Tarjuma ya Quran Tukufu kwa kiswahili

71.Surat Nuh


image
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
0

image
1. Hakika Sisi tulimtuma Nuh'u kwa watu wake: Uwaonye kaumu yako kabla ya kuwafikia adhabu chungu.
1

image
2. Akasema: Enyi watu wangu! Kwa hakika mimi ni mwonyaji wa dhaahiri kwenu,
2

image
3. Ya kwamba mumuabudu Mwenyezi Mungu, na mumche Yeye, na mumt'ii.
3

image
4. Atakughufirieni madhambi yenu, na atakuakhirisheni mpaka muda ulio wekwa. Hakika muda wa Mwenyezi Mungu utapo fika haucheleweshwi. Laiti mngejua!
4

image
5. Akasema: Ee Mola wangu Mlezi! Hakika mimi nimewaita watu wangu usiku na mchana,
5

image
6. Lakini wito wangu haukuwazidisha ila kukimbia.
6

image
7. Na hakika mimi kila nilipo waita ili upate kuwaghufiria, walijiziba masikio yao kwa vidole vyao, na wakajigubika nguo zao, na wakakamia, na wakatakabari vikubwa mno!
7

image
8. Tena niliwaita kwa uwazi,
8

image
9. Kisha nikawatangazia kwa kelele, tena nikasema nao kwa siri.
9

image
10. Nikasema: Ombeni msamaha kwa Mola wenu Mlezi; hakika Yeye ni Mwingi wa kusamehe.
10

image
11. Atakuleteeni mvua inyeshe mfululizo.
11

image
12. Na atakupeni mali na wana, na atakupeni mabustani na atakufanyieni mito.
12

image
13. Mna nini hamweki heshima ya Mwenyezi Mungu?
13

image
14. Na hali Yeye kakuumbeni daraja baada ya daraja?
14

image
15. Kwani hamwoni jinsi Mwenyezi Mungu alivyo ziumba mbingu saba kwa matabaka?
15

image
16. Na akaufanya mwezi ndani yake uwe nuru, na akalifanya jua kuwa taa?
16

image
17. Na Mwenyezi Mungu amekuotesheni katika ardhi kama mimea.
17

image
18. Kisha atakurudsheni humo na atakutoeni tena.
18

image
19. Na Mwenyezi Mungu amekukunjulieni ardhi kama busati.
19

image
20. Ili mtembee humo katika njia zilizo pana.
20

image
21. Nuh'u akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika hao wameniasi, na wamemfuata yule ambaye mali yake na wanawe hawakumzidishia ila khasara.
21

image
22. Na wakapanga vitimbi vikubwa.
22

image
23. Na wakasema: Msiwaache miungu yenu, wala msimwache Wadda wala Suwaa' wala Yaghutha, wala Yau'qa, wala Nasra.
23

image
24. Na hao walikwisha wapoteza wengi, wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.
24

image
25. Basi kwa ajili ya makosa yao waligharikishwa wakaingizwa Motoni, wala hawakuwapata wa kuwanusuru badala ya Mwenyezi Mungu.
25

image
26. Na Nuh'u akasema: Mola wangu Mlezi! Usimwache juu ya ardhi mkaazi wake yeyote katika makafiri!
26

image
27. Hakika ukiwaacha watawapoteza waja wako, wala wao hawatazaa ila waovu makafiri.
27

image
28. Mola wangu Mlezi! Nighufirie mimi na wazazi wangu, na kila aliye ingia nyumbani mwangu kuwa ni mwenye kuamini, na Waumini wote wanaume, na Waumini wanawake. Na wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea.
28


Imetarjumiwa na Sheikh Ali Muhsin Al-Barwani
Ikiwa una ushauri au maoni juu ya tarjuma hii, andika kwa anwani hii qurani-tukufu@geocities.com 
Copyright � 22 August 1997, Sheikh Ali Muhsin Al Barwani