Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

38.Surat Swaad


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. S'ad, Naapa kwa Qur'ani yenye mawaidha. 1

image
2. Lakini walio kufuru wamo katika majivuno na upinzani 2

image
3. Mataifa mangapi tumeyaangamiza kabla yao, na wakapiga kelele, lakini wakati wa kuokoka ulikwisha pita. image
4. Na walistaajabu kuwajia mwonyaji anaye tokana nao wenyewe, na makafiri wakasema: Huyu ni mchawi, mwongo. 4

image
5. Amewafanya miungu wote kuwa ni Mungu Mmoja tu? Hakika hili ni jambo la ajabu. 5

image
6. Na wakaondoka wakubwa wao wakiwaambia: Nendeni zenu na dumuni na miungu yenu, kwani hili ni jambo lililo pangwa. 6

image
7. Sisi hatukusikia haya katika mila hii ya mwisho. Haya si chochote ila ni uzushi tu. 7

image
8. Ati yeye tu ndiye aliye teremshiwa mawaidha peke yake katika sisi? Lakini hao wana shaka na mawaidha yangu, bali hawajaionja adhabu yangu. 8

image
9. Au wanazo wao khazina za rehema za Mola wako Mlezi, Mwenye nguvu, Mpaji? 9

image
10. Au wao wana ufalme wa mbingu na ardhi na viliomo kati yao? Basi nawazipande njia za kwendea huko! 10

image
11. Hao ni askari watao shindwa miongoni mwa makundi yatayo shindwa. 11

image
12. Walikanusha kabla yao kaumu ya Nuhu, na kina A'adi na Firauni mwenye majengo. 12

image
13. Na Thamud na kaumu Lut'i na watu wa Machakani. Hayo ndiyo makundi. 13

image
14. Hao wote waliwakadhibisha Mitume; basi wakastahiki adhabu yangu. 14

image
15. Na hawa hawangojei ila ukelele mmoja tu usio na muda. 15

image
16. Na wao husema: Mola wetu Mlezi! Tuletee upesi sehemu yetu ya adhabu kabla ya Siku ya Hisabu. 16

image
17. Subiri kwa hayo wayasemayo, na umkumbuke mja wetu Daudi, mwenye nguvu. Hakika yeye alikuwa mwingi wa kutubia. 17

image
18. Hakika tuliidhalilisha milima pamoja naye ikisabihi jioni na asubuhi pamoja naye. 18

image
19. Na pia ndege walio kusanywa makundi kwa makundi; wote walikuwa wanyenyekevu kwake. 19

image
20. Na tukautia nguvu ufalme wake, na tukampa hikima, na kukata hukumu. 20

image
21. Na je! Imekufikia khabari ya wagombanao walipo pindukia ukuta kuingia chumbani? 21

image
22. Walipo muingilia Daudi, naye akawaogopa. Wakasema: Usiogope! Sisi ni wagombanao wawili, mmoja wetu amemdhulumu mwenziwe. Basi tuhukumu kwa haki, wala usipendelee. Na utuongoe kwenye njia iliyo sawa. 22

image
23. Hakika huyu ndugu yangu ana kondoo wa kike tisiini na tisa; na mimi ninaye kondoo mke mmoja. Akasema: Nipe huyo nikufugie! Na amenishinda kwa maneno. 23

image
24. Akasema: Kweli amekudhulumu kwa kumtaka kondoo wako mmoja kuongezea kwenye kondoo wake. Na hakika washirika wengi hudhulumiana wao kwa wao, isipo kuwa walio amini na wakatenda mema. Na hao ni wachache. Na Daudi akajua kuwa tumemfanyia mtihani. Basi akamwomba msamaha Mola wake Mlezi, na akaanguka kusujudu na kutubia. 24

image
25. Basi tukamsamehe kwa hayo. Naye kwa hakika anao mkaribisho mkubwa na marejeo mazuri kwetu. 25

image
26. Ewe Daudi! Hakika Sisi tumekufanya wewe uwe Khalifa katika nchi. Basi wahukumu watu kwa haki, wala usifuate matamanio yakakupoteza kwenye Njia ya Mwenyezi Mungu. Hakika wanao ipotea Njia ya Mwenyezi Mungu wakaiacha, watapata adhabu kali kwa sababu ya kusahau kwao Siku ya Hisabu. 26

image
27. Na hatukuziumba mbingu na ardhi na viliomo ndani yao bure. Hiyo ni dhana ya walio kufuru. Ole wao walio kufuru kwa Moto utao wapata. 27

image
28. Je! Tuwafanye walio amini na wakatenda mema kama wafanyao uharibifu katika nchi? Au tuwafanye wachamngu kama waovu? 28

image


     29. Na hiki Kitabu, tumekuteremshia wewe, kimebarikiwa, ili wazizingatie Aya zake, na wawaidhike wenye akili. 29

image
 30. Na Daudi tukamtunukia Suleiman. Alikuwa mja mwema. Na hakika alikuwa mwingi wa kutubia. 30

image


31. Alipo pelekewa jioni farasi wasimamao kidete, tayari kutoka shoti;

image
 
 32. Basi akasema: Navipenda vitu vizuri kwa kumkumbuka Mola wangu Mlezi. Kisha wakafichikana nyuma ya boma.

  image
33. Nirudishieni! Akaanza kuwapapasa miguu na shingo.

image


34. Na tulimtia mtihanini Suleiman, na tukauweka mwili juu ya kiti chake, kisha akarejea kwa kutubu.

image
35. Akasema: Mola wangu Mlezi! Nisamehe na unipe ufalme usio mwelekea yeyote baada yangu. Hakika Wewe ndiye Mpaji.

 
image

36. Basi tukaufanya upepo umtumikie, ukenda kwa amri yake, popote alipo taka kufika.

image


37. Na tukayafanya mashet'ani yamtumikie, wote wajenzi na wapiga mbizi.

image
38. Na wengine wafungwao kwa minyororo.

image


39. Hichi ndicho kipawa chetu. Basi toa au zuia, bila ya hisabu.

image


40. Na hakika yeye kwetu Sisi ana cheo cha kukaribishwa kwetu, na pahala pazuri pa kurejea.

image
41. Na mkumbuke mja wetu Ayubu alipo mwita Mola wake Mlezi akasema: Kwa hakika Shet'ani amenifikishia udhia na adhabu. 41

image
42. (Akaambiwa:) Piga-piga ardhi kwa mguu wako! Basi haya maji baridi ya kuogea na ya kunywa. 42

image
43. Na tukampa ahali zake na wengine kama wao pamoja nao, kuwa ni rehema itokayo kwetu, na iwe kumbusho kwa watu wenye akili. 43

image


44. Na shika kicha cha vijiti tu mkononi mwako, kisha ndio upigie nacho, wala usivunje kiapo. Hakika tulimkuta mwenye subira, mbora wa waja, kwa hakika alikuwa mwingi wa kutubu. 44

image


45. Na wakumbuke waja wetu, Ibrahim na Is-haqa na Yaa'qubu walio kuwa na nguvu na busara. 45

image

46. Sisi tumewakhusisha wao kwa sifa ya ukumbusho wa Akhera. 46

image

47. Na hakika wao kwetu sisi ni wateuliwa walio bora. 47

image

48. Na mkumbuke Ismail na Alyasaa na Dhulkifli, na wote hao ni katika walio bora. 48

image

49. Huu ni ukumbusho. Na hakika wachamngu wana marudio mazuri. 49

image

50. Bustani za milele zitazo funguliwa milango yao kwa ajili yao. 50

image

51. Humo wataegemea matakia, wawe wanaagiza humo matunda mengi na vinywaji. 51

image

52. Na pamoja nao wake zao wenye kutuliza macho, hirimu zao. 52

image

53. aya ndiyo mliyo ahidiwa kwa Siku ya Hisabu. 53

image
54. Hakika hii ndiyo riziki yetu isiyo malizika. 54

image
55. Ndio hivi! Na hakika wenye kuasi bila ya shaka watapata marudio maovu kabisa; 55

image
56. Nayo ni Jahannamu! Wataingia humo. Nacho hicho ni kitanda kiovu mno cha kulalia. 56

image
57. Ndio hivi! Basi na wayaonje maji ya moto na ya usaha! 57

image
58. Na adhabu nyenginezo za namna hii. 58

image
59. Hili ndilo kundi litakalo ingia pamoja nanyi. Hapana makaribisho mema kwao. Hakika hao wanaingia Motoni. 59

image
60. Waseme: Lakini nyinyi! Hamna mapokezi mazuri! Nyinyi ndio mlio tusabibisha haya, napo ni pahala paovu kabisa! 60

image
61. Waseme: Mola wetu Mlezi! Aliye tusabibisha haya mzidishie adhabu mara mbili Motoni. 61

image
62. Watasema: Tuna nini hata hatuwaoni wale watu ambao tukiwahisabu ndio katika waovu? 62

image
63. Tulikosea tulipo wafanyia maskhara, au macho yetu tu hayawaoni ? 63

image
64. Hakika hayo bila ya shaka ndiyo makhasimiano ya watu wa Motoni. 64

image
65. Sema: Hakika mimi ni mwonyaji tu; na hapana mungu ila Mwenyezi Mungu Mmoja, Mtenda nguvu, 65

image
66. Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na viliomo baina yake, Mwenye nguvu, Mwenye kusamehe. 66

image
67. Sema: Hii ni khabari kubwa kabisa. 67

image
68. Ambayo nyinyi mnaipuuza. 68

image
69. Sikuwa na ilimu ya mambo ya viumbe wakuu watukufu walipo kuwa wakishindana. 69

image
70. Haikufunuliwa kwangu isipo kuwa ya kwamba hakika mimi ni mwonyaji dhaahiri. 70

image
71. Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitaumba mtu kutokana na udongo.

 
image
72. Na nitakapo mkamilisha na kumpulizia roho inayo tokana nami, basi muangukieni kwa kumt'ii.

 
image
73. Basi Malaika wakat'ii wote pamoja.

 
image
74. Isipo kuwa Iblisi; alijivuna na akawa katika makafiri.

 
image
75. Mwenyezi Mungu akamwambia: Ewe Iblisi! Kipi kilicho kuzuia kumt'ii yule niliye muumba kwa mikono yangu? Je! Umejiona mkubwa, au umekuwa katika wakuu kweli?

 
image
76. Akasema: Mimi ni bora kuliko yeye. Umeniumba kwa moto, na yeye umemuumba kwa udongo.

 
image
77. Akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe umelaanika.

 
image
78. Na hakika laana yangu itakuwa juu yako mpaka Siku ya Malipo.

 
image
79. Akasema: Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watayo fufuliwa viumbe.

 
image
80. Mwenyezi Mungu akasema: Basi umekwisha kuwa miongoni mwa walio pewa muhula,

 
image
81. Mpaka siku ya wakati maalumu. 81

image
82. Akasema (Iblisi): Naapa kwa utukufu wako, bila ya shaka nitawapoteza wote, 82

image
83. Isipo kuwa wale waja wako miongoni mwao walio khitariwa. 83

image
84. kasema: Haki! Na haki ninaisema. 84

image
85. Bila ya shaka nitaijaza Jahannamu kwa wewe na kwa hao wote wenye kukufuata miongoni mwao. 85

image
86. Sema (Ewe Mtume) : Sikuombeni ujira juu ya haya, wala mimi si katika wadanganyifu. 86

image
87. Hayakuwa haya ila ni mawaidha kwa walimwengu wote. 87

image
88. Na bila ya shaka mtajua khabari zake baada ya muda. 88


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani