1. Sema: Najikinga na Mola Mlezi wa wanaadamu, Mwenye kuendesha mambo yao.

 

2. Mfalme wa wanaadamu, kwa ufalme ulio timia, kuwamiliki wote wafalme wao na maraia.

3. Mungu wa  wanaadamu, Mwenye uweza kwa kuwasarifu kwa ukamilifu atakavyo.

 

4. Na shari ya mwenye kutia wasiwasi watu, ambaye hurudi nyuma ukiomba msaada kwa Mwenyezi Mungu dhidi yake.

 

5. Ambaye hutia kwa kificho katika vifua vya watu ya kuwaachisha wasende kwenye njia ya uwongofu.

 

6. Kutokana na majini na wanaadamu.