Vifaa saba na herufi saba katika usomaji wa quran


image


Ni zipi hizo herufi saba, na ni vipi viraa saba katika usomaji wa Quran


Viraa saba na herufi saba.
Wataalamu wa tajwid wanaeleza kuhusu herufi saba za usomaji wa qurani. Itambulike kuwa qurani imeshuka kwa lugha ya kiarabu. Na pia itambulike kuwa waarabu wenyewe walitofautiana katika lahaja za lugha ya kiarabu. Lahaja hizi zilikuwa katika makabila saba ya kiarabu yaliyopo maka. Yaani ni kuwa waarabu walikuwa na makabila saba wakati ule. Na makabila haya ijapokuwa yalizungumza kiarabu lakini walikuwa wakitofautiana katika maneno, utamkaji na hata uandishi. Hivyo lahaja hizi zilijulikana kama herufi saba (za usomaji wa qurani).



Hivyo lahaja saba hizi ndizo chanzo za hizi herufi saba. Na hili linathibitika katika maneno ya Mtume (s.a.w) aliposema: ((Jibriyl alinisomea kwa herufi moja, nikaifanyia marudio mpaka akanifundisha nyingine, nikaendelea kumuomba nyinginezo mpaka mwishowe zikawa herufi (lahaja) saba)) (Bukhari na Ahmad).



Makabila haya yalikuwa Quraysh, Hudhayl, Thaqiyf, Hawaazin, Kinaanah, Tamiym na Yeman. Hivyo qurani ilishuka katika lahaja saba kulingana na makabila. Hivyo ikawa kila kabila linasoma qurani kwa namna ambavyo lahaja yao inawafanya waelewe. Wakawa watu wanaandika qurani kwa namna ambavyo wanaelewa wao. Kulingana na lahaja ya kabila lao. Hali hii ilifanya usomaji wa qurani utofautiaane. Mifano; “’alayhim” wengineo walitamka “’alayhimuw”, neno la “swiraatw” walitamka wengineo “zwiraatw” na wengine “siraatw”, “muumin” wengineo walitamka “muwmin” 



Amesimulia ‘Umar Ibn Al-khatab kuwa: “Nilimsikia Hishaam ibn Hakiym akisoma Suwratul-Furqaan tofuati na vile ninavyoisoma na alivyonifundisha Mtume ( لى لله عليه وسلم B). Nilikaribia kumsimamisha (asiswalishe) lakini nikamvumilia mpaka akamaliza kisha nikamshika nguo yake shingoni na kumvuta mpaka kwa Mtume لى لله عليه وسلم) B) nikasema: “Nimesikia huyu mtu akisoma (Suwratul- Furqaan) kinyume na ulivyonifundisha”. Mtume ( لى لله عليه وسلم B) akasema: ((Mwachie!)) Akamwambia (Hishaam): ((Soma)). Akasoma. Akasema ((Hivi ndivyo ilivyoteremshwa)). Kisha akaniambia mimi: ((Soma)). Nikasoma. Akasema: ((Hivi ndivyo ilivyoteremshwa. Hakika Qur-aan imeteremshwa kwa herufi saba, hivyo someni iliyokuwa sahali kwenu)



Uislamu ulipoenea zaidi ikawepo haja ya kuiandika qurani katika lahaja moja ambayo itasomwa. Na hii ni kutokana na kuwepo makosa katika usomaji wa qurani. Hivyo katika utawala Kikundi cha Maswahaba, kilichoongozwa na Hudhayfah bin al-Yamaaniy ambaye alikuwa Iraq, kilikuja kwa ‘Uthmaan ( رضي لله عنه ) na wakamsihi "auokoe ummah wa Kiislamu kabla haujatofautiana juu ya Quraan." ‘Uthmaan ( رضي لله عنه ) akaamrisha chini ya uongozi wa Zayd bin Thaabit رضي لله عنه) ) nakala za Qur-aan ziandikwe na nakala zote zisizo rasmi zichomwe moto.

 

Lahaja iliyotumika kuandika Qur-aan ni ile ya ki-Quraysh na Msahafu ukajulikana kuwa ni ‘Msahafu wa ‘Uthmaan’. Nakala hizo zilisambazwa miji mikuu ya Waislamu zikiwa kama nuskhah (kopi) rasmi. Na nuskhah ya asili ikabakishwa kwa Mama wa Waumini Hafswah ( رضي لله عنها ). Alimwacha Zayd bin Thaabit Madiynah, ‘Abdullaah bin Swaa’ib alitumwa Makkah,Mughiyrah bin Shu’bah alitumwa Syria, Abu ‘Abdir-Rahmaan As-Sulamy alitumwa Kuwfah, ‘Aamir bin ‘Abdil-Qays alitumwa Baswrah. (www.al-hidaayah.com)



Baada ya msahafu huu kusambazwa katika dola ya kiislamu lahaja zote ambazo siorasmi zilipotea. Msahafu huu ndio chimbuko la misahafu tulionayo leo. Ijapokuwa kuna tofauti kubwa za kiuandishi kati ya misahafu ya leo na msahafu huu. Kwa m fano msahafu huu haukuwa na dot kwenye herufi za dot au irabu pia hazikuwepo. Hayo yato yalifanyika baadaye kadiri uislamu ulipoenea maeneo mbalimbali ya dunia na ikaonekana ugumu wa kutumia msahafu ule kwa watu wasiokuwa waarabu.


Viraa saba.
Viraa hivi saba ndivyo ambavyo vimetokana na lahaja ya kikurayshi ambayo ndio msahafu wa ‘Uthmani umeandikiwa. Viraa hivi wataalamu wa elimu ya tajwid wamevizungumzia katika vitabu vya elimu hii.



Sponsored Posts


  👉    1 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       👉    2 Madrasa kiganjani offline       👉    3 Jifunze Fiqh       👉    4 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Aina za usomaji wa Quran
Je kuna aina ngapi zabusomaji wa Quran Soma Zaidi...

image Aina za Madd far-iy
Mada zipo katika makundi mawili ambayo ni madda far-iy na mdada twab-iy. Soma Zaidi...

image Fadhila za kusoma Quran na umuhimu wa kusoma Quran
Unazijua faida za kusoma Quran, na je ni faida gani utapata ukisoma Quran? Soma Zaidi...

image Sababu za kushuka surat al Quraysh
Qurayh ni jina la kabila la Mtume Muhammad S.A.W. Sura hii itakwenda kukujulisha neema ambazo Maquraysh wamepewa na hawataoewa wao wowote baada ya wao. Soma Zaidi...

image Fadhila za kusoma surat al Baqarah
Surat al Baqarah ni katika sura ambazo tunapaswa tuwe tunasoma mara kwa mara. Post hii itakufundisha kuhusu fadhila za sura hii. Soma Zaidi...

image Sababu za kushuka kwa surat al qariah
Surat Al qariah, ni moja katika sura zilizochuka miaka ya mwanzoni mwa utume. Soma Zaidi...

image Aasbab Nuzul surat Ash sharh: sababu za kushuka alam nashrah (surat Ash sharh)
Makala hii itakwenda kukufundisha sababu za kushuka kwa alam nasharah yaani Surat Ash sharh. Soma Zaidi...

image hukumu za kujifunza tajwid
Kujifunza tajwid ni katika mambo muhimu wakati wa kusoma Quran Soma Zaidi...

image Sababu za kushuka Surat al Kafirun
Sura hii imekuja kukata rai ya Makafiri wa Makka kuhusu ibada ya ushirika. Hivi leo tungesema kuhusu dini mseto. Soma Zaidi...

image Faida za kujuwa Quran tajwid
Hapa nitakufindisha faida za kusoma quran kwa Tajwid. Soma Zaidi...