PYTHON - somo la 8: method za namba zinazotumika kwenye python


image



Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu number method yaani function zinazofanya kazi kwenye namba.



Matendo ya hesabu

Katika mahedabu Kuna matendo makuu manne ambayo ni:-

Kujumlisha

Kutoa

Kuzidisha

Kugawanya

 

 

Kujumlisha

Kama ilivyo kwa lugha nyinginezo hata katika python unapojumlisha utatumia alama ya +. Unaweza kujumlisha variable kwa variable ambazo zinawakikisha namba

Mfano:

a = 5;

b=6;

print(a+b)

Hii itakupa jibu 11;

 

 

 

Pia unaweza kujumlisha kweli list

a = [2,4,6,7]

print(a[2] + a[1])

 

 

Hii itatupa jibu 10 kwa kuwa index ya 2 ni 6 na index ya 1 ni 4. Hivyo ni sawa na kusema 6+4.

 

 

Pia unaweza kujumlisha namba hasi na chanya chanya na kupata matokeo yaleyale. 

Mfano: print(-6 + 2) hii itatupa jibu 4

 

 

Kutoa 

Kama tulivyoona hapo juu kuhusu kujumlisha basi na kutoa kunafuata kanuni zilezile tunatumia alama ya - Ili kutoa.

Mfano:

a = [2,4,6,7]

print(a[2] - a[1])

Hii itatupa jibu 2

 

 

Mfano

print(9-5)

Hii itatupa jibu 4

 

 

Kuzidisha

Katika kuzidisha tutatumia * 

print(6*3)

Hii itakupa jibu 18

a = [2,4,6,7]

print(a[2] * a[1])

Hii itatupa jibu 24

 

 

Kugawanya

Katika kugawanya tutatumia /

Mfano:

print(10/2)

Hii itatupa jibu 5

a = [2,4,6,7]

print(a[2] / a[0])

Hii itatupa jibu 3.0

 

 

 

 

Tuingie ndani zaidi

Sasa tunakwenda kuingia ndani zaidi kwenye somo hili. Kuna case nitakuletea hapo chini:-

case 1:

print(10/3)

Hii itatupa jibu 3.3333333333333335

 Utaona hapo imegawanya na kutuletea fesimali nyingi sana, baada ya kibaki. Sasa tutakwenda kutatuwa changamoto hii kwa namna mbili.

Kukadiria viwango vya desimali

Sasa tunataka hapo juu tukadirie viwango kadhaa vya desimali. Kufanya hivyo tutatumia round() function.

 

 

Function hii itakuwa na argument 2 ambazo ni namba husika na digit ambazo unataka zitokee kwenye viwango vya desimali. Namba na digit vitatenganishwa na alama ya koma (,)

 

 

Mfano tunahitaji kupata viwango viwili tu vya desimali.

namba = 10/3

print(round(namba, 2))

Hii itatupa jibu 3.33 utaona hapo tumepata viwango viwili tu vya desimali

 

 

Kuandika kiasi kilichobaki

Tofauti na kupata mrundikano wa namba za desimali, unaweza pia kuandika kiasi likichobaki TU. Katika mfano wetu hapo juu namba 10 ukiigawa kwa namba 3 itabaki Moja.

 

 

Kufanya hivi tutatumia function ya divmod() function hii itakuwa na argument 2 ambazo ni namba inayogawanywa na namba inayogawanya.

 

 

Na katika majibu itakuja hivyo hivyo namba ya kwanza itaonesha jibu na namba ya pili itaonyesha kilichobaki.

 

 

print(divmod(10,3))

Hii itatupa jibu (3,1) yaani jibu ni 3 na itabaki 1.

 

 

Case 2:

Tunahitaji kuandika zile namba zenye power yaani video na vipeuo. Mfano tunataka kupata majibu ya 2 kipeo Cha 3 yaani 2*2*2. Hii katika Hali ya kawaida huandikwa 23

 

 

Hapo 2 ndio huitwa base na hiyo 3 huitwa power. Katika python tunaweza kutekeleza hayo kwa kutumia pow() ambayo itakuwa na argument 2. Ya kwanza ni base na ya pili ni power.

 

 

print(pow(2,3))

Hii itakupa jibu 8

 

 

case 3:

Wakati mwingine unahitaji watu waingine namba kwa mfano unahitaji mtu ajaze umri wake. Sasa Kuna watu wanawezs kujaza -21 baada ya kuandika 21. Sasa hihesabu hizo ni namba mbili tofauti kabisa.

 

 

Kutatuwa tatizo Hilo utahitajikankubapa absolute namba, yaani namba halisi. Katika python function tutakayoitumia ni adb() ambayo itabeba argument Moja nayo ni hiyo namba.

pr

int(abs(-21))

Hii itatupa jibu 21.

 

 

Mwisho:

Somo linalofuata tutakwenda kujifunza zaidi kuhusu method nyinginezo.



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Imeandikwa na Rajabu Terehe 2023-10-21 Download PDF Share on facebook WhatsApp

RELATED POSTS

picha

Katika soo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kubaduli aina moja
picha

Katika somo hili utajifunza kuhusu maana ya python na kazi
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza syntaxy za python yaani sheria
picha

Katika somo hili utakwenda kujfnza kuhusu string method nyinginezo. Katika
picha

Katika somo hili tunakwenda kujifunza aina nyingine za data ambazo
picha

Katika somo hili utajifunza jisni ya kujuwa aina ya data
picha

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu string indexing. Kama tulivyojifunza
picha

Katika somo hili utajifunza maana ya variable, na sheria za
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza aina za data ambazo hutumika
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu operator. Hasa hapa tutakwend