PYTHON - somo la 1: Jinsi ya ku install python


image



Katika somo hili utajifunza kuhusu maana ya python na kazi zake. pia jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya somo.



Python ni moja katika lugha za kikompyuta zilizo maarufu. Ilianzishwa mwaka 1991 na Guido van Rossum. Python ni moja katika high level programming language ambayo ni general programming language yaani inatumika kwenye field nyingi.

 

Python imekuwa ikifanyiwa marekebisho mengi toka ilipoanzishwa na sasa tupo katika toleo la 3 yaani python 3. Katika course hii tutakwenda kutumia toleo la 3 la python.

 

Matumizi ya python

  1. Hutumika kwenye kutengeneza website, web app na blog kama sever side langage. Yaani ku wasiliana na server .
  2. Hutumiaka kwenye kutengeneza software mbalimbali kama game
  3. Hutumika kufanya mahesabau kama kwenye takwimu.
  4. Pia huweza kutumika kuwa kama system scripting.

 

Python file extension:

Kama ilivyo kuwa language zote zina extension kama ilivyo hatml ni .html, php ni .php, basi na python ni .py. Mfano main.py

 

Maandalizi kwa ajili ya course hii:

 

Kwa watumiaji wa kompyuta:

Course zinazopatikana bongoclass zinalenga wanafunzi wa aina zote. Kwa wale wanaotumia kompyuta na wale waotumia simu janja. Sasa kwa wale wanaotumia kompyuta fuata maelekezo haya:-

  1. Kwanza install python. Njia rahisi ya kuistall python ni kuwa na python IDE. Ninapendelea utumie pytharm kutoka jetbrain. IDE hii ni rahisi kutumia na haihitaji configuration nyingine. Fuata link hii  https://www.jetbrains.com/pycharm/download/download-thanks.html?platform=windows&code=PCC
  2. Baada ya ku download install hiyo software. Hakikisha una internet ili kwamba kama itahitaji ongezeko la tools iweze ku download. Hata hivyo software hii ni ya offline
  3. Baada ya kumaliza ku install, bofya icon yake ili kuifunguwa. Hapo utakutana na ukurasa huu.

 

Hapo bofya palipoandika New Project.kisha utakuja ukurasa mwingine ambao ni huu

 

Kama ndio mara yako ya kwanza hapo usiset kitu chochote zaidi ya jina la project yako tu. hapo mwanzoni kabisha kuna palipoandikwa pythonProject 

Badili jina la project yako kutoka pythonProject kuwa jina unalotaka wewe. Kwa mfano mimi nitasema pythonMafunzo 

Baada ya hapo bofya create kwa chini upande wa kulia. Itaanza kuload ili kuandaa mazngira ya hiyo project yako. Baada ya kumaliza utakutana na ukurasa mkubwa ambao ndio uwanja wa kuanzika code zako.

 

Kwa upande wa kushoto kuna project root. Ambapo kuna faili linaonekana limefungka kwa upande wa kulia na kuna code utaziona. Faili hilo linaita main.py hilo ndio faili la kwanza la project yako.

 

Sasa fanuya hivi. Kwenye huo ukurasa uliofunguka upande wa kulia futa kila kitu kisha weka code hizi:

print("haloo bongoclass")

 

Baada ya hapo run hizo code kwa kubofya kialama cha ku play kilicho upande wa kulia kwa juu

 

Angalia kwa chini kuna ukurasa umefunguka. Ukurasa huo utaochesha vitu vitatu:-

  1. Location ya hilo faili
  2. Matokeo ya hizo code
  3. Uwepo wa error

 

Hiyo namba 1 inaonyesha hilo faili linapatikana wapi kwenye kompyuta yako. Hiyo namba 2 ndio matokeo ya code zetu. Kwa mfano hapo utaona haloo bongoclass hayo ni matokeo ya code ambayo tumeandika hapo juu. Ha hiyo namba tatu utaona kuwa code 0 kumaanisa kuwa hakuna tatizo. Kama umefiika hapo basi kompyuta yako ipo tayari kuendelea ku code python.

 

Location ya project yako:

Ili kujuwa mahali ilipo  project yako utakwenda kwenye local disc c, kisha user kisha jina la user wa kompyuta yako, kisha shuka mpaka chini utakuta folder limeandika pycharmProject. Hapo ndipo project yako utaikuta.

 

Kwa watumiaji wa kompyuta somo letu limeishia hapa. Tkutane somo la pili ambapo tutakwenda kuzungumzsia sheria za kuandika code ya python.

 

Kwa watumiaji wa simu:

  1. Ingia play store kisha tafuta app inayoitwa Python 3 - IDE for Python 3 kama inavyoonekana kwenye picha hapo chini. App hii ukisha install haihitaji ulazima wa kuwa na internet. Pia ina uwezo wa ku install extensions

 

  1. Baada ya hapo utaifungauwa. Kuna setting utatakiwa kuzifanya. Angalia picha hizo hapo chini.

 

 

 

 

  1. Baada ya kumaliza hizo setting utakuja ukurasa wa kuandika. Hapo andika code hizi print(“haloo bongoclass”) baada ya hapo utabofya kialama cha ku play kipo kwa chini upande wa kulia. Angalia picha hapo chini.

 

Baada ya kubofya alama hiyo utapata matokeo ya code zako kama inavyoonekana hapo chini. Utaona hapo neno haloo bongoclass na chini yake kuna maneno yanasomeka kama program finished. Angalia hizo picha hapo chini.

 

Sasa ni wakati wa ku save faili letu. Angalia kwa juu kuna icon ya folda bofya hiyo. Kisha bofya save . utafunguka ukurasa wa kuchaguwa wapi u save, wewe cjhaguwa hapo mwanzo kama inavyoonekana kwenye picha. Program itatengeneza folder lake na utaona maandishi chini yanasema use this folder bofya hapo. Utatakiwa ku ruhusu app iweze ku access mafaili kwenye simu yako. Itakubidi uruhusu hapo.


 

 

 

 

 

Baada ya kumaliza hatuwa hiyo utarudishwa tena kwenye app yako kwa ajili ya ku save jina la faili lako. Futa jina lililokuwepo kisha weka main.py. Hiyo main ndio jina la faili na .py ndio extension ya faili kama ilivyo .php, au .html au .css.


 

 

 

LOCATION YA PROJECT YAKO:

Kama unataka sasa kulona fplder lenye project yako, nenda kwenye file maneger kisha ingia kwenye document. Hapo utakutana na folder la python 3 ukifunguwa ndani ya folder hilo utakutana na faili lako la main.py.

 

 

 

 

Kama umefika hatuwa hiyo basi simu yako ipo tayari kuendelea na masomo yanayofuata. Tukutane somo la pili tutakwenda kuzungumzia sheria ya kuandika code za python.

 

 



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Imeandikwa na Rajabu Terehe 2023-10-20 Download PDF Share on facebook WhatsApp

RELATED POSTS

picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu operator. Hasa hapa tutakwend
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza syntaxy za python yaani sheria
picha

Katika somo hili tunakwenda kujifunza aina nyingine za data ambazo
picha

Katika somo hili utajifunza maana ya variable, na sheria za
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu number method yaani function
picha

Katika somo hili utakwenda kujfnza kuhusu string method nyinginezo. Katika
picha

Katika somo hili utajifunza jisni ya kujuwa aina ya data
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza aina za data ambazo hutumika
picha

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu string indexing. Kama tulivyojifunza
picha

Katika soo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kubaduli aina moja