DART somo la 3: Aina za Data


image



Katika somo hili utakwenda kujifunza aina za data zinazotumika kwenye Dart.



Dart ni kama lugha nyinginezo za kompyuta, karibia aina za data zinazotumuka kwenye dart ni sawa katika language nyinginezo. Aina hizo za data ni :-

  1. Namba
  2. String
  3. Boolean
  4. Lists
  5. Map
  6. Runes

 

  1. Namba ni aina za data ambazo ni namba tu. 

Namaba zinaweza kuwa ni int yaani namba nzima ama double yaani namba zenye desimali.

void main(){

 print(2);

 print(1.5);

}

  1. String

Hizi ni data zilizo katika mfumo wa mchanganyiko wa herufi, namba, na alama za uandishi. String huandikwa ndani ya alama za funga na fungua semi mbili (“) ama moja (). Jambo la kuzingatia ni kuwa utakayoa anza nayo ndio umalizie nayo. Yaani ukitumia (“) mwanzo basi na mwisho utumie (“)

void main(){

 print("bongoclass");

 print('info@example.com');

 print("#@?");

}

Pia unaweza kuunganisha string zaidi ya moja yaani kufanya concatnation. Kuna njia 3 ambazo hutumika kuunganisa string zaidi ya moja. Njia hizo ni kama

  1. Kwa kutumia alama ya kujumlisha +
  2. Kwa kutenganisha string mbili kwa kuacha nafasi kati yao
  3. Kwa kutumia interpolation yaani unaunganisha string na variable.

void main(){

 //concatnation kwa kutumia +

 print("karibu "+"Bongoclass");

 //kwa kucha nafasi kati ya string mbili

 print('karibu ' 'Bongoclass');

 //kufanya interpolation

 //x ni variable. Tutajifunza zaidi kwenye somo lijalo

 var x = 'bongoclass';

 print('karibu ${x}');

}

Kwenye string unaweza ku break line kwa kutumia back slash () ikifuatiwa na herufi n hii ni sawa na matumizi ya <br> kwenye html

 

void main(){

print(' karibu bongoclass upate kujifunza');

}

Kuna changamoto nyingine angalia mfano huu

void main(){

print("mama anauza ng'ombe");

}

Hapa utaona hakuna error. Ila sasa wacha tutumia single quotation mark (‘)

void main(){

print('mama anauza ng'ombe');

}

Hapo kwenye neno ng’ombe hiyo alama ya apostroph (‘) haiwezi kuendana na hizo funga semi. Hivyo kutatua tatizo hilo tutatumia back slash ().

void main(){

print('mama anauza ng'ombe');

}

 

 

3. List

Hizi ni data zilizo katika orodha ya vitu vingi. List huandikwa kwenye mabano [ ]. Tunaweza kuitumia kila data iliyo ndani ya list kivyake kwa kutumia indexing. Tutakuja kujifunza zaidi kuhusu undexing.

void main(){

print([1,2,3,4,5]);

print(['bongoclass', 'google', 'facebook']);

 

var x = ['Tanzania', 'Kenya', 'Uganda'];

print(x);

print(x[1]);

}

 

4. Boolean

Hizi ni data zenye majibu mawili tu yaani True na False. Ni sawa na kusema On na off.

Mfano 2 ni kubwa kuliko 1 hivyo jibu ni kweli.

void main(){

print(2 >1);

}

 

5. Map

Data hizi zinafanana kidogo na list. Tofauti ni kuwa zenyewe zipo kama na pea kuna key na value. Ila key haitakiwi kufanana na nyingine. Data hizi zinakuwa kwenye mabano haya {} tofauti na list ambazo zilitumia mabani haya ().

 

Ili uweze kuandika map utaanz ana mabano {} kisha utaweka key ya hiyodata. Kama ni string itakaa ndani ya zile alama za finga na funguwa semi. Kisha itafuatiwa na nukta pacha (:) kisha utaandika value yaani thamani ya hiyo data. Kutenganisha itemmoja na nyingine utatumia alama ya koma (,)

 

Unapotaka kuitumia item yeyote kwenye list tutatumia key yake. Kwa mfano angalia jinsi nilivyo display jina la juma kmwey mfano hapo chini.

void main(){

print({'jina':'Bongoclass','umri':6, "status":'live' });

 

var x = {'jina': 'juma', 'umri': 35, 'uraia': 'Tanzania'};

print(x['jina']);

}

 

6. Runes

Hii hutumika pale unapotaka ku display symbol kwa mfano zile emoj. Hapa tutatumia alama ya back slash.

void main(){

 print('u2665');

 print('u{1f600}');

}

Jinsi ya kujuwa aina ya data iliyotumika

Kufanya hivi tutatumia runtimeType Angalia mfano hapo chini.

void main() {

 print(2.runtimeType);

 print("haloo".runtimeType);

 print(2.9.runtimeType);

 print(true.runtimeType);

 print([2,'tatu', 4].runtimeType);

 print({'jina':'bongoclass'}.runtimeType);

}

 

Mwisho

Tukutane somo linalofuata titakwenda kujifunza kuhusu variable.

 



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Imeandikwa na Rajabu Terehe 2023-11-18 Download PDF Share on facebook WhatsApp

RELATED POSTS

picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu function kwenye dart, jisni
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu operator kwenye Dart, kazi
picha

Katika somo hili utajifunza kuhusu dart library. Pia tutakwend aktengeneza
picha

Katika somo hili tutakwenda kuzungumzia kuhusu parameter kwenye Dart function.
picha

Katika somo hili tutakwenda kujifunz ajinsi ya kutumia library ya
picha

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu method ambazo hutumika kwenye
picha

Katika somo hili utakwenda kujfunza kuhusu String method zinazotumika kwenye
picha

Katika somo lililopita tumejifunza kuhusu sintaksia za dart. Katika somo
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu kazi za dart language.
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu namna ambavyo program inaweza
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza method yhinginge zinazofanya kazi kwenye
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia constatnt kwenye
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kusoma na kuandika
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu break na continue kwenye
picha

Jinsi ya kuchukuwa user input kwenye Dart kwa ajili ya
picha

Katika somo hili utakwenda kuziona method za dart zinazotumika kwenye