PHP somo la 19: Jinsi ya kudhibiti mpangilio wa data baada ya kuzisoma


image



Katika somo hili utajifunza kupangilia data wakati wa kuzisoma kwenye database kw akutumia PHP



Kabla ya kuendelea na somo kuna kitu kwanza nahitaji ukijuwe. Ni kuwa data za kwenye database unaweza kuzisoma kwenye HTML paragraph na table ama kwenye dag za kuorodhesga na namna ingine unayoitaka. Sasa hapa nataka nikufundishe kutengeneza kajitable kadogo kwa ajili ya kuwekea data zetu.

Tumia code hizi kutengeneza table ya HTML kwa ajili ya kuwekea data zetu. Tafadhali rejea mafunzo ya HTML Angalia video hii

<style>

   table, th, td {

       border: 1px solid black;

   }

</style>

<table style="width:100%">

   <tr>

       <th>id</th>

       <th>Name</th>

       <th>Description</th>

       <th>Price</th>

   </tr>

   <tr>

       <td></td>

 

   </tr>

</table>

 

Baada ya hapo sasatutakwenda kuzisoma data zetu kwenye hii table. Hivyo unatakiwa utumie SELECT kwa ajili ya kusoma database. Rejea somo lililotangulia.Kwa ,ujibu wa somo lililotangulia code nzima tunayoitumia kusoma database kwenye html ni hizi 

<?php

$sql = mysqli_query($conn, "SELECT * FROM `menu` ");

       while($fetch = mysqli_fetch_array($sql)){

       ?>

Kisha katika kila tagi hii <td> ndani yake kutakwenda kuziweka data zetu kwa kutumia echo au print. Itambulike kuwa <th> maana yake ni table head na <td> maana yake ni table data. Hivyo <th> ni kwa ajili ya title au heading za kila column, na <td> ni kwa ajili ya kuwekea hizo data. rejea mafunzo ya html level 2). Ili kutumia echo kuweka hizo data kwenye <td> kwa mujibu wa somo lililoangulia tunatumia code hizi:-

<?php echo $fetch['x']; ?> hapo kwenye x unaweza kuweka jina la column, kama id, au name au price au description. Kwa ufupi <td> itasomeka hivi 

<tr>

       <td><?php echo $fetch['id']; ?></td>

       <td><?php echo $fetch['name']; ?></td>

       <td><?php echo $fetch['description']; ?></td>

       <td><?php echo $fetch['price']; ?></td>

   </tr>

 

Kama utafuata maelekezo vizuri code nzima zitakuwa hivi:-

<?php

$servername = "localhost";

$username = "root";

$password = "";

$dbname = "hotel";

$conn = mysqli_connect($servername, $username, $password, $dbname);

?>

<style>

   table, th, td {

       border: 1px solid black;

   }

</style>

<table style="width:100%">

   <tr>

       <th>id</th>

       <th>Name</th>

       <th>Description</th>

       <th>price</th>

   </tr>

 

<?php

$sql = mysqli_query($conn, "SELECT * FROM `menu` ");

       while($fetch = mysqli_fetch_array($sql)){

       ?>

   <tr>

       <td><?php echo $fetch['id']; ?></td>

       <td><?php echo $fetch['name']; ?></td>

       <td><?php echo $fetch['description']; ?></td>

       <td><?php echo $fetch['price']; ?></td>

   </tr>

</ta<?php }?>ble>

 

Hizi zitakupa matokeo haya:-

Sasa kama umeshafika hatuwa hii hapa ndipo tutaanza na somo letu. Tytakwenda kubadili mpangilio wa hizi data kwa kutumia PHP na WHERE na ORDER  kwenye SQL. Jambo la kuangalia hapa ni kubadili SQL za kwenye kuselect, maeneo yaliyobaki ni sawa.

 

MATUMIZI YA ORDER

1.Kuzipanga kwa kuzingatia alphabeti (kutoka A kwenda Z)

SELECT * FROM `menu` order by name asc

 

2. Kuzipanga kwa kuzingatia alphabet (kutoka Z kwenda A)

SELECT * FROM `menu` order by name desc

 

3. Kuzipanga kulingana na price kutoka ndogo kwenda kubwa

SELECT * FROM `menu` order by price asc

 

4. Kuzipanga kulingana na price kutoka kubwa kwenda ndogo

SELECT * FROM `menu` order by price desc

 

5. Kuzipanga kwa mvurugiko yaani random

SELECT * FROM `menu` order by rand()

 

6. kupanga idadi maalumu ya taarifa unazotaka kuzionyesha mfano unataka kuona idadi maalumutu. Tuseme unataka kuona menu 3 tu hapa tutatumia limit 3. (Rejea mafunzo ya database)

SELECT * FROM `menu` limit 3

 

7. Kuina tatu za mwisho tu

SELECT * FROM `menu` order by id desc limit 3

 

MATUMIZI YA WHERE

1. Tunataka kuona menu ambazo price yake ni zaidi ya 3000

SELECT * FROM `menu` where price > 2000

 

2. kutaka kuona data kulingana na prie kati ya 1300 mpaka 2400

SELECT * FROM `menu` where price between 1200 and 2400

 

3. kutaka kuona data ambazo id yake ni ndogo kuliko 3 

SELECT * FROM `menu` where id <3

 

Unaweza kuendelea na mifano mingi zaidi ya hiyo. Tafadhali rejea mafunzo ya database somo la 8,9 na 10. Utaweza kujifunza kuchanganya order by na where. 

 

Tukutane somo linalofuata tutajifunza namna ya Kuedit na kufuta data kwenye database kwa kutumia PHP.

 



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Imeandikwa na Rajabu Terehe 2023-10-18 Download PDF Share on facebook WhatsApp

RELATED POSTS

picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kazi na matumizi ya construct
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku upload mafaili
picha

Katika somo hili uatakwenda kujifunza jinsi ya kutumia htaccess ili
picha

Katika somo hili utajifunza jinsi ya ku connect database, kwa
picha

Katika post hii utajifunza jinsi ya kupata taarifa muhimu za
picha

Katika somo hili utakwend kujifunza kuhusu static property na jnsi
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya PHP na jinsi
picha

katika post hii utajifunza jinsi ya kutengeneza ukurasa wa dashboard
picha

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kukusanya taarifa ambazo watu
picha

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kufanya sanitization kwenye user
picha

katika somo hili utajifunza jinsi ya ku upload multiple file
picha

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutuma email kwa kutumia
picha

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuingiza data kwenye dtabase
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kufanya encryption na
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ktumia baadhi ya
picha

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kufuta table ya databse