Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika constant kwenye PHP. Pia utajifunza utofauti wake na variable
PHP COSTANTS
Constant ni jina linalowakilisha thamani fulani. Thamani hi haiwezi kubadilika wakti wa code kufanya kazi. Constant inaweza kuanzwa kwa herufi lakini si kwa alama ya dola $ kama ilivyo kwenye variable.
Jinsi ya kuweka constant kwenye php.
Utaanza kuweka neno define likifuatiwa na mabano mfano define() ndani ya mabano utaweka jina la constant na thamani vyote vinatakiwa viwekwe kwenye funga semi.
Mfano:-
define("tunda", "Tunda ni zao la mti linalopatikana baada ya uwa");
echo tunda;
?>
Hii itakupa matokeo:
Tunda ni zao la mti linalopatikana baada ya uwa
Constant hutumika katika kuweka data ambazo hazitakiwi kubadilika wakati wa kuchakata code. Kwa mfano password na database connection.
KUTUMIA CONSTANT KWENYE PHP FUNCTION
Unaweza kutumia constant kwenye code zako zote yaani constant moja unaweza kuitumia katika code zako bila kujali ipo wapi. Kwa urahisi ni sawa na kusema unaweza kutumia constant hata kwenye function ama kwingineko.
Mfano:-
define("salamu", "halo hujambo");
function mfano() {
echo salamu;
}
mfano();
?>
Hii itakupa matokeo
Halo hujambo
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Imeandikwa na Rajabu Terehe 2023-10-18 Download PDF Share on facebook WhatsApp