1. Unamjua anaye kanusha malipo na hisabu ya Akhera?
2,3. Ukitaka kumjua basi ni huyo ambaye anaye msukuma
yatima kwa nguvu, na anamtumilia mabavu, na anamdhulumu, na wala hahimizi
kulishwa masikini.
4,5. Maangamio yatawashukia wanao sali na wakasifika
kwa sifa hizi, na wakaghafilika na Sala zao wasinafiike nazo.
6. Ambao huonyesha kwa watu vitendo vyao, ili wapate cheo
katika nyoyo za hao watu, na wasifiwe.
7. Na huku wanazuia hisani zao na msaada wao kwa watu.