Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

50.Surat Qaaf


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU 0

image
1. Qaaf. Naapa kwa Qur'ani tukufu!
1

image
2. Bali wanastaajabu kwamba amewafikia mwonyaji kutoka miongoni mwao, na wakasema makafiri: Hili ni jambo la ajabu!
2

image
3. Ati tukifa na tukawa udongo...? Kurejea huko kuko mbali!
3

image
4. Hakika Sisi tunajua kiasi cha kila kinacho punguzwa na ardhi kutokana nao. Na kwetu kipo Kitabu kinacho hifadhi yote.
4

image
5. Lakini waliikanusha Haki ilipo wajia; kwa hivyo wamo katika mambo ya mkorogo.
5

image
6. Je! Hawaangalii mbingu zilizo juu yao! Vipi tulivyo zijenga, na tukazipamba. Wala hazina nyufa.
6

image
7. Na ardhi tumeitandaza na tukaiwekea milima, na tukaiotesha mimea mizuri ya kila namna.
7

image
8. Yawe haya ni kifumbua macho na ukumbusho kwa kila mja mwenye kuelekea.
8

image
9. Na tumeteremsha kutoka mbinguni maji yaliyo barikiwa, na kwa hayo tukaotesha mabustani na nafaka za kuvunwa.
9

image
10. Na mitende mirefu yenye makole yaliyo zaa kwa wingi,
10

image
11. Ili iwe ni riziki kwa waja wangu. Na tukaifufua kwa maji nchi iliyo kuwa imekufa. Kama hivyo ndivyo utakavyo kuwa ufufuaji.
11

image
12. Kabla yao walikadhibisha kaumu ya Nuhu na wakaazi wa Rassi na Thamudi.
12

image
13. Na A'di na Firauni na kaumu ya Lut'i.
13

image
14. Na wakaazi wa Machakani, na watu wa Tubbaa'. Wote hao waliwakanusha Mitume, kwa hivyo onyo likathibitika juu yao.
14

image
15. Kwani tulichoka kwa kuumba mara ya kwanza. Bali wao wamo katika shaka tu juu ya umbo jipya.
15

image
16. Na hakika tumemuumba mtu, nasi tunayajua yanayo mpitikia katika nafsi yake. Na Sisi tuko karibu naye kuliko mshipa wa shingoni mwake.
16

image
17. Wanapo pokea wapokeaji wawili, wanao kaa kuliani na kushotoni.
17

image
18. Hatamki neno ila karibu yake yupo mwangalizi tayari.
18

image
19. Na uchungu wa kutoka roho utamjia kwa haki. Hayo ndiyo uliyo kuwa ukiyakimbia.
19

image
20. Na litapulizwa baragumu. Hiyo ndiyo Siku ya Miadi.
20

image
21. Na kila nafsi itakuja na pamoja nayo mchungaji na shahidi.
21

image
22. (Aambiwe): Kwa hakika ulikuwa umeghafilika na haya; basi leo tumekuondolea pazia lako, na kwa hivyo kuona kwako leo ni kukali.
22

image
23. Na mwenzake atasema: Huyu niliye naye mimi kesha tayarishwa.
23

image
24. Mtupeni katika Jahannamu kila kafiri mwenye inda,
24

image
25. Akatazaye kheri, arukaye mipaka, mwenye kutia shaka,
25

image
26. Aliye weka mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Basi mtupeni katika adhabu kali.
26

image
27. Mwenzake aseme: Ee Mola wetu Mlezi! Sikumpoteza mimi, bali yeye mwenyewe alikuwa katika upotovu wa mbali.
27

image
28. (Mwenyezi Mungu) aseme: Msigombane mbele yangu. Nilikuleteeni mbele onyo langu.
28

image
29. Mbele yangu haibadilishwi kauli, wala Mimi siwadhulumu waja wangu.
29

image
30. Siku tutapo iambia Jahannamu: Je! Umejaa? Nayo itasema: Je! Kuna ziada?
30

image
31. Na Pepo italetwa karibu kwa ajili ya wachamngu, haitakuwa mbali.
31

image
32. Haya ndiyo mnayo ahidiwa kwa kila mwenye kurejea kwa Mwenyezi Mungu na akajilinda.
32

image
33. Mwenye kumwogopa Mwingi wa Rehema hali kuwa hamwoni, na akaja kwa moyo ulio elekea
33

image
34. (Ataambiwa) ingieni kwa salama. Hiyo ndiyo siku ya daima dawamu.
34

image
35. Humo watapata wakitakacho, na kwetu yako ya ziada.
35

image
36. Na kaumu ngapi tuliziangamiza kabla yao walio kuwa na nguvu zaidi kuliko hawa! Nao walitanga tanga katika nchi nyingi. Je! Walipata pa kukimbilia?
36

image
37. Hakika katika hayo upo ukumbusho kwa mwenye moyo au akatega sikio naye yupo anashuhudia.
37

image
38. Na bila ya shaka Sisi tumeziumba mbingu na ardhi na vilio baina yao mnamo siku sita; na wala hayakutugusa machofu.
38

image
39. Basi vumilia kwa hayo wasemayo, na mtakase kwa kumsifu Mola wako Mlezi kabla ya kuchomoza jua na kabla ya kuchwa.
39

image
40. Na katika usiku pia mtakase, na baada ya kusujudu.
40

image
41. Na sikiliza siku atapo nadi mwenye kunadi kutoka pahala karibu.
41

image
42. Siku watakapo sikia ukelele wa haki. Hiyo ndiyo siku ya kufufuka.
42

image
43. Hakika Sisi tunahuisha na tunafisha, na kwetu Sisi ndio marejeo.
43

image
44. Siku itapo wapasukia ardhi mbio mbio! Mkusanyo huo kwetu ni mwepesi.
44

image
45. Sisi tunajua kabisa wayasemayo. Wala wewe si mwenye kuwatawalia kwa ujabari. Basi mkumbushe kwa Qur'ani anaye liogopa onyo.
45


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani