) alikubali, na ukaitwa “Mkataba wa Hudaybiyah”.
Rejea Qur’an (48:1).



Vipengele vya Mkataba wa Hudaybiyah.
1.Waislamu warudi Madinah bila kufanya ‘Umrah’.
2.Waislamu wanaweza kurudi mwakani (7 A.H) kufanya ‘Umrah’ lakini wakae siku tatu.
3.Wakija Makkah wasije na silaha ila panga zikiwa ndani yah ala zao.
4.Waislamu hawataenda nao Madinah waislamu wanaoishi Makkah na wala hawatamzuia yeyote miongoni mwao anayetaka kubakia Makkah.
5.Kama yeyote wa Makkah atatoroka kwenda kusilimu, Waislamu hawana budi kumrudisha (wasimpokee), lakini yeyote kutoka Madinah akitoroka kwenda Makkah kuritadi, Maquraish hawatapaswa kumrudisha Madinah (watampokea).
6.Makabila ya Waarabu yatakuwa huru kufanya Itifaki (urafiki) na upande wowote ule yanaoupendelea.
7.Pasiwe na vita kwa kipindi cha miaka 10 baina ya waislamu na Maquraish na baina ya waitifaki (Allies) wa Waislamu na waitifaki wa Maquraish.
8.Hapana ruhusa ya kutengua hata sharti moja katika hizi kabla ya miaka 10 kupita.



Mafunzo yatokanayo na Mkataba wa Hudaybiyah.
1.Ahadi ya Mwenyezi Mungu (s.w) siku zote ni ya kweli na yenye kutimia, kama alivyotimiza ahadi kwa Mtume (s.a.w) alipoota kuwa siku 1 atakwenda ‘Umra’.
">...

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Main: ICT File: Download PDF Views 3370

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Ni nini maana ya ilham?

Ni mtiririko wa habari au ujumbe unaomjia mwanaadamu bila ya kufundishwa na mtu yeyote au kuona mfano wake katika mazingira yoyote.

Soma Zaidi...