PHP - somo la 29: Jinsi ya kaundika function kwenye php


image



Katika somo hili utakwenda kujifundisha kuhus matumizi ya function kwenye php. Pia utajifunza jinsi ya kuandika function



PHP FUNCTIONS:

Function ni kikundi cha code ambazo huweza kutumika kwa zaidi ya mara moja. Function zipo katika aina mbi ambazo ni:-

Zile ambazo zimekuja moja kwa moja katika php yenyewe hizi huitwa built in functions

Zile ambazo unaweza kuzitengeneza wewe mwenyewe. Hizi huitwa user defined functions

 

Sifa za Functions:

Huweza kutumika zaidi ya mara moja

Haiload kila page inapoload

Hutumika pale tu itakapoitwa

 

USER DEFINED FUNCTIONS:

Sasa hebu tuone jinsi ya kutengeneza function yako mwenyewe. Ili uweze kufanya hivi itahitajika kutumia kanuni ifuatayo:-

function jina() {

   //weka code hapa

}

 

Jinsi ya kuandika function yako:

Kwanza anza na neno keyword function likifuatiwa na jina la hiyo function. Kwa mfano tunataka function ya kujumlisha namba mbili. Hivyo tutaipa jina la jumlisha. Kwahyo itakuwa kama hivi: function jumlisha kisha utaweka mabano haya (). Pia jina la function halitakiwi lianze na namba au special character. Kama ile ya dola tulioitumia kwenye variable.Baada ya hapo utaweka mabano haya {} ambapo ndani yake ndipo kutakuwa na code za hiyo function.

 

Mfano 1

Function jumlisha(){

Code zinakaa hapa.

}

 

Hebu sasa tuone mfano halisi wa function ya kujumlisha namba mbili:

Mfano 2:

<?php

function jumlisha() {

   $a = 4;

   $b = 5;

   $c = $a + $b;

   echo "$c";

}

?>

Hapo tumeshatengeneza function kwa ajili ya kujumlisha namba mbili. Sasa endappo uta load huo ukurasa hautaonyesha chochote, ni kwa sababu function haionyeshi kitu mpaka iitwe. Ili kuiita hiyo function unatakiwa urudie kuliandika jina lake likifuatiwa na mabano (). Mfano katika code hapo juu utaandakia jumlisha () hapo utakuwa umeiita function na itakupa majibu. Hivyo basi code nzima itakuwa:-

<?php

function jumlisha() {

   $a = 4;

   $b = 5;

   $c = $a + $b;

   echo "$c";

}

jumlisha()

?>

 

 

Jinsi ya kutatua matatizo kwa kutumia PHP function

Chukulia mfano unaandika program ya kuorodhesha majina ya wanafunzi kwa jinsia zao. Sasa una jinsia mbili ya kike na ya kiume. Sasa baada ya kila inapotaja jina la mwanafunzi uandike na jinsia yake. Kwa kutumia function hatutakuwa na haja ya kutaja jinsia kila wakati.

 

Mfano: 3

<?php

function mv() {

   echo "Mvulana <br>";

}

 

function ms() {

   echo "Msichana <br>";

}

 

echo "Juma " . "jinsia ";  mv() ; echo "<br>";

echo "Aisha " . "jinsia ";  ms() ; echo "<br>";

echo "Baraka " . "jinsia ";  mv() ; echo "<br>";

echo "Neema" . "jinsia ";  ms() ; echo "<br>";

echo "Joharia" . "jinsia ";  ms() ; echo "<br>"

?>

 

 

Function inaweza kuwa ni reference (kumbukumbu)

Mfano unataka test vitu vingi kwa kutumia kitu kimoja. Hicho kimoja ambacho kitatestiwa kitakuwa ndio reference. Mfano tunataka kujumlisha namba kadhaa na namba moja. Hivyo tofauti na kuiandika hiyo namba kila wakati tunapotest basi tutaifanya kuwa reference.

 

Mfano 4:

<?php

function saba(&$kumbukumbu) {

   $kumbukumbu += 7;

}

 

$x = 3;

saba($x);

echo $x;

 

echo "<br>";

$b = 6;

saba($b);

echo $b;

?>

 

 

Function pia hutumia return statement ili kurudisha thamani fulani. Return keyword hutumika ili kusitisha function kuenelea kufanya kazi. Hii kwanza itasitisha function kisha italeta majibu kutokana na expression iliyowekwa.

 

Mfano 5:

<?php

function Zidisha($a,  $b) {

   $c = $a * $b;

   return $c;

}

 

echo  zidisha(5, 4) . "<br>";

?>

 

 

PHP function pia hubeba argument (parameter)

Hizi hutumika kama variable. Baada ya kurudia kuandika neno fulani unalifanya kuwa argument kwenye function na kupata thani yake moja kwa moja. Kwa mfano watoto wa Daudi.Baada ya kumuandika daudi kila baada ya kumuandika mtoto. Utatumia function

 

Mfano 6:

<?php

function jina($baba, $mwaka) {

   echo "$baba Daudi. Amezaliwa mwaka $mwaka <br>";

}

 

jina("Saidi", "2003");

jina("Steven", "2008");

jina("Juma", "2009");

?>

 

Somo linalofuata tutaangalia baadhi ya function ambazo ni built in. Yaani zimetengenezwa moja kwa moja toka kwa waundaji wa PHP. Somo lijalo litakuwa rahisi endapo utakuwa umeshapitia somo la function katika php level 1.

 



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Imeandikwa na Rajabu Terehe 2023-10-18 Download PDF Share on facebook WhatsApp

RELATED POSTS

picha

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutengeneza system ambayo mta
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza aina kuu 3 za variable
picha

Katika somo hili utajifunza kuhusu syntax za PHP
picha

Katika somo hili utakwendakujifunza concept ya namespaces na jinsi inavyosaidi
picha

Hapa utajifunza jinsi ya kutengeneza table ambayo tutaitumia kwenye blog
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ktumia baadhi ya
picha

Katika somo hili utajifunza kupangilia data wakati wa kuzisoma kwenye
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu class inheritance kwenye object
picha

Katika somo hili utajifunza jinsi ya ku connect database, kwa
picha

Katika somo hili utajwenda kujifunza jinsi ya kuzuia hacking kwenye
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza concept mpya ya abstract class
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku update na
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za loop DO,
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function za
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza concept ya interface na concept
picha

Katika somo hili unakwenda kujifunza jinsi y kutengeneza database na