DART somo la 2: syntax za dart


image



Katika somo hili tutatkwenda kuziona baadhi ya xyntax yaani kanunu za uandishi wa code za dart.



Somo letu litakwenda kuanzia kwenye program ya kwanza kabisa ya Hello World copi code hapo chini kisa zi pest kwenye dart editor inayotumia kisha bofya batani ya ku excute code ama ku run code. 

Void main(){

 print('Hello World');

}

 

Kama uta run code hizo utapata majibu haya Hello World

 

Sasa somo letu linaanzia hapa. 

  1. File extension

File extension ya dart ni .dart.

 

  1. Mwanzo wa program

Dart inatumia mfumo kama baadhi ya programming lnaguage nyingine kama java. Kwamba mwanzo wa program ni kwenye function ya main(). Hapa ndipo panapoanziwa program ya dart. Kwa kuwa function yetu hai return data ndio maana hapo mwanzo kumeanza na meno void kama linavyosomeka hapo void main(){}. Hata hivyo unaweza kuondoa neno void  na bado program yetu ika run vyema.

 

Ukiangalia vyema hao utaona kuna mabano {} baada ya neno main(). Ipo hivi neno main ni jina la function na ndani ya badno () hapo kutakaa parameter nyingine zo za function na ndani ya mabano {} kutakaa code abazo zinatakiwa zifanye kazi endapo program ita run.

 

Utaona hapo ndani ya mabano ya {} kuna code zinasomeka print('Hello World');

Hizi ni code ambazo zitatakiwa kufanya kazi wakati program yetu ina run. Sasa hapo kuna function nyingine ya print(). Hii ni kwa ajili ya ku print text kwenye screen. Wacha nikupe mfano mwingine.

 

main(){

 print(3 + 6);

}

 

Hapo umeona tumetumia mahesabu sasa tume jumlisha 3 na 6. Pia tumeondoa neno void. Katika mifano yetu hiyo miwili neno print, main, void hufahamika kama keyword.

 

  1. Matumizi ya semicolon (;)

Dart hutumia semicolon ili kutenganisha statement moja na nyingine. Kama ilivyo kwenye lugha nyingine. Angalia mfano huu

main(){

 print('Karibu Bongoclass')

}

 

Hapo uki run hizo code utapata error kwa sababu hakuna semicolon kwenye function ya print. Ilitakiwa iwe print('Karibu Bongoclass');

Hivyo basi ni muhimu kuzingatia matumizi ya semicolon kwenye Dart kama ilivyo kwenye lugha nyingine.

 

  1. Kuacha nafasi wazi:

Dart haiangalii mistari ilioachwa wazi. Unaweza kuruka nafasi kadiri unavyotaka hakuna tatizo. Program yenyewe itakwenda kuangalia code na sio nafasi. Dart inazingatia bnafasi moja tu ili kuppisha keyword na keyword nyingine. Kwa mfano hapo kama hutaacha nafasi kutoka kwenye neno void na neno main program yako itakuwa na shida 

voidmain(){

print('Karibu Bongoclass');

}

Hiyo program hapo haiwezi ku run kwa kuwa ina matatizo.

 

  1. comment

Ili kuweka comment dart inatumia alama ya backslash mbili yaani (//) kwa ajili ya comment ya mstari mmoja. Na kama comment yako ni paragraph yaani mistari zaidi ya mmoja utatumia  /*   */.

 

Comment hutumuka kuweka kumbukumbu kwenye code ama kutoa maelekezo kwa watakaokuja kutumia hizo code. Comment hazihusiki kwenye kufanya program ifanye kazi. Comment hazitokei kwenye screen.

 

Mfano wa comment za single line

//mwanzo wa program

void main(){

//print text kwenye screen

print('Karibu Bongoclass');

}

 

Mfano wa comment za mistari zaidi ya mmoja

//mwanzo wa program

void main(){

/*huu ni mfano wa

comment ambazo zina mistari

zaidi ya mmoja

 */

print('Karibu Bongoclass');

}

Pia kuan aina nyingine za comment ambazo hutumia ///. Hizi utumika kwenye kufanya documentation ya program. Mara nyingi hizi hutumika kama unatengeneza kibrary.

 

7. Case sensitivity

Dart ni case sensitivity kwa maana kuwa husingatia matumizi ya herufi ndogo na kubwa. Kwa mfano neno Print  na neno print  ni tofauti. Kwa sababu hilo la kwanza limeanzwa na herufi kubwa na hilo la pili ni ndogo. 

 

Mfano

void main(){

 Print('Karibu Bongoclass');

}

Hizo code hapa zitakupa error kwa sababu nimetumoia P badala ya p

 

Mwisho

Katika somo linalofuata tutakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza variable na kuziwekea value zake.

 



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Imeandikwa na Rajabu Terehe 2023-11-16 Download PDF Share on facebook WhatsApp

ZOEZI

Jaza maswali yote ama baadhi kisha bofya kitufe za kutuma majibu hapo chini.



1 : Dart huzingatia matumizi ya herufi kubwa na ndogo. hali hii hutambulika kama ________





2 : Neno void a main hufahamika kama dart ______





3 : Code hizi zina tatizo print('Karibu Bongoclass') marekebisho yake ni ________





4 : main() na print() hizi ni ________





5 : Mwanzo wa program ya Dart ni ________





6 : Moja katika njia zifuatazo haitumiki kuweka comment kwenye Dart __________





7 : umegundua kosa gani kwenye hii code hapa voidmain(){ print('Karibu Bongoclass'); }





8 : ni ipi extension format ya Dart







RELATED POSTS

picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu kazi za dart language.
picha

Katika somo hili tutakwenda kuzungumzia kuhusu parameter kwenye Dart function.
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu namna ambavyo program inaweza
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu set data type pamoja
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu operator kwenye Dart, kazi
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu switch case na jinsi
picha

Katika somo hili tutakwenda kujifunza kuhusu method ambazo hutumika kwenye
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza aina za data zinazotumika kwenye
picha

Katika somo hili tutakwenda kuingia ndani zaidi kwenye somo la
picha

Katika somo hili utakwenda kujfunza kuhusu String method zinazotumika kwenye
picha

Katika somo hili tutakwenda kujifunz ajinsi ya kutumia library ya
picha

Katika soo hili utakwenda kujifunza kuhusu reserved keywords katika Dart
picha

Jinsi ya kuchukuwa user input kwenye Dart kwa ajili ya
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu function kwenye dart, jisni
picha

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kusoma na kuandika
picha

Katika somo hili utakwend akujifunza kuhusu while loop na do