PYTHON - somo la 3: Jinsi ya kuandika variable kwenye python


image



Katika somo hili utajifunza maana ya variable, na sheria za kutengeneza variable kwenye python. Pia utajifunza maneno ambayo hayafai kutumiwa kama variable



Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya variable na jinsi ya kuandika variable.

Variable tunaweza sema ni kitu ambacho kinabeba thamani ya kitu fulani, ama huwakilisha kitu fulani. Kwa mfano unaposena x  ni sawa na 7 hapo hiyo x ni variable na hiyo saba ni thamani.

 

Jinai ya kuandika variable na  kuipa  thamani (value).

  1. Kwanza utaandka jina la variable yako. Mfano jina

  2. Kisha itafuata alama ya sawasawa (=) alama hii kazi yake ni ku declare varibale yaani kuipa thamani varibale

  3. Kisha ndipo utaandika hiyo thamani ya variable yako. Mfano “juma” kumaanisha kuwa variable jina ilioajw aapo kipengene a, thamani yake ni juma. Kwenye python variable hiiitaonakena hivi jina = "juma"

 

 

 

Angalia mfano huu:

jina_la_kwanza = "juma"

jinalapili = "saidi"

umri = 34

print(jina_la_kwanza)

print(jinalapili)

print(umri) 

 

 

Variable hizi zitakupa matokeo haya:-

 

 

 

Sifa za variable kwenye python:

  1. Kwanza haitakiwi kuanza na special character kama @, #, $, %, ? na nyinginezo. Mfano #jina = ali hii sio sawa. Usawa wake ni jina =” ali”

  2. Unaweza kutumia underscore (_) mwanzoni mwa varibale badala ya kuanza na namba mfano _2023 

  3. Pili variable haitakiwi kuanza na namba. Mfan 2023 = “mwaka” hii sio sawa. Usawa wake iwe _2023

  4. Zingati herufi yaani neno “Jina” na neno “jina” haya ni maneno mawili tofauti mfanoVariable hizi ni mbili tofauti jina = "juma" ; JinA = "juma"

  5. Vyema kama variable yako ina maneno zaidi ya moja nganisha kwa kutumia underscore yaani (_) mfano jina_la_baba

  6. Ikiwa thamani ya variable ni neno ama maneneo ama herufi au alama basi zungushia kwa (“)  au kwa (‘) b mfano jina = “bongoclass” au jina = ‘tarzan’

  7. Endao variable ni namba basi hautaweka hizo alama za kuninuu. Endapo utaziweka hiyo variable yako haitahesabika kuwa ni namba. 

Mfano:

mwaka = 2023

print(mwaka)

 

Hiyo itakupa matokeo ya 2023

8. Unaweza ku update thamani ya variable baada ya kui declare kwa kutumia thamni mpya. 

jina = "bongoclass"

jina = "Tanzania"

print(jina)

 

Code hizo zitakupa matokeo Tanzania na sio bongoclass kwa sababu variable umebadilishwa baada ya kui declare kwa mara nyingine kwa thamani toauti

 

9. Unaweza kuunganisha variable zaidi ya moja kwa kutumia alama ya jumlisha (+) hii hujulikana kama concatnation

Mfano:

mafunzo = "python"

darasa = "bongoclass"

gharama = "bure"

print("Jifunze" + mafunzo + "kutoka"+darasa + "kwa gharama ya "+gharama)

 

 

Hii itakupa matokeo

 

  1. Pia unaweza kufanya mahesabu kwa kutumia variable. Angalia mfano huu

a = 5

b = 6

print(a *b)

 

Hi itakupa jibu la 30

 

10. MANENO HAYA HAYATAKIWI KUTUMIKA KWENYE VARIABLE:

False    def    if    raise

None    del    import    return

True    elif    in    try

and    else    is    while

as    except    lambda    with

assert    finally    nonlocal    yield

break    for    not

class    form    or

continue    global    pass

 

 

 

Mwisho:

Katika somo linalofuata tutakwenda kujifunza aina za data kwenye python. Katika somo hilo tutakwenda kufanyia kazi somo hili la variable kwa vitendo hatuwa kwa hatuwa.



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Imeandikwa na Rajabu Terehe 2023-10-20 Download PDF Share on facebook WhatsApp

RELATED POSTS

picha

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu string indexing. Kama tulivyojifunza
picha

Katika somo hili utajifunza jisni ya kujuwa aina ya data
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu number method yaani function
picha

Katika somo hili utajifunza kuhusu maana ya python na kazi
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza syntaxy za python yaani sheria
picha

Katika somo hili utakwenda kujfnza kuhusu string method nyinginezo. Katika
picha

Katika somo hili tunakwenda kujifunza aina nyingine za data ambazo
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza aina za data ambazo hutumika
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu operator. Hasa hapa tutakwend
picha

Katika soo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kubaduli aina moja